• Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Machapisho
    • Taarifa za Mapato
    • Majarida
    • Fomu Mbali mbali
    • Presentations
  • Miongozo
    • Miongozo OR TAMISEMI
    • Miongozo ya mradi wa SEQUIP
    • Green and Smart Cities
    • Miongozo ya Kilimo
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Michoro ya Ujenzi
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)

Waziri Jafo Awaaga wana OR TAMISEMI

Imewekwa tar.: August 21st, 2020

Na Fred Kibano

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR TAMISEMI) Selemani Jafo amewashukuru wanafamilia ya Ofisi ya Rais TAMISEMI kwa kumpa ushirikiano mzuri kipindi alichohudumu katika wizara hiyo.

Waziri Jafo ameongea katika hafla fupi ya chakula cha jioni aliyoiandaa binafsi kwa ajili ya kuwaaga Viongozi na watumishi wa wizara hiyo huku akisema ushirikiano mkubwa ndio chanzo cha yeye kuhudumu mpaka hatua aliyofikia hali akimsaidia Mhe. Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli.

“nakushukuru sana Katibu Mkuu Mhandisi Joseph Nyamhanga na timu yako mmekuwa mstari wa mbele katika kunisaidia kwenye majukumu mbalimbali ambayo nimeyatekeleza katika Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa”

Jafo amesema wizara hiyo ambayo ina majukumu lukuki ni wizara ngumu na yenye matatizo mengi kwani inahusu maisha ya kila siku ya Watanzania na hanabudi kuwashukuru Viongozi wa wizara hiyo na watumishi ambao wamekuwa mstari wa mbele katika kutekeleza majukumu yake bila hata kujali umri wao.

“wengi hamkujalisha umri wenu wakati mkifanya kazi nami, pia madaraka niliyopewa na Mhe. Rais nikiwa kijana mmdogo, kazi tuliyoifanya katika miaka mitano ni kazi kubwa sana na huwezi kupata mafanikio kama huna timu work (timu ya kufanya kazi pamoja)”,alisema Jafo.

Aidha amesema anaendelea na mchakato wa kuomba ridhaa kwa watanzania ambao watampigia kura kuwa mbunge waa Kisarawe lakini yeye binafsi angependelea kuendelea na wizara hii ambayo amepata ushirikiano mkubwa kutoka kwa Watendaji na watumishi na hivyo kama akipewa nafasi ya kuingia katika Baraza la Mawaziri na na kama ikimpendeza Mhe. Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli amrudishe katika wizara hiyo ya Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa.

Katibu Mkuu Ofisi yaRais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhandisi Joseph Nyamhanga amemshukuru kwa kualikwa wanafamilia wa ofisi yake na kwamba ofisi hiyo wiki mbili zilizopita iliadhimisha  wiki ya Ofisi ya Rais  Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa kwa kuonyesha mafanikio ya sekta ya Afya, Elimu, Miundombinu ambayo waziri Jafo amekuwa chachu ya mafanikio hayo.

Mhandisi Nyamhanga amesema angependa waziri Jafo arudi katika wizara hii lakini jambo hilo hana mamlaka nalo lakini pia kama hatorudi basi maombi yake ni kupata nafasi kubwa zaidi.

“Jafo ana maono ya mbali na usipokuwa makini atakuacha mbali sana tumekuwa na mafanikio makubwa chini ya uongozi wake, pongezi pia natoa kwa Mheshimiwa Mwita Waitara na Mheshimiwa Josephat Kandege kwa kushind kura za maoni kwenye majimbo yao ya uchaguzi na kuteuliwa na chama kugombea ubunge”

Aidha, Nyamhanga amesema Mhe. Jafo atakuwa jimboni mwake kwa muda mrefu na kwamba cheo chake cha uwaziri kitaendelea kuwepo mpaka masaa machache ya kuapishwa kwa Rais Mteule baada ya kutangazwa matokeo.

Kwa upande wake Bwana Tixon Nzunda Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu ameshukuru Mhe. Jafo kwa kuonyesha upendo na kuwaleta pamoja wanafamilia ya Ofisi ya Rais TAMISEMI na kuwa amejifunza mambo mengi kutoka kwake.

“wewe ni mtu mwemwa sana na kama kufanya kazi kama timu wakati wote ulituleta pamoja wana TAMISEMI pamoja na Viongozi wengine na kuamini kuwa kila mmoja ana mchango katika taasisi, niseme tu Mheshimiwa Waziri unayo bidii ya kazi, unaonekana mdogo lakini unafikiria mambo makubwa kwa wizara hii na umejenga heshima kubwa kwako na Watanzania”

Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma Kessy Maduka amesema kwamba tangu alipokuwa Waziri amewaunganisha watu wote na kuwakomaza kwa kuwapa matumaini na kuwafanya  kuwa watendaji.

Winfrida Rutaindurwa Katibu Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC) amemsimulia Jafo kama mtendaji ambaye hataki Viongozi kukaa maofisini bali kwenda maeneo ya kazi na kufanya ufuatiliaji wa kina ili kupata matokeo.

“namkumbuka waziri Jafo pale aliposema, msikae ofisini bali nendeni sight (maeneo ya kazi) mkajionee na kufanya kazi huko, pia bajeti ya Tume ya TSC imepanda sana kwa kuipigania na inasaidia uendeshaji wa ofisi yetu ukilinganisha na kipindi kilichopita, tunatoa pongezi pia kwa ujenzi wa Mji wa Serikali Mtumba jengo limejengwa vizuri”

Akitoa neon la shukrani Asifiwe Makweta ambaye ni Afisa Tawala Idara ya Tawala za Mikoa Ofisi ya Rais TAMISEMI amesema, “katika utendaji wako wa kazi umesisitiza kufanya kazi kwa weledi na kuacha kufanya kazi kwa mazoea, tumeweza kufanya wizara mpya kupitia wewe, umefanya TAMISEMI kujulikana sana”

Katika hafla hiyo walihudhuria Viongozi wa wizara, Wakuu wa Idara na Vitengo, Wakuu wa Taasisi zilizopo chini ya Ofisi ya Rais TAMISEMI ambazo ni Bodi ya Mikopo ya Serikali za Mitaa, DART, Chuo cha Serikali za mitaa Hombolo, Shirika la Masoko Kariakoo, Shirika la Elimu Kibaha na TARURA.


Matangazo

  • Orodha ya waliopata vibali vya Uhamisho Septemba - Disemba 2022 (OR - TAMISEMI) January 21, 2023
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kidato cha Kwanza Waliorudia Mtihani January 15, 2023
  • Matumizi ya Lugha ya Kiswahili na Kingereza January 14, 2023
  • Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Kwanza 2023 December 14, 2022
  • Orodha ya Waliopangwa kwenye Vituo vya Kazi Kada za Afya (Awamu ya Pili) Agosti 2022 August 30, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA KWA KADA ZA AFYA (Marudio) July 20, 2022
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • LAAC YAPOKEA TAARIFA KUHUSU UTAWALA NA UENDESHAJI WA MAMLAKA ZA SERIKALI ZA MITAA

    March 14, 2023
  • SERIKALI YAWEKA MIKAKATI KATIKA USIMAMIZI WA MIRADI YA MENDELEO, UKUSANYAJI NA UDHIBITI WA MAPATO KATIKA HALMASHAURI

    March 13, 2023
  • WAUGUZI NA WAKUNGA WATAKIWA KUSIMAMIA MAADILI YA KAZI

    March 13, 2023
  • ACHENI KUTUMIANA NYARAKA ZA SERIKALI KWENYE MITANDAO YA KIJAMII NA BARUA PEPE BINAFSI - DKT. MPANGO

    March 13, 2023
  • Angalia zote

Video

Taarifa ya Ukusanyaji wa Mapato ya Halmashauri, kipindi cha robo ya pili ya mwaka wa fedha 2021/22
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.