Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

Wananchi watakiwa kushiriki Ujenzi wa Hospitali za Wilaya.

Imewekwa tar.: March 11th, 2019


Wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino, katika kijiji cha Mlowa Barabarani wametakiwa kutoa ushirikikiano katika ujenzi wa Hospitali ya Wilaya hiyo ili kuleta maendeleo na kupunguza changamoto za afya nchini.

Hayo yamebainishwa na Naibu Katibu Mkuu Afya kutoka Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI), Dkt.Dorothy Gwajima wakati wa ziara ya kikazi ya kukagua utendaji kazi wa vituo vya afya vya Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino Jijini Dodoma.

Dkt. Gwajima amesema kuwa Serikali pekee haiwezi kufanikiwa katika kuleta maendeleo bila kuwepo ushirikiano kutoka kwa wananchi wake hivyo ni vyema wananchi wakashirikishwa kikamilifu katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo nchini.

Amesema Serikali imejenga miundombinu ya afya nchini ikiwa na lengo la kuhakikisha huduma za afya zinaboreka kuanzia ngazi ya Zahanati, Vituo vya afya, Hospitali za Mikoa ili kupunguza changamoto katika sekta ya afya.

Akiendelea kufafanua amesema kuwa  wananchi wanatakiwa kuwa na dhamira ya dhati ya kusimamia  miradi ya ujenzi wa Hospitali za Wilaya    ili zijengwe  kwa ubora  kulingana na  fedha zilizotolewa na Serikali.

“Wananchi hakikisheni mnasiamia ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Chamwino kwa umakini mkubwa kwa kuangalia gharama zinazotumika zinaenda sambamba na majengo yanayojengwa kwa kuwa Hospitali hizi ni mali ya wananchi” Amesisistiza Gwajima

Akifafanua kuhusu ubora wa huduma zinazotolewa kwenye vituo vya afya amesema Serikali imejenga miudombinu ya afya nchini lakini bado changamoto kubwa ni watendaji waliopo katika vituo hivyo kutotimiza majukumu yao kwa uadilifu katika kutoa huduma bora kwa jamii hali ambayo inasababisha wananchi wengi kutokufika katika vituo hivyo.

“ Baadhi ya watoa huduma wamekuwa na lugha chafu kwa wateja, kutokuwa na ukarimu, kutowajibika kikamilifu, uzembe, rushwa ambapo  vitu vyote hivi vinapelekea wananchi kutokuja kutibiwa kwenye vituo vya afya vya Serikali na kukimbilia  vituo binafsi, naagiza watoa huduma wote nchini kuhakikisha wanafanyakazi kwa weledi katika kuwahudumia wananchi” Amesema Gwajima

Aidha amewataka wananchi kuhakikisha wanatoa taarifa pale wanapojibiwa vibaya na watoa huduma za afya nchini na Serikali haitasita kuwachukulia hatua za kinidhamu watumishi wote watakaobainika kuwa na makosa.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Chamwino, Athuman Masasi amesema kuwa watahakikisha wanakamilisha ujenzi wa Hospitali ya Wilaya hiyo kwa wakati ili wananchi waanze kupata huduma.

 



Matangazo

  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert (extension) 1 May 28, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert (extension) May 28, 2025
  • TOR - Msimbazi Watershed Management – Modelling May 26, 2025
  • Monitoring & Support, TOR - DMDP 2 SWM Service Framework & Delivery System in Dar May 26, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • Mhe. Katimba awapokea Wabunge wa Zambia waliokuja kujifunza kuhusu Usimamizi na Uendeshaji wa Mamlaka za Serikali za Mitaa Tanzania Bara

    May 28, 2025
  • Mtwale Atoa Mwongozo kwa Makatibu Tawala Wasaidizi wa Mikoa

    May 27, 2025
  • Nipo tayari kufanya kazi pamoja nanyi kufikia malengo ya Mhe. Rais – Prof. Tumaini Nagu

    May 26, 2025
  • TARURA IMEKUWA NA MCHANGO MKUBWA KWA SERIKALI YA AWAMU YA SITA

    May 26, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.