Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

Wananchi waipongeza Serikali kwa kujenga Vituo vya afya wataka huduma ziboreshwe.

Imewekwa tar.: July 30th, 2019

Wananchi wa Kijiji cha Mpwayungu  kata ya Mpwayungu,  Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino Mkoani Dodoma  wamemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  kwa kuwajengea  miundombinu ya afya  ambayo imesaidia kuboresha huduma za afya  katika kijiji hicho.

 Wakiongea leo wakati wa ziara ya kikazi ya kukagua ujenzi wa miundombinu ya afya na hali ya utoaji wa huduma  za afya katika kijiji hicho iliyofanywa na   Naibu Katibu Mkuu kutoka Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa anayeshughulikia Afya Dkt. Dorothy Gwajima wananchi hao wamesema, kabla ya kujengewa miundombinu ya afya hali ya utoaji wa huduma za afya ilikuwa mbaya kiasi ambacho walikuwa wakifuata huduma hiyo katika Hospitali ya Mvumi

Akiongea kwa niaba ya wananchi wa kijiji hicho Mwenyekiti wa Kamati ya Usimamizi wa Kituo cha Afya cha Mpwayungu Bw. Chibwele Magubika amesema, awali hali ya utoaji wa huduma za afya katika kituo hicho zilikuwa duni kiasi ya kwamba wananchi wengi walikuwa wakikimbilia kupata huduma hizo katika Hospitali ya Misheni Mvumi au Hospitali ya Mkoa wa Dodoma.

Bw. Magubika ameishukuru Serikali kwa kujenga miundombinu ya afya na kuboresha huduma za afya kwa wananchi ila ameiomba Serikali ihakikishe huduma hizo zinaboreshwa na kwamba, watumishi wanakuwa na lugha nzuri kwa wateja na kufanya kazi kwa weledi ili wananchi wengi waweze kuvutiwa na utoaji wa huduma katika kituo hicho.

 “Inasikitisha kuona Serikali imewekeza fedha nyingi katika ujenzi wa  miundombinu ya afya yakiwemo majengo mazuri makubwa na yenye kuvutia lakini baadhi ya watumishi bado wanakuwa na lugha chafu ambazo haziwavutii wananchi kuja kupata huduma kwenye vituo kama hivi” Amesema Magubika.

Ameendelea kufafanua kuwa kuna baadhi ya watumishi hapa ni watovu wa nidhamu, wana lugha chafu kabisa, hawana maadili katika utendaji kazi wao, wanalewa pombe, hawatoi huduma kwa wakati jambo ambalo linakatisha tamaa wananchi kufika kupata huduma.

Naye Afisa Mtendaji wa Kijiji cha Mpwayungu Selemani Kibakaya amesema kuwa, huduma zikiboreshwa, watumishi wakafanya kazi kwa ushirikiano bila kutegeana itasaidia kupunguza changamoto mbalimbali zinazojitokeza ikiwemo ya utoaji wa huduma bora kwa wananchi,

Amewataka wafanyakazi kuhakikisha wanatoa huduma kwa wakati, kwa kuwajali wagonjwa ili kuweza kupunguza msongamano pamoja na wananchi kukaa muda mrefu kusubiri huduma za afya jambo ambalo linakatisha tamaa ya kupata huduma za afya.

Wakati huohuo Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa anayeshughulikia Afya Dkt. Dorothy Gwajima amawaagiza Waganga Wakuu wa Mikoa na Wilaya kuhakikisha wanafanya ufuatiliaji wa kero wanazopata wananchi wakati wa kufika kwenye vituo vya huduma kwa kuongea na wateja, viongozi wa serikali ya kijiji na Wajumbe wa Kamati ya Usimamizi wa Kituo wanaowawakilisha wananchi kwenye uongozi wa kituo.

Vilevile, Dkt, Gwajima amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri kuhakikisha wanachukua hatua stahiki kwa wakati pale wanapopelekewa malalamiko siyo tena nao wanakaa miezi 6 bila kuchukua hatua kama ilivyotokea kituoni hapo.

Dkt Gwajima amesema, ukosefu wa hatua stahiki dhidi ya kero zinazoripotiwa na wananchi ndiyo mojawapo ya mambo yanayowakwaza wananchi na kuamua kutotumia vituo husika au kuamua wanavyoona wao inafaa.

 “CHMT NA RHMT hakikisheni mnafuatilia na kusimamia  utendaji kazi wa watumishi katika vituo vya kutolea huduma, kutoa msaada na ushauri wa kitaalamu pia, kusikiliza kero za wananchi dhidi ya huduma na katika kila jambo, kuchukua hatua stahiki kwa wakati na bila kuonea upande wowote ule. Msisubiri hadi Wizara itembelee ndiyo iibue hizi kero na nyie mpo huku.

Amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino kuhakikisha anafanyia kazi malalamiko ya wananchi na kuchukua hatua stahiki za kiutumishi dhidi ya mtumishi Claude Chilala ambaye anatuhumiwa na wananchi kukiuka maadili ya kiutumishi na kuwa kero sugu kwa wateja.

Dkt. Gwajima amewapongeza watumishi wengine ambao wananchi wamekiri kuwa hawana shida ukilinganisha na huyo anayelalamikiwa na kila mteja.

Aidha amewataka watumishi kutoiga tabia ambazo zinakiuka maadili ya utumishi wa umma na kwamba, washirikiane daima vinginevyo, mambo yakiharibika inaweza ikawa vigumu kutowajibika kwa namna moja au ingine.

Na. Angela Msimbira OR-TAMISEMI


 



Matangazo

  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert (extension) 1 May 28, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert (extension) May 28, 2025
  • TOR - Msimbazi Watershed Management – Modelling May 26, 2025
  • Monitoring & Support, TOR - DMDP 2 SWM Service Framework & Delivery System in Dar May 26, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • Mhe. Katimba awapokea Wabunge wa Zambia waliokuja kujifunza kuhusu Usimamizi na Uendeshaji wa Mamlaka za Serikali za Mitaa Tanzania Bara

    May 28, 2025
  • Mtwale Atoa Mwongozo kwa Makatibu Tawala Wasaidizi wa Mikoa

    May 27, 2025
  • Nipo tayari kufanya kazi pamoja nanyi kufikia malengo ya Mhe. Rais – Prof. Tumaini Nagu

    May 26, 2025
  • TARURA IMEKUWA NA MCHANGO MKUBWA KWA SERIKALI YA AWAMU YA SITA

    May 26, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.