Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

Waganga Wakuu wa Mikoa wapewa mwezi mmoja kutathmini utendaji wa Kamati za afya za Mikoa na Wilaya zao

Imewekwa tar.: May 5th, 2019

Waganga wakuu wa Mikoa Tanzania Bara wamepewa mwezi mmoja kuhakikisha kuwa wanazifanyia tathmini ya kina Kamati za Uendeshaji Huduma za Afya za Mikoa na Wilaya zao kuona kama zinaendana na kasi ya mabadiliko yanayokusudiwa na Serikali ya Awamu ya Tano.

Agizo hilo limetolewa jana mjini Songea na Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa TAMISEMI anayeshughulikia Afya Dkt. Dorothy Gwajima wakati akizungumza na Wajumbe wa Kamati ya Uendeshaji Huduma za Afya ya Mkoa wa Ruvuma pamoja na Wajumbe wa Kamati za Uendeshaji Huduma za Afya kutoka Halmashauri ya Namtumbo, Halmashauri ya Wilaya ya Songea pamoja na Manispaa ya Songea.

Amesema anawapa siku 30 Waganga Wakuu wa Mikoa yote kuhakikisha kuwa wanafanya tathmini ya Wajumbe waliopo katika ofisi zao kama wanatosha kuendelea na nyadhifa zao za kusimamia jukumu la uendeshaji huduma za afya katika mikoa na halmashauri zao.

Dkt Gwajima ameongeza kuwa endapo itabainika kuwa baadhi ya Wajumbe wa Kamati hizo hawana sifa zinazowafanya kushindwa kutekeleza majukumu yao ya usimamizi na uendeshaji huduma za afya katika maeneo yao, Waganga Wakuu wa Mikoa watalazimika kuwaweka pembeni Wajumbe hao na kuunda upya Kamati ambazo zitaweza kuiendeleza agenda ya mabadiliko katika sekta ya afya.

“Kinyume na hapo katika ziara hizi ninazoendelea kuzifanya mikoani nikikuta yupo Mganga Mkuu wa Mkoa ambaye ametulia tu, mapungufu katika vituo bado yapo na amewezeshwa na Serikali, ajue wazi kuwa wa kutokutosha wa kwanza atakuwa yeye,” amesema Dkt Gwajima na kuongeza:

“Haiwezekani tukute mapungufu madogo kabisa katika vituo, ambayo yangeweza kuonwa na wao walioko huko eti hayaonekani hadi tuje sisi kutoka Tamisemi ndiyo mapungufu hao yafanyiwe kazi,”amesisitiza Dkt Gwajima.

Naibu Katibu Mkuu huyo ameonya tabia iliyojengeka miongoni mwa Wajumbe wa Kamati za Uendeshaji Huduma ya Afya kukimbilia kuomba msamaha pindi zinaposhindwa kutekeleza majukumu yake kwa makusudi.

Amesema huu ni wakati wa kuboresha sekta ya afya katika vituo vya afya na zahanati kwa kuhakikisha kuwa mazingira ya utoaji huduma yanaboreshwa ili yaweze kuwavutia wananchi wengi kukimbilia kupata huduma katika zahanati na vituo vya afya vinavyomilikiwa na serikali ikiwemo hospitali za halmashauri.

Dkt Gwajima amesema kuwa kamwe hatawapa nafasi Wajumbe wa Kamati za Uendeshaji Huduma za Afya wa Mikoa na Wilaya ambao siku zote wamekuwa ni watu wa visingizio vya kuomba kusamehewa ama kupewa muda kuwa wamefahamu mapungufu yao wakati mapungufu husika ni yale yale ambayo kila siku Serikali inatoa maelekezo kuwa yafanyiwe kazi.

Amesema angependa kuona Kamati za Uendeshaji Huduma za Afya katika Mikoa na Halmashauri zikijikita katika kuongelea mambo ya ubora wa huduma kwa mteja “’quality care” na kuwa, mteja ni mfalme na si vinginevyo. Serikali imeshirikisha Wananchi na kutuwezesha miundombinu safi na dawa za kutosha, bajeti ya kufuatilia huduma inatolewa, semina za uongozi zinafanyika, maelekezo yanatolewa je, tatizo huwa linatokea wapi?

“Hivi vitu vidogo vidogo vya kitaalamu tubebe sisi wenyewe, Wananchi wametuunga mkono, tumeweza kushirikiana nao kujenga zahanati na vituo vya afya katika mikoa na halmashauri zetu hivyo ni jukumu letu sasa kuhakikisha kuwa tunatoa huduma bora za afya kwa Wananchi na kuondoa hii tabia ya kuwepo kwa malalamiko yanayosababishwa na uzembe katika kufuatilia na kusimamia,” amesema.

Kwa mujibu wa Dkt.Gwajima, katika ziara zake alizokwisha zifanya katika mikoa ya Morogoro, Dodoma, Njombe na Songea amejionea mapungufu mbalimbali ya utoaji wa huduma bora za afya katika vituo vya afya na zahanati ambayo yapo ndani ya uwezo wa Kamati za Usimamizi na Uendeshaji Huduma za Afya katika mikoa na halmashauri husika.

Ameongeza kuwa mapungufu hayo ambayo ameyashuhudia kwenye vituo vya afya na zahanati zinazomilikiwa na umma yametokana na watoa huduma waliopo katika vituo hivyo kutopata usimamizi unaostahili kutoka kwa Kamati za Usimamizi na Uendeshaji wa Huduma za Afya za Mikoa na Halmashauri husika.

Dkt Gwajima anaamini kuwa, kushindwa kwa Kamati za Uendeshaji na Usimamizi wa utoaji huduma za afya katika ngazi za mikoa na halmashauri kutekeleza majukumu yao, ndiko kulikopelekea kukithiri kwa uchafu katika majengo ya vituo vya afya na zahanati, kushindwa kufanyiwa matengenezo muhimu ya kuboresha mazingira ya zahanati na vituo hivyo licha ya vituo hivyo kuwa na fedha za uendeshaji wake.

 “Unakuta kituo kina fedha za kutosha kwenye akaunti lakini mapungufu madogo madogo ya kukera yamejaa,” ameeleza Naibu Katibu Mkuu.

Amesema hali hiyo imesababishwa na kushindwa kwa Kamati za Uendeshaji Huduma za Afya za Mkoa (RHMT) na zile za Halmashauri (CHMT) kwa kutofanya kazi ya ufuatiliaji wa utoaji huduma bora na utaalam kwenye vituo vya afya nchini licha ya kuwezeshwa na Serikali.

Sambamba na kuwataka Waganga Wakuu wa Mikoa kuzitathmini Kamati hizo, Dkt Gwajima pia amewataka wajumbe wa Kamati hizo kutambua kuwa, Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt John Pombe Magufuli ipo na agenda moja tu ya kuleta mabadiliko katika sekta ya afya na kuwagusa watumiaji wa huduma hizo kwa huduma zenye ubora unaostahili.

“Hatutapimwa kwa idadi ya semina au uwepo wa kituo cha afya tu karibu na Wananchi bali kwa ubora huduma zinazotoleewa katika vituo hivi, vinginevyo Wananchi watakuwa karibu na vituo husika lakini hawavitumii,” amesema.

Dkt Gwajima amebainisha mapungufu kadhaa aliyoyaona kwenye ziara yake kuwa ni pamoja na Kamati za Uendeshaji Huduma ya Afya kushindwa kuzifanyia kazi changamoto mbalimbali zinazojitokeza kwenye vituo vyao vya afya na zahanati, kuwepo kwa malalamiko toka kwa wagonjwa, kukosekana kwa takwimu sahihi za utendaji kazi na Wajumbe wa Kamati za uendeshaji huduma za Afya kushindwa kuandika vizuri kumbukumbu za taarifa za kazi za ikiwemo mihutasari ya vikao na wengine kutokaa kabisa vikao muhimu.

Akiwa katika kituo cha afya Mjimwema Manispaa ya Songea Naibu Katibu Mkuu Dkt.Gwajima alipokea kero za wagonjwa kuhusu uwepo wa kauli mbaya toka kwa baadhi ya watumishi wakiwemo wauguzi na matabibu, tatizo la ukosefu dawa na vifaa tiba muhimu hususan vya akina mama wajawazito.

“Hapa Mjimwema nimebaini kasoro nyingi mojawapo kauli mbaya za watumishi na tatizo la dawa na vifaa tiba kwa wagonjwa ” ameonya Dkt .Gwajima.

Aidha, alimpongeza tabibu msaidizi mmoja aliyeibuliwa na mteja kwamba, anatamani watoa huduma wote wangekuwa kama tabibu huyo anayeitwa Lidya Mwakyusa Hii ni mara ya pili kwa wateja kuwataja hadharani watumishi watoa huduma wenye huduma inayojali mteja akiwemo Edward Mapunda wa Kituo cha Afya cha Halmashauri ya Njombe.

Dkt. Gwajima amewapongeza watoa huduma wanaotambua wajibu wao kuwa, mteja ni mfalme na amewataka kutovunjwa moyo na baadhi ya watumishi wasiozingatia maadili ya kazi na kuleta kero kwa wateja.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Dkt. Jairy Khanga ameahidi kuchukua hatua za mapema kufanya mabadiliko ya utendaji kazi wa Kamati za Usimamizi wa Huduma za Afya katika Mkoa wa Ruvuma

Anaandika Mathew Kwembe Songea,

Matangazo

  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert (extension) 1 May 28, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert (extension) May 28, 2025
  • TOR - Msimbazi Watershed Management – Modelling May 26, 2025
  • Monitoring & Support, TOR - DMDP 2 SWM Service Framework & Delivery System in Dar May 26, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • Mhe. Katimba awapokea Wabunge wa Zambia waliokuja kujifunza kuhusu Usimamizi na Uendeshaji wa Mamlaka za Serikali za Mitaa Tanzania Bara

    May 28, 2025
  • Mtwale Atoa Mwongozo kwa Makatibu Tawala Wasaidizi wa Mikoa

    May 27, 2025
  • Nipo tayari kufanya kazi pamoja nanyi kufikia malengo ya Mhe. Rais – Prof. Tumaini Nagu

    May 26, 2025
  • TARURA IMEKUWA NA MCHANGO MKUBWA KWA SERIKALI YA AWAMU YA SITA

    May 26, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.