• Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Machapisho
    • Taarifa za Mapato
    • Majarida
    • Fomu Mbali mbali
    • Presentations
  • Miongozo
    • Miongozo OR TAMISEMI
    • Miongozo ya mradi wa SEQUIP
    • Green and Smart Cities
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Michoro ya Ujenzi
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
    • Machaguo Kidato cha 5 & Vyuo

Viongozi wa Mikoa na Halmashauri wapewa wiki mbili kuandaa orodha ya Majengo

Imewekwa tar.: February 5th, 2021

Na Atley Kuni, Dodoma

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo amewapa wiki mbili Viongozi wa Sekretarieti za Mikoa, na Mamlaka za Serikali za Mitaa kuhakikisha kuwa ndani ya wiki mbili kuanzia sasa wawe wamesimika mfumo wa kutambua orodha ya majengo na mabango yaliyopo katika maeneo yao ili kurahisisha ukusanyaji wa kodi na ushuru.

Akizungumza wakati wa kikao kilicho wakutanisha, Makatibu Tawala wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa nchini leo jijini Dodoma, Mhe. Jafo amesema, changamoto kubwa ambayo inasababisha zoezi la ukusanyaji kodi za majengo ni kutokuwepo kwa orodha kamili ya majengo katika mamlaka husika.

Hivyo, amesema suluhu ya kudumu itakayosaidia kuyabaini kwa wepesi na kurahisisha ukusanyaji wa kodi za majengo na ushuru wa mabango ni kuwepo kwa mfumo utakaosaidia kuyabaini majengo yote na mabango na kuhifadhi kumbukumbu hizo katika Kompyuta.

“Tunataka kuanzia tarehe 05 hadi 28 Februari, 2021, iwe ni kazi ya kubainisha majengo yote yanayopaswa na ambayo yanakidhi kulipiwa kodi,” amesema Waziri Jafo na kuongeza kuwa nyumba za matope zimeondolewa katika utaratibu huu.

“Kila Mtendaji wa Mtaa, Mwenyekiti wa Kijiji anatakiwa kuwa na takwimu za majengo yote yanayopaswa kulipiwa kodi, Mkurugenzi hakikisha kuwa Mtendaji wako wa Kijiji au Mtaa anakupatia takwimu ndani ya Wiki mbili kuanzia leo,” alisisitiza Mhe. Jafo.

Waziri Jafo amesema, Wakurugenzi wa Halmashauri watatakiwa kuwasilisha kanzi data hizo ngazi ya Wilaya kwa ajili ya uhakiki kwa Mkuu wa Wilaya, kabla ya kuwasilisha ngazi ya Mkoa kwa Katibu Tawala wa Mkoa na ifikapo tarehe 04 Machi, 2021 zoezi hilo liwe limekamilika na taarifa ya majumuisho iwe imetumwa kwa Katibu Mkuu TAMISEMI.

Waziri amesisitiza kuwa, taarifa hizo zitatakiwa kuanisha nyumba, mmiliki na mawasiliano yake kwa wepesi wa rejea, ambapo mara baada ya hapo, itafanyika kampeni maalum ya kuanza kukusanya kodi ya majengo nchi nzima, itakayoanza tarehe 22 Machi hadi tarehe 05 Aprili, 2021.

“Tunataka huko mbeleni hizi Mamlaka za Serikali za Mitaa ziweze kufanya baadhi ya shughuli za Maendeleo zenyewe, hivyo katika zoezi hili tutaweka mfumo maalum utakaoweza kuona mambo kadhaa yanayo endelea nchi nzima kwenye kazi hii, hatutaki watu washindane bali tunataka kila Halmashauri iwe ya kwanza,” amesema Mhe. Jafo.

Kuhusu vitambaulisho vya wajasiriamali, Waziri Jafo, amesema tayari vitambulisho million 1.6 vimechapishwa na mamlaka ya Mapato Tanzania na kusambazwa katika Mikoa.

“Huu ndio mwanzo na maelekezo ya Serikali, ambayo yatakuwa katika makundi matatu, Wafanya Biashara wakubwa wanaolipa kodi TRA, Wafanyabishara wa kati wenye Leseni za Halmashauri na kundi la tatu ni wenye Vitambulisho vya Mjasiriamali, kila mmoja wetu lazima awe sehemu ya kundi moja wapo” amesema Waziri Jafo

Amesema kuwa asiyekuwa na kitambulisho au hana kundi lolote kati ya hayo, asiruhusiwe kufanya biashara.

Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha, Aldolf Ndunguru amesema pamoja na kwamba zoezi la kukusanya kodi hizo limehamishiwa Mamlaka za Serikali za Mitaa bado anaamini ushirikishwaji madhubuti wa viongozi katika maeneo mbali mbali utawezesha kukabiliana na mianya ya upotevu wa mapato ya Serikali.

Akitoa salamu za Mamlaka ya Mapato nchini, Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato nchini TRA, Dkt Edwin Mhede, ametaka kuwepo ushirikiano na Wakuu wa Wilaya kwani maeneo hasa ya upande wa forodha bado hali siyo nzuri kama matarajio na malengo yao yalivyo, hivyo akaomba msaada wa karibu kutoka kwa viongozi hao ambao ni wenyeviti wa Kamati za ulinzi za Wilaya.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA KWA KADA ZA AFYA (Marudio) July 20, 2022
  • TANGAZO LA KAZI - TOA July 22, 2022
  • MAJINA YA WALIOPATA AJIRA KADA ZA AFYA NA UALIMU June 26, 2022
  • ORODHA YA WAKUU WA KITENGO CHA FEDHA YENYE MABADILIKO 5-5-2022 May 06, 2022
  • Kazi za muda za makarani na wasimamizi wa Sensa 2022 May 05, 2022
  • MUDA WA NYONGEZA MAOMBI YA AJIRA ZA TAMISEMI 2022 May 04, 2022
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • Utekelezaji wa Miradi ya Elimu isimamiwe na kukamilika kwa wakati- Dkt. Msonde

    August 15, 2022
  • UBUNIFU KIVUTIO UMISSETA 2022

    August 15, 2022
  • Bilioni 776.6 zaelekezwa katika ujenzi, ukarabati na matengenezo ya barabara vijijini na mijini katika mwaka wa fedha 2022/23

    August 14, 2022
  • TARURA KUONGEZA MTANDAO WA BARABARA ZA LAMI KM 1,450, CHANGARAWE KM 73,242’ ENG. SEFF

    August 14, 2022
  • Angalia zote

Video

Taarifa ya Ukusanyaji wa Mapato ya Halmashauri, kipindi cha robo ya pili ya mwaka wa fedha 2021/22
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.