Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

UCHAGUZI UMEKWISHA, SASA NI MUDA WA KUJADILIANA NAMNA KULETA MAENDELEO - Bw. Msuva

Imewekwa tar.: December 2nd, 2024

Na. Na Mwandishi wetu, Dodoma

Mkurugenzi wa Shirika la Bridge for Change Bw. Ocheki Msuva ambaye ni mtaalamu wa Siasa na Utawala anayejiushisha na masuala ya vijana katika eneo la ushiriki na ushirikishwaji amesema, uchaguzi wa Serikali za Mitaa umeisha hivyo ni muhimu kufunguka kwa majukwaa ya mazungumzo na majadiliano yenye kujenga umoja wa kitaifa kwa maslahi ya maendeleo ya taifa.

Bw. Msuva ametoa wito huo leo jijini Dodoma, ikiwa ni siku ya nne mara baada ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI Mhe. Mohamed Mchengerwa kutangaza matokeo ya jumla ya uchaguzi huo wa Serikali za Mitaa wa mwaka 2024.

Bw. Msuva ameanisha kuwa, muda huu ni wakati muafaka wa kufunguka kwa majukwaa ya mazungumzo na majadiliano yenye kujenga jamii moja ili kutoa fursa ya kuwasikiliza wale ambao wanaona kwa namna moja au nyingine hawakulizika na mchakato wa uchaguzi, fursa hiyo itakuwa ni sehemu ya kufanya maboresho kwa mustakabali wa uchaguzi ujao.

“Ushauri wangu kwa vyama vya siasa na wananchi ambao wanaona kulikuwa na dosari chache katika mchakato wa uchaguzi, ni muhimu wakawa ni sehemu ya kutoa maoni ya kiulijenga taifa ili kujiepusha na athari zitakazolikwamisha taifa kupiga hatua katika maendeleo,” Bw. Msuma amesisitiza.

Sanjali na hilo, Bw. Msuva amehimiza kuwa uchaguzi huu umekuwa wa kipekee sana kwani unatoa fursa ya kutafakari kama jamii, ni kwa namna gani tunataka kusonga mbele na kuwa sehemu ya mabadiliko katika kuchagiza maendeleo ya taifa letu,” Bw. Msuva amehimiza.

Bw. Msuva ameongeza kuwa, huu ndio wakati wa kushikamana, kujadiliana, kujenga umoja na kufikiri ni kwa namna gani bora zaidi tunaweza kuwa ni sehemu ya mchakato wa maendeleo bila kuvunja umoja wetu na amani tuliyonayo katika taifa.  

Aidha, Bw. Msuva amesema ni wazi kuwa uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa Mwaka 2024 kwa kiasi kikubwa umefanyika kwa amani na utulivu na ndio maana wananchi wengi wameshiriki tofauti na chaguzi zilizopita ambazo hazikuwa na mwitikio mkubwa wa wananchi.

“Kitendo cha wananchi wengi kujitokeza kupiga kura kinaashiria kwamba walipewa hamasa na elimu ya kutosha, hivyo walipata mwamko wa kutambua wajibu wao kikatiba na umuhimu wa kupiga kura,” Bw. Msuva amesisitiza.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan aliwaongoza watanzania 26,963,182 kupiga kura katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa uliofanyika Novemba 27, 2024.

Matangazo

  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert (extension) 1 May 28, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert (extension) May 28, 2025
  • TOR - Msimbazi Watershed Management – Modelling May 26, 2025
  • Monitoring & Support, TOR - DMDP 2 SWM Service Framework & Delivery System in Dar May 26, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • Mhe. Katimba awapokea Wabunge wa Zambia waliokuja kujifunza kuhusu Usimamizi na Uendeshaji wa Mamlaka za Serikali za Mitaa Tanzania Bara

    May 28, 2025
  • Mtwale Atoa Mwongozo kwa Makatibu Tawala Wasaidizi wa Mikoa

    May 27, 2025
  • Nipo tayari kufanya kazi pamoja nanyi kufikia malengo ya Mhe. Rais – Prof. Tumaini Nagu

    May 26, 2025
  • TARURA IMEKUWA NA MCHANGO MKUBWA KWA SERIKALI YA AWAMU YA SITA

    May 26, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.