• Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Machapisho
    • Taarifa za Mapato
    • Majarida
    • Fomu Mbali mbali
    • Presentations
  • Miongozo
    • Miongozo OR TAMISEMI
    • Miongozo ya mradi wa SEQUIP
    • Green and Smart Cities
    • Miongozo ya Kilimo
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Michoro ya Ujenzi
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)

Serikali yalegeza masharti mikopo ya asilimia 10

Imewekwa tar.: February 27th, 2021


Na Atley Kuni, DODOMA

SERIKALI imelegeza masharti ya kukopa mikopo ya asilimia 10 inayotolewa halmashauri kwa vikundi vya wanawake, vijana na walemavu ili kuviwezesha vikundi vingi zaidi kukopa.

Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dodoma na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mhe. Selemani Jafo wakati akifunga mkutano mkuu wa nne wa maafisa maendeleo jamii.

Waziri Jafo amesema kuanzia leo tarehe 26 Februari, 2021, Serikali imerekebisha na kutoa kanuni mpya ambazo zimechapishwa kwenye gazeti la Serikali ili zianze kutumika na kuwa moja ya kigezo kilicholegezwa ni kupungua kwa idadi ya wanavikundi.

“Kigezo cha kuwa na idadi ya watu kumi kwa vijana na wanawake na watu watano kwa walemavu, kwa muda mrefu kimechangia kwa baadhi ya watu waliokubaliana na malengo yanayofanana kushindwa kuungana.”

“Kanuni mpya zinasema kwa vikundi ya vijana na kina mama wakipatikana watano kikundi hicho kinaweza kukopesheka, lakini tumeenda mbali zaidi kubadilisha kanuni kumwezesha hata mtu mmoja mwenye ulemavu anaweza kupewa mkopo, haya ni mapinduzi makubwa,” amesema Waziri Jafo

Amesema kuanza kutumika kwa kanuni hizo mpya kutatoa fursa kwa vikundi vingi kuwa na sifa ya kupata mikopo hiyo.

Waziri Jafo katika eneo lingine ambalo limeimarishwa ni suala la urahisishwaji wa ufuatiliaji wa mikopo kwa Serikali kutenga fungu kulingana na ukopeshaji wa kila mamlaka.

“Kuanzia sasa kanuni mpya zinaelekeza kwa kila halmashauri kutenga kiasi cha fedha ili kuwawezesha maafisa maendeleo jamii kufanya tathmini na ufuatiliaji wa mikopo iliyotolewa.”

Akifafanua zaidi, Waziri Jafo amesema kwa halmashauri ambazo mapato yake ya ndani hayazidi shilingi bilioni moja katika kila marejesho idara ya Maendeleo ya Jamii itatengewa shilingi laki tano wakati halmashauri ambazo mapato yake ni zaidi shilingi bilioni moja zimeelekezwa kutenga kati ya Sh milioni moja na shilingi milioni moja na nusu kwa mwezi kwa ajili ya ufuatiliaji.

Aidha kwa halmashauri ambazo mapato yake yapo kati shilingi bilioni tano, na kuendelea amesema idara ya maendeleo ya jamii ipatiwe shilingi milioni tano kwa ajili ya tathmini na ufuatiliaji.

Sambamba na maboresho hayo, waziri Jafo amewataka, wataalamu wa kada hiyo, kwenda kusimamia ipasavyo marejesho ya mikopo na atakayeshindwa kufanya hivyo, basi atakuwa ameshindwa kazi.

Katika hatua nyingine Waziri Jafo, ameziagiza Mamalaka za Serikali za Mitaa, kuhakikisha wanawahusisha wataalamu wa Maendeleo ya Jamii, kwenye Miradi yote inayotekelezwa katika eneo husika kuanzia hatua za awali.

Amesema kutokana na umuhimu wa Maafisa Maendeleo Jamii kama wahamasishaji wa Jamii kwenye shughuli za Maendeleo, ameziagiza Mamlaka za Serikali za Mitaa, kuwashikisha wataalam wa kada hii katika miradi yote inayotekelezwa.

Kufuatia kauli hiyo ya Waziri Jafo, akizungumza kwa niaba ya Maafisa Maendeleo Jamii wenzake, rais mpya wa chama hicho Angela Kiama, amesema wamepokea kwa furaha mabadiliko ambayo serikali imeyafanya katika kanuni.

“Tatizo lilikuwepo mathalani kwa walemavu, unaweza kukuta mlemavu mmoja katika eneo anashindwa kupewa mkopo kwa kigezo cha kuwataka wawe kikundi, kwa kweli tunaishukuru sana serikali kwa kuliona hili na kufanya maboresho kwenye kanuni hizo,” amesema Kiama.

Maafisa Maendeleo Jamii hao waliokutana kwa siku tatu kutathmini hali ya utendaji wao wa kazi sambamba na kuwachagua viongozi wa chama chao.

Mkutano mkuu wa Maafisa Maendeleo ya Jamii, ni wa nne tangu kuanzishwa kwa chama hicho mwaka 2017, na ulikuwa na kauli mbiu, “Maafisa Maendeleo ya Jamii Nguzo Muhimu kufikia Uchumi wa Viwanda” na umewashirikisha maafisa wa kada hiyo kutoka serikalini na taasisi binafsi.

 

Matangazo

  • Orodha ya waliopata vibali vya Uhamisho Septemba - Disemba 2022 (OR - TAMISEMI) January 21, 2023
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kidato cha Kwanza Waliorudia Mtihani January 15, 2023
  • Matumizi ya Lugha ya Kiswahili na Kingereza January 14, 2023
  • Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Kwanza 2023 December 14, 2022
  • Orodha ya Waliopangwa kwenye Vituo vya Kazi Kada za Afya (Awamu ya Pili) Agosti 2022 August 30, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA KWA KADA ZA AFYA (Marudio) July 20, 2022
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • TUNZENI VIFAA VYA AFYA VILIVYONUNULIWA NA SERIKALI - DKT. MAHERA

    March 30, 2023
  • REJESHENI MIKOPO ILI WENZENU WAPATE KUKOPA –KAMATI YA LAAC

    March 31, 2023
  • LAAC YARIDHISHWA NA USIMAMIZI WA UKARABATI SHULE YA SEKONDARI WASICHANA MTWARA

    March 31, 2023
  • KAMATI YA LAAC YAKAGUA MADARASA 7 YALIYOJENGWA KWA MAPATO YA NDANI NA NGUVU ZA WANACHI - MANISPAA YA SUMBAWANGA

    March 31, 2023
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.