• Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Machapisho
    • Taarifa za Mapato
    • Majarida
    • Fomu Mbali mbali
    • Presentations
  • Miongozo
    • Miongozo OR TAMISEMI
    • Miongozo ya mradi wa SEQUIP
    • Green and Smart Cities
    • Miongozo ya Kilimo
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Michoro ya Ujenzi
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)

Serikali na Wadau Wajenga Viwanda 4,777 ndani ya Mwaka mmoja

Imewekwa tar.: March 20th, 2019

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR - TAMISEMI) Mhe. Selemani S.Jafo amesema jumla ya viwanda 4,777 vimekwisha anzishwa nchini hadi kufikia tarehe 31 Desemba, 2018 sawa na asilimia 183.73 ya lengo kujenga viwanda 2,600 katika mikoa yote.

Waziri Jafo ametoa kauli hiyo wakati akipokea taarifa ya utekelezaji wa ujenzi wa viwanda 100 kwa kila mkoa kuishia Disemba, 2018 katika kikao kilichofanyika katika ukumbi wa Hazina Jijini Dodoma.

Mafanikio hayo yanakuja baada ya uzinduzi wa Kampeni ya ujenzi wa viwanda katika Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa kote nchini ikiwa na kaulimbiu ya ‘Mkoa wetu, Viwanda vyetu’ ambayo aliitoa rasmi Novemba, 2017 katika chuo cha Mipango Dodoma.

Jafo amesema ni uamuzi wa Serikali ya awamu ya Tano wa kujenga uchumi wa viwanda unalenga kuleta maendeleo jumuishi na endelevu kwa kutumia ipasavyo rasilimali zilizopo na hivyo kuchangia katika kukuza Pato la Taifa, kutoa nafasi nyingi na endelevu za ajira, kuzalisha na kukuza teknolojia zinazohitajika na kuwa chachu ya maendeleo ya sekta zinazohusiana na kuzalisha bidhaa bora kwa ajili ya masoko ya ndani na nje ya nchi.

Viwanda vikubwa vilivyojengwa Nchini kwa muda wa mwaka mmoja ni Viwanda 108, Viwanda vya Kati ni 236, Viwanda Vidogo ni 2,422 na Viwanda Vidogo vidogo ni 2,010 ambavyo vyote kwa ujumla vimetoa ajira kwa Wananchi wapatao 36,796

Mkoa wa Dar es Salaam ndiyo Mkoa uliongoza katika ujenzi wa viwanda vikubwa, ikifanikiwa kuanzisha viwanda vikubwa 46 ikifuatiwa na Mkoa wa Pwani iliyojenga viwanda vikubwa 8. Mikoa ya Mwanza, Lindi na Simiyu yote kwa pamoja imeshika nafasi ya tatu kwa kufanikiwa kujenga viwanda vikubwa 7 kila Mkoa.

Mkoa wa Geita umeongoza katika ujenzi wa Viwanda vya Kati ukiwa umefanikiwa kuanzisha Viwanda vya Kati 57 ikifuatiwa na Mkoa wa Mbeya iliyojenga Viwanda vya Kati 40.  Mkoa wa Pwani umeshika nafasi ya tatu kwa kufanikisha kujenga Viwanda 21 vya kati.  Aidha, Mkoa wa Dar es Salaam umeongoza katika ujenzi wa Viwanda vidogo kwa kufanikiwa kuanzisha Viwanda vidogo 245 ikifuatiwa na Mkoa wa Pwani yenye kuanzisha Viwanda vidogo 219 na ya tatu ni Dodoma yenye Viwanda 196.

Mkoa wa Lindi umeongoza katika ujenzi wa Viwanda vidogo Vidogo kwa kuanzisha Viwanda vipatavyo 452 ikifuatiwa na Mkoa wa Mara yenye kuanzisha Viwanda vidogo vidogo 377 na Mkoa wa tatu ni Mkoa wa Dar es Salaam ambao umefanikiwa kujenga Viwanda  vidogo vidogo 180.

Vile vile ameagiza mikoa ambayo haikufikia lengo la viwanda 100 licha ya kufanya vizuri katika kutekeleza azma ya Serikali ya Awamu ya Tano kwa kujenga viwanda vingi.

Waziri Jafo amesema ametoa muda hadi kufikia mwezi Juni mwaka huu mikoa hiyo iwe imefikia malengo yaliyokusudiwa la sivyo ataitaja hadharani kwa kushindwa kufikia malengo ya Serikali ya Awamu ya Tano kupitia mpango wa maendeleo wa miaka mitano 2016/17 hadi 2020/21 ambapo kwa Ofisi ya Rais TAMISEMI iliweka mkakati wa viwanda 100 kila mkoa ili kusaidiana na wizara ya Viwanda na Biashara kuelekea uchumi wa kati na Tanzania ya Viwanda.

Katika hatua nyingine, Jafo amezitaja changamoto zilizokwamisha jitihada za Serikali na wadau katika kuendeleza Sekta ya Viwanda hususan Viwanda vidogo na vya kati kuwa ni pamoja na upimaji wa ardhi kwa ajili ya uwekezaji, upatikanaji wa maji ya uhakika, upatikanaji wa nishati ya umeme wa uhakika, miundombinu ya barabara na upatikanaji wa vifungashio kwa gharama nafuu.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri ambaye ni mwakililishi wa Wakuu wa Mikoa Tanzania Bara, amesema maagizo yote yaliyotolewa na Serikali wameshayachukua na watayafanyia kazi mara moja ili kufikia azma ya Serikali ya Awamu ya Tano.


                        Anaandika Fred Kibano

Matangazo

  • Orodha ya waliopata vibali vya Uhamisho Septemba - Disemba 2022 (OR - TAMISEMI) January 21, 2023
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kidato cha Kwanza Waliorudia Mtihani January 15, 2023
  • Matumizi ya Lugha ya Kiswahili na Kingereza January 14, 2023
  • Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Kwanza 2023 December 14, 2022
  • Orodha ya Waliopangwa kwenye Vituo vya Kazi Kada za Afya (Awamu ya Pili) Agosti 2022 August 30, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA KWA KADA ZA AFYA (Marudio) July 20, 2022
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • LAAC YAPOKEA TAARIFA KUHUSU UTAWALA NA UENDESHAJI WA MAMLAKA ZA SERIKALI ZA MITAA

    March 14, 2023
  • SERIKALI YAWEKA MIKAKATI KATIKA USIMAMIZI WA MIRADI YA MENDELEO, UKUSANYAJI NA UDHIBITI WA MAPATO KATIKA HALMASHAURI

    March 13, 2023
  • WAUGUZI NA WAKUNGA WATAKIWA KUSIMAMIA MAADILI YA KAZI

    March 13, 2023
  • ACHENI KUTUMIANA NYARAKA ZA SERIKALI KWENYE MITANDAO YA KIJAMII NA BARUA PEPE BINAFSI - DKT. MPANGO

    March 13, 2023
  • Angalia zote

Video

Taarifa ya Ukusanyaji wa Mapato ya Halmashauri, kipindi cha robo ya pili ya mwaka wa fedha 2021/22
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.