Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

Serikali yazindua Mwongozo wa Utoaji Elimu ya Kujitegemea, yapiga marufuku kurudisha wanafunzi nyumbani kwa kukosa michango

Imewekwa tar.: July 26th, 2024

Na Fred Kibano, Dodoma   

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda amezindua Mwongozo wa utoaji wa elimu ya kujitegemea shuleni ili kuimarisha ujifunzaji na ufundishaji shuleni.

Prof. Mkenda ametoa kauli hiyo mapema leo tarehe 26 Julai, 2024 Jijini Dodoma wakati akizindua Mwongozo wa utoaji wa Elimu ya Kujitegemea katika shule za msingi na sekondari Tanzania Bara na kuitaka jamii kuwajibika katika uchangiaji wa chakula na lishe badala ya kumrudisha nyumbani mwanafunzi au mwanafunzi kutopatiwa chakula awapo shuleni kwa kuwa hajachangia kwani itarudisha nyuma jitihada za kuimarisha ujifunzaji wa mwanafunzi shuleni.

“ni marufuku kwa mwanafunzi yoyote kwenye shule za Umma kurudishwa nyumbani kwa sababu tu mzazi hajachangia mchango wa aina yoyote ukiwemo chakula ambao umekubalika, zipo hatua nyingi zinaweza kuchukuliwa wakati mtoto anasoma” alisema Mhe. Mkenda.

Mkenda amesema katika jamii zetu, vijiji vyetu, kuna ngazi ya utawala na kanuni ambazo zina mamlaka ya kumchukulia hatua mzazi ambaye anagoma kuchangia katika suala la chakula kwa makubaliano yaliyofanyika na wanakijiji na jamii ya shule lakini mwanafunzi asinyimwe chakula kilichochangiwa na wenzake.  

Aidha, amempongea Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kusaini Mkataba wa Lishe na Wakuu wa Mikoa kuhusu utekelezaji wa afua za lishe kwani matunda yake yameanza kuonekana kupitia Wakuu wa Mikoa na Wilaya ambao ndio wahamasishaji wa suala la chakula na lishe ikiwemo shuleni kwani ipo mikoa inayofanya vizuri katika kutoa huduma ya chakula ambapo aliitaja mikoa ya Njombe kwa asilimia 98, Kilimanjaro (94), Arusha (88), Pwani (87.8), Iringa (87.2) na Manyara (82.9).

Katika hatua nyingine Prof. Mkenda amesema Ofisi ya Rais TAMISEMI kwa kushirikiana na shirika la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) waliandaa Mpango wa utekelezaji wa Mwongozo wa utoaji wa huduma ya chakula lishe shuleni ambao ulizinduliwa mwezi Novemba, 2023 na utatumiwa na Wadau wa lishe katika kuhamasisha wazazi na walezi kuendelea kuchangia chakula kwa wanafunzi pindi wawapo shuleni.

Akitoa Salamu za mkoa, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Rosemary Sitaki Senyamule amesema mkoa wake umejipanga katika kuhamasisha wazazi kuchangia chakula ili wanafunzi wapate hudma ya chakula na lishe shuleni na kwa sasa ni asilimia 76 ya mashamba na bustani yanalimwa ili kuimarisha utoaji wa chakula katika shule za msingi mkoani humo hii ni sambamba na uzinduzi wa Mpango Mkakati wa ufaulu wa mkoa.

Naye Mwalimu Mkuu shule ya msingi Iyenge Thomas Malembe ameipongeza Global Communities kwa kuwajengea uwezo Kamati ya Shule na Wazazi kwani wazazi waliweza kuchangia kiasi cha shilingi milioni tano ambazo zimesaidia wanafunzi kupata chakula, kuwa na akiba ya gunia 50 za nafaka lakini pia wameweza kuvuna gunia 30 za nafaka na mazao jamii ya kunde zaidi ya kilogramu 500 mwaka 2024 ambazo zimeimarisha suala la chakula na lishe shuleni kuondoa utoro na kuongeza ufaulu.


Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert May 12, 2025
  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert May 12, 2025
  • Fursa kwa Wahitimu wa Kidato cha Nne 2024 kubadili Tahasusi na Kozi April 02, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI AJIRA ZA AFYA - TAMISEMI 2025 March 15, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI

    May 23, 2025
  • PJT-MMMAM Yawezesha Uanzishwaji wa Vituo 206 vya Malezi ya Watoto Wadogo

    May 21, 2025
  • SERIKALI KUJENGA DARAJA LINALOUNGANISHA KIJIJI CHA NEGERO – KILINDI

    May 21, 2025
  • MHE. MCHENGERWA ABORESHA TAARIFA ZAKE KWENYE  DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA

    May 20, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.