Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

Sekretarieti za Mikoa jiridhisheni maeneo zinapojengwa Hospitali za Wilaya -Dkt. Gwajima

Imewekwa tar.: July 15th, 2020

Na. Atley Kuni-MOROGORO

Naibu Katibu Mkuu anayeshughulikia masuala ya Afya Ofisi ya Rais TAMISEMI, Dkt. Dorothy Gwajima, amezisisitiza Sekretarieti za Mikoa yote nchini kujiridhisha na maeneo yaliyotengwa na Halmashauri kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali kabla ya kuanza ujenzi huo. Dkt Gwajima ameyasema hayo akiwa Halmashauri ya Mlimba mkoani Mrogoro katka ziara ya kikazi ya kufuatilia mpango wa Serikali wa ujenzi wa Hospitali 28 za Halmashauri zilizopewa Tsh milioni 500 kila mmoja kwenye mwqaka wa fedha 2019/20.

Katika Halmashauri hiyo Naibu Katibu Mkuu huyo, alitembelea eneo lililotengwa kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali hiyo na kubaini uwepo wa miinuko mikali na hivyo kuielekeza Halmashauri hiyo kufanya utaratibu wa kubadilisha eneo hilo na kuchagua lenye nafuu ili kuepuka gharama kubwa za kudhibti miinuko na mabonde hayo yanayoweza pia kuathiri mchakato wa uendeshaji wa huduma.

“Mkumbuke kuwa eneo hili litatumiwa na wagonjwa wa aina mbalimbali hivyo lazima liwe rafiki na siyo liwe chanzo cha kero na changamoto kwa wagonjwa, watoa huduma na kwa bajeti ya Serikali, hivyo tafuteni eneo mbadala. Na nyie wataalamu wa afya mliopo Halmashauri simameni katika nafasi zenu” amesema Dkt Gwajima.

Dkt. Gwajima ametumia fursa hiyo kuzitahadharisha Sekretarieti za Mikoa na Halmashauri zingine nchini kuwa zishirikiane katika kuhakiki maeneo husika na kuwepo na muhtasari wa makubaliano kuwa eneo hilo limehakikiwa na kukubalika kuwa ni sahihi na ngazi zote yaani Halmashauri na Mkoa.  

Naye Mganga Mkuu wa Mkoa Dkt Kusirye Ukio amesema hakubaliani na kwamba huo ndio mwanzo wakuzalisha gharama, amesema, mtakuja kujenga hapa Hospitali moja na nusu wakati wenzenu kwa kiasi hicho hicho wameweza kukamilisha majengo yaliyokusudiwa huku akitoa ahadi mbele ya Naibu Katibu Mkuu, na kumuhakikishia kufuatilia kwa karibu na kutoka na majawabu sahihi juu ya nini kifanyike na ujenzi wa Hospitali uendelee  na kutoa ahadi ya kutoa taarifa Ofisi ya Rais TAMISEMI ndani ya juma moja toka tarehe ya ziara hiyo.

Akionesha kukiri mapungufu hayo Mganga Mkuu wa Halmashauri hiyo Dkt. Christina Guvert alisema, yeye pamoja na timu ya wataalamu amepokea na ameahidi kufanya utekelezaji ndani ya siku 14 na kisha kuwasilisha taarifa kwa Mganga Mkuu wa Mkoa kwa ajili ya kuiwasilisha Ofisi ya Rais TAMISEMI.

Serikali kupitia Ofisi ya Rais TAMISEMI, imekwishatoa kiasi cha milioni 500 kwa ajili ya kuanza ujenzi wa Hospitali Mpya za Halmashauri za Wilaya 28 kwa mwaka wa fedha 2019/20 ikiwa ni awamu ya pili ya mkakati wa ujewa Hospitali hizi ulioanza na awamu ya kwanza ya ujenzi wa Hospitali 67 mwaka wa fedha 2018/19 ambapo tayari majngo ya Hospitali 53 yameanza kutumika.

Hivi sasa wataalamu kutoka Ofisi ya Rais-TAMISEMI kwa kushirikiana na Sekretarieti za Mikoa yote na wadau wanaendelea na zoezi la ufatiliaji wa karibu ili kuhakikisha utekelezaji wa mpango huo unafanyika kwa tija na kudhibiti changamoto zisizo za lazima.

Matangazo

  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert (extension) 1 May 28, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert (extension) May 28, 2025
  • TOR - Msimbazi Watershed Management – Modelling May 26, 2025
  • Monitoring & Support, TOR - DMDP 2 SWM Service Framework & Delivery System in Dar May 26, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • Mhe. Katimba awapokea Wabunge wa Zambia waliokuja kujifunza kuhusu Usimamizi na Uendeshaji wa Mamlaka za Serikali za Mitaa Tanzania Bara

    May 28, 2025
  • Mtwale Atoa Mwongozo kwa Makatibu Tawala Wasaidizi wa Mikoa

    May 27, 2025
  • Nipo tayari kufanya kazi pamoja nanyi kufikia malengo ya Mhe. Rais – Prof. Tumaini Nagu

    May 26, 2025
  • TARURA IMEKUWA NA MCHANGO MKUBWA KWA SERIKALI YA AWAMU YA SITA

    May 26, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.