Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

Mchezo wa Riadha watia fora Mashindano ya FEASSSA jijini Arusha

Imewekwa tar.: August 23rd, 2019

Na Mathew Kwembe, Arusha

Mashindano ya michezo ya shule za Sekondari kwa nchi za Afrika Mashariki (FEASSSA) imeingia katika siku ya nane leo ambapo mbali na michezo mingine inayoendelea kulifanyika pia mchezo wa riadha ambapo wanariadha kutoka nchi za Kenya, Uganda na Tanzania walitia fora baada ya kujizolea pointi na medali nyingi katika michuano hiyo.

Hadi michezo hiyo inakamilika leo mchana, timu ya wanariadha kutoka nchini Kenya ndiyo inayoongoza kwenye mashindano hayo kwa upande wa riadha kwa kujishindia jumla ya pointi 345 kufuatia wanariadha wake kupata medali 18 za dhahabu, 9 za fedha na 10 za shaba na jumla kujizoelea medali 37.

Nafasi ya pili katika mchezo wa riadha ilichukuliwa na wanariadha kutoka Uganda ambao walijizolea pointi 316 baada ya kushinda medali 8 za dhahabu, 14 za fedha na 10 za shaba huku wenyeji Tanzania wakiambulia nafasi ya tatu baada ya kupata jumla ya pointi 197 kwa kupata medali 2 za dhahabu, 5 za fedha na 6 za shaba.

Mchanganuo wa matokeo hayo unaonyesha kuwa  ushindi wa Kenya umechangiwa na wanariadha wake wasichana kwa wavulana kufanya vizuri katika mashindano hayo ambapo timu yake ya wasichana ilijizolea medali 7 za dhahabu, 4 za fedha, na 6 za shaba na hivyo kujinyakulia pointi 162, huku wanariadha wavulana kutoka nchi hiyo walifanikiwa kupata medali 11 za dhahabu, 5 za fedha na 4 za shaba,

Kwa upande wa Uganda ushindi wao ulitokana na mafanikio ya wanariadha wao wasichana ambao walipata medali 5 za dhahabu, 8 za fedha na 4 za shaba na kujizolea jumla ya pointi 165, huku wavulana walipata medali 3 za dhahabu, 6 za fedha na 3 za shaba

Tanzania kwa upande wao timu yao ilishika nafasi ya tatu kufuatia timu yao ya wasichana kujishindia medali 2 za dhahabu, 2 za fedha na 4 za shaba na jumla kupata pointi 104 huku wavulana kutoka Tanzania walipata medali 3 za fedha na 2 za shaba.

Waliofanikiwa kuiletea medali ya dhahabu Tanzania ni mwanariadha Carreen Philipo kutoka shule ya sekondari ya wasichana Kondoa iliyopo mkoani Dodoma, mwanafunzi wa kidato cha tano ambaye alifanikiwa kushinda medali hiyo baada ya kufanikiwa kurusha tufe umbali wa mita 12.71 na kuwashinda Penina Akoth wa Kenya na Alanyo Catherine wa Uganda ambao walishika nafasi ya pili na tatu.

Medali nyingine ya dhahabu ilitokana na ushindi wa timu ya wasichana ya Tanzania katika mchezo wa kupokezana vijiti mita 100 x 4 ambapo wasichana wanne kutoka Tanzania walifanikiwa kushika nafasi ya kwanza mbele ya wanariadha wa Kenya na Uganda.

Akizungumzia michuano hiyo Kocha wa riadha wa Tanzania Taratibu Machaku amesema kuwa mashindano ya mwaka huu yalikuwa magumu kuliko walivyodhani lakini amewasifu vijana wake kwa ushujaa waliouonyesha kwenye mashindano hayo licha ya ukweli kuwa wanariadha wengi wa Tanzania hawatoki kwenye shule za michezo kulinganisha na wanariadha kutoka Kenya na Uganda.

Hivyo Machaku amewataka wadau wa michezo nchini kujenga shule nyingi za kulea vipaji vya michezo nchini ili Tanzania iweze kuwa na timu imara ya kuweza kushindana na nchi za Kenya na Uganda.

Naye Mwanariadha  Mathayo Sombi wa Tanzania, Mwanafunzi wa kidato cha tano kutoka shule ya vipaji ya Alliance ya jijini Mwanza ambaye alifanikiwa kupata medali 2 za fedha baada ya kushika nafasi ya pili katika mbio ndefu za mita 10,000 na mita 5,000 alisema kuwa hali ya hewa ya Arusha ilichangia kumuathiri kushinda nafasi ya kwanza na amesema anajipanga mwakani ili aweze kushinda mashindano hayo.

Kwa upande wake Felix Ogwang ambaye ni mwandishi wa michezo kutoka Uganda amesema kwa upande wake ameona vipaji vingi vya michezo kutoka nchi za Kenya, Uganda na Tanzania lakini kwa maoni yake ameona kuwa kinachowakosesha ushindi wanariadha wa Tanzania ni kuchukulia michezo kama kitu cha ziada cha kufanya baada ya masomo.

Amesema kuwa hali hiyo ni tofauti na Uganda kwani wanafunzi wanaoshiriki michuano mikubwa ya FEASSSA ambao hupewa cheti maalum na wizara ya elimu ya Uganda hupata alama 5 ambazo hujumlishwa kwenye matokeo ya kujiunga na elimu ya juu nchini humo jambo ambalo Ogwang ameliita kama motisha inayowavuta vijana wengi nchini humo kujituma zaidi katika michezo.

Mashindano ya 39 ya FEASSSA yanatarajiwa kukamilika tarehe 25 agosti 2019 katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha ambapo jumla ya mataifa sita ya Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi, Malawi na wenyeji Tanzania yalishiriki mashindano hayo.

 

 

Matangazo

  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert (extension) 1 May 28, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert (extension) May 28, 2025
  • TOR - Msimbazi Watershed Management – Modelling May 26, 2025
  • Monitoring & Support, TOR - DMDP 2 SWM Service Framework & Delivery System in Dar May 26, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • Mhe. Katimba awapokea Wabunge wa Zambia waliokuja kujifunza kuhusu Usimamizi na Uendeshaji wa Mamlaka za Serikali za Mitaa Tanzania Bara

    May 28, 2025
  • Mtwale Atoa Mwongozo kwa Makatibu Tawala Wasaidizi wa Mikoa

    May 27, 2025
  • Nipo tayari kufanya kazi pamoja nanyi kufikia malengo ya Mhe. Rais – Prof. Tumaini Nagu

    May 26, 2025
  • TARURA IMEKUWA NA MCHANGO MKUBWA KWA SERIKALI YA AWAMU YA SITA

    May 26, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.