Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

MTAKA awapa somo Wanganga Wakuu wa Mikoa na Wilaya.

Imewekwa tar.: August 17th, 2018


Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe Antony Mtaka amewataka Waganga Wakuu wa Mikoa na Wilaya kuahikikisha wanatumia taaluma yao katika kuleta maendeleo kwa jamii ili kuwasaidia wananchi maskini.

Ameyasema hayo wakati akifunga Mkutano Mkuu wa Wanganga Wakuu wa Mikoa na Wilaya leo uliofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa LAPF Jijini Dodoma.

Mhe Mtaka amewataka Waganga hao kuhakikisha wanafanyakazi kwa kuzingatia sheria, taratibu na weledi weledi wa hali ya juu kwa kutetea kada ya madaktari nchini ili kuongeza ufanisi na kuleta maendeleo nchini.

“Inasikitisha kuona Mganga Mkuu wa Mkoa na Wilaya yupo halafu unakuta kituo cha afya kimejengwa hovyo, mpaka viongozi waje ndio wanagundua kasoro, ukiona hivyo inaonyesha hautoshi katika uongozi.” Anasema Mtaka.

Amesema kuwa Serikali imewekeza fedha nyingi katika sekta ya Afya hivyo ni wajibu wao kuhakikisha wanafikia malengo ya kuleta mabadiliko katika sekta ya afya ili kumsaidia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli katika suala zima kusaidia jamii maskini nchini.  

Mhe. Mtaka amesema Serikali imewekeza fedha nyingi katika Sekta ya afya hivyo ni wajibu wa kila kiongozi kusimamia kwa weledi ili kuleta mabadiliko na kupunguza kero za afya nchini.

Akisistiza katika kuwekeza kwa wataalam wa afya Mhe Mtaka amewataka Waganga hao kuhakikisha wanaridhisha taalum hiyo kwa wataalam wapya wa afya ili iweze kuwa endelevu na kuwataka kusimamia maadili katika utendaji kazi.

“Tuwekeze  kwa wataalam wa afya kwa kuwasomesha na kuwaridhisha taaluma hiyo ili vizazi vijavyo viweze kufanya kazi kwa uadilifu na uaminifu katika utoaji wa huduma za afya nchini ‘’Anasema Mtaka.

Amesema kuwa kama hakuna maadili katika sekta ya afya taaluma hiyo haitakuwa na manufaa kwa jamii, hivyo amewataka kuhakikisha wanasimamia maadili kwa watumishi wa sekta ya afya nchini.

Aidha ameawataka kuhakikisha kuwa wanakuwa chachu ya maendeleo katika jamii kwa kutumia taaluma yao katika kutoa ushauri ili mabadiliko hayo yafanyike kuanzia ngazi ya vijiji, kata na taifa kwa ujumla.

Wakati huohuo Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa anayeshughulikia afya Dkt. Zainabu Chaula amewataka watumishi wa sekta ya afya kushirikiana katika kazi ili kuleta maendeleo na kutoa huduma bora za afya.

“Wataalam wote wanawajibu wa kuwajibika ipasavyo katika utoaji wa huduma kwa jamii ili kuweza kutekeleza ilani ya Chama cha Mapinduzi ya kuhakikisha sekta ya afya inatoa huduma stahiki kwa jamii.

Aidha amesema kuwa hakutakuwa na mafanikio kama hakutakuwa na umoja na mshikamano katika utendaji kazi, hivyo amewataka kuhakikisha kuwa wanafanyakazi katika umoja na kuleta maendeleo.



Matangazo

  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert (extension) 1 May 28, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert (extension) May 28, 2025
  • TOR - Msimbazi Watershed Management – Modelling May 26, 2025
  • Monitoring & Support, TOR - DMDP 2 SWM Service Framework & Delivery System in Dar May 26, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • Mhe. Katimba awapokea Wabunge wa Zambia waliokuja kujifunza kuhusu Usimamizi na Uendeshaji wa Mamlaka za Serikali za Mitaa Tanzania Bara

    May 28, 2025
  • Mtwale Atoa Mwongozo kwa Makatibu Tawala Wasaidizi wa Mikoa

    May 27, 2025
  • Nipo tayari kufanya kazi pamoja nanyi kufikia malengo ya Mhe. Rais – Prof. Tumaini Nagu

    May 26, 2025
  • TARURA IMEKUWA NA MCHANGO MKUBWA KWA SERIKALI YA AWAMU YA SITA

    May 26, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.