Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

JAFO: Ugatuaji wa Madaraka ni muhimu katika Mamlaka za Serikali za Mitaa

Imewekwa tar.: September 10th, 2019

Waziri Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo amesema ili Mamlaka za Serikali za Mitaa ziweze kujiendesha lazima kuwepo na demokrasia  ambapo ugatuaji wa madaraka ni muhimu  katika  Mamlaka za Serikali za Mitaa

Ameyasema hayo leo wakati akifungua Kikao kazi  kati ya Menejimenti ya  Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa  na Watumishi kutoka Ofisi ya Rais Tawala na Serikali za Mitaa na Idara maalum ya Zanznibar  kilichofanyika katika  Ofisi za OR-TAMISEMI Jijini Dodoma.

Mhe. Jafo amesema katika kuhakikisha wananchi wanapata viongozi bora katika jamii Ofisi ya Rais TAMISEMI husimamia viongozi wa vijiji wasiopungua 12,000, viongozi wa Mitaa ambao wao wanapatikana katika Majiji, Manispaa na Halmashauri za Mijiambao ni zaidi ya 4000 na viongozi wa vitongoji zaidi ya elfu 64.

Amefafanua kuwa OR-TAMIEMI ni kiungo muhimu katika kusimamia utekelezaji wa sera mbalimbali zinazoandaliwa na Wizara zote nchini hivyo inaposhindwa kutimiza majukumu yake, kunakuwepo na ongezeko kubwa la Malalamiko kwa wananchi.

“Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa ni kiungo muhimu katika Sekta zote ambapo isipotimiza wajibu wake kwa weledi haitatimiza lengo la Serikali la kuhakikisha uwepo wa maendeleo katika kila sekta nchini” Amefafanua Jafo.

Amesema kuwa OR-TAMISEMI ni watekelezaji wa Sera na miongozo mbalimbali inayotolewa na Wizara za Kisekta kwa kuwa ndio yenye Halmashauri ambazo hutoa huduma kuanzia ngazi ya kitongoji, kijiji na mtaa lengo likiwa ni kutatua kero mbalimbali za wananchi.

Amezitaja Taasisi ambazo zipo chini ya OR-TAMISEMI kuwa ni elimu Kibaha ambayo inasimamia masuala ya elimu, Taasisi ya Mabasi ya Mwendokasi, Chuo cha Hombolo ambacho kinaendesha mafunzo kwa ajili ya kutengeneza watumishi watakaosimamia utendaji kazi katika Mamlaka za Serikali za Mitaa

Mhe. Jafo amesema ugatuaji wa madaraka hufanyika pia katika  Sekta ya Elimu ambapo  kazi ya Wizara ya Elimu ni kutunga Sera na miongozo mbalimbali wakati OR-TAMISEMI kazi yake ni  kusimamia miundombinu ya Elimu  kuanzia ngazi ya Msingi hadi Sekondari lengo likiwa ni kuboresha utoaji wa elimu nchini.

Hata hivyo amesema kwa upande wa Sekta ya Afya Serikali imeweza kufanya mabadiliko makubwa ambapo mpaka sasa Hospitali za Wilaya 67 zinajengwa na Vituo vya kutolea huduma 352 vimekarabatiwa na kujengwa katika Mamlaka za Serikali za Mitaa nchini.

Amewataka watumishi kutoka Ofisi ya Rais Tawala za Serikali za Mitaa na Idara maalum kutoka Zanzibar kujifunza kazi zinazofanywa na Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tanzania Bara ili waweze kufanyia kazi yale ambayo watayapata katika kikao kazi hicho.

Wakati huohuo Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhandisi Joseph Nyamhanga amewapongeza watumishi hao kwa kuamua kujifunza kuhusu ugatuaji wa madaraka katika Mamlaka za Serikali za Mitaa lengo likiwa ni kubadilishana uzoefu katika majukumu ili kuleta mabadiliko katika jamii.

Naye Naibu Waziri, Ofisi ya Rais Tawala na Serikali za Mitaa  na Idara Maalum  Zanzibar Mhe. Shamata Khamisi amesema kuwa lengo la ujio wao ni kubadilishana uzoefu kwa kuwa Zanzibar imeanza kupeleka majukumu kwa wananchi ikiwa ni ugatuaji wa madaraka.

Amesema kuwa kwa upande wa Zanzibar utekelezaji wa Sera ya ugatuaji wa madaraka inatakribani miaka miwili ambapo yapo mafanikio ambayo yanaonekana hivyo ni wajibu wetu kuja kujifunza zaidi  juu ya ugatuaji wa madaraka ili kuweza kuendelea  kutoa huduma bora kwa jamii.

 Na. Angela Msimbira OR-TAMISEMI

Matangazo

  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert (extension) 1 May 28, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert (extension) May 28, 2025
  • TOR - Msimbazi Watershed Management – Modelling May 26, 2025
  • Monitoring & Support, TOR - DMDP 2 SWM Service Framework & Delivery System in Dar May 26, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • Mhe. Katimba awapokea Wabunge wa Zambia waliokuja kujifunza kuhusu Usimamizi na Uendeshaji wa Mamlaka za Serikali za Mitaa Tanzania Bara

    May 28, 2025
  • Mtwale Atoa Mwongozo kwa Makatibu Tawala Wasaidizi wa Mikoa

    May 27, 2025
  • Nipo tayari kufanya kazi pamoja nanyi kufikia malengo ya Mhe. Rais – Prof. Tumaini Nagu

    May 26, 2025
  • TARURA IMEKUWA NA MCHANGO MKUBWA KWA SERIKALI YA AWAMU YA SITA

    May 26, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.