Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

Jafo awaruhusu wagombea wote nchini waliochukua fomu na kuzirejesha kushiriki uchaguzi wa Serikali za Mitaa.

Imewekwa tar.: November 10th, 2019

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo wagombea wote waliochukua na kurejesha fomu za kuwania nafasi mbalimbali za uongozi katika uchaguzi wa serikali za mitaa bila kujali kama walienguliwa isipokuwa kwa wale wasio raia wa Tanzania, hawakujiandikisha au wamejiandikisha mara mbili.

Ameyasema hayo leo wakati  akiongea na waandishi wa Habari   ofisini kwake Jijini Dodoma kuhusiana na mapingamizi na rufaa mbalimbali zilizotolewa wakati wa urejeshaji wa fomu  katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa.

Mhe. Jafo amesema kuwa hatua hiyo imetokana na kanuni za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa ambapo Waziri mwenye dhamana ya uchaguzi ana nafasi ya kutoa mwongozo wa jambo lolote kuhusu uchaguzi huo.

 “ Kwa mujibu wa kanuni za uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka 2019 Tangazo la Serikali Na. 371, Kanuni ya 49, Tangazao Na. 372 la mwaka 2019 Kanuni ya 51, Tangaza la Serikali Na. 373 la mwaka 2019 la mwaka 2019 Kanuni ya 52 na Tangazo la Serikali Na. 374 la mwaka 2019 kanuni ya 52 ninaotoa mwongozo kwamba wagombea wote ambao waliteuliwa na kudhaminiwa na vyama vyao na kufanikiwa kurejesha fomu zao za uteuzi kwa wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi katika kipindi kilichokuwa kimepangwa cha kuchukua na kurejesha fomu wanapewa sifa ya kupigiwa kura na wananchi.”

Amezitaja sababu ambazo hazitamruhusu mtu kugombea nafasi ya uongozi kuwa ni wale ambao watabainika kuwa wamejidhamini wenyewe, kutodhaminiwa na chama chake cha siasa, wagombea wawili wa chama kimoja kurejesha fomu katika nafasi moja na kama atakuwa amejitoa kwa mujibu wa Kanuni za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa

“Nadhani ni habari njema kwa wale waliokuwa na madukuduku, mapingamizi sasa mambo yote yale tumeyaondoa ili mradi wamerejesha fomu zao lakini hawana pingamizi za uraia na mambo mengine niliyoyaeleza basi naelekeza wasimamizi na wasimamizi wasaidizi wawajumuishe kwa kuwa wamepewa sifa” amesema Mhe, Jafo.

Mhe. Jafo amesema hakuna kuweka mpira kwapani, hakuna kukimbia hapa mpaka kieleweke, kama mtu alirejesha fomu na hana makandokando niliyoyabainisha wote wamepewa sifa na watajumuisha kwenye wangombea wa uchaguzi.

Kuhusu Vyama vilivyojitoa Mhe. Jafo amesema kwa mujibu wa kanuni za uchaguzi zinatambua kujitoa kwa mgombea na si Chama kujitoa hivyo mpaka sasa wagombea ambao walijaza fomu na kuzirejesha zikiwa zimedhaminiwa na vyama vya siasa wagombea hao wanatambulika kushiriki uchaguzi huo.

“Kama kuna chama kinataka kutoshiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa havikatazwi kuendelea kugoma kwani huwenda hiyo ndiyo aina ya demokrasia yao.”amefafanua Mhe. Jafo

Ameendelea kusema kuwa utaratibu wa uchukuaji na urejeshaji fomu, jumla ya wananchi 555,036 kutoka vyama vyenye usajili wa kudumu walifanikiwa kuchukua fomu za kugombea na kati ya hao wananchi 539,993 sawa na wasilimia 97.3 walifanikiwa kurejesha fomu zao.

Mhe. Jafo amesema wananchi walichukua fomu kutoka Chama cha Mapinduzi walikuwa ni 412,872 ikiwa ni asilimia 74 ya watu wote waliochukua fomu wakati Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) walikuwa ni 105,937 ambayo ni sawa na asilimia 19.

Amesema Chama cha Wananchi (CUF) walikuwa ni 24,592 ambao ni sawa na asilimia 4, ACT- Wazalendo  walikuwa ni 8,526 ambao ni sawa na aslimia 1.5, NCCR-Mageuzi walikuwa ni 2,244 ambao ni asilimi 0.4 huku vyama vingine vyenye usajili wa kudumu walikuwa chini ya asilimi 0.1 kwa kila chama.

Hata hivyo Mhe. Jafo amesema mapingamizi na rufaa mbalimbali zipatazo 15,380 ziliwasilishwa katika kamati za rufaa kote nchini na kuwa baada ya uamuzi kutolewa rufaa 4,921 ambazo ni sawa na asilimi 32 ya rufaa zote zilitishwa.

“Baada ya maamuzi ya kamati, asilimia 32 ya rufaa hizo zilipitishwa lakini asilimi 68 ya rufaa zilikosa sifa kwa sababu mbalimbali kulingana na kanuni za uchaguzi.”amesema Mhe. Jafo

Mhe Jafo amefafanua kuwa katika machakto wa kuchukua na kurudisha fomu CCM iliweza kupita bila kupingwa katika maeneo mbalimbali kwa kuwa hapakuwa na mgombea yeyote kutoka vyama vingine vya siasa.

“Hii inamaana katika nafasi zilizoombwa katika baadhi ya maeneo, aliyechukua fomu na kurudisha fomu ni mgombea kutoka Chama cha Mapinduzi pekee na hakukuwa na mgombea yeyote kutoka vyama vingine vya siasa,” amesema Mhe. Jafo.

Akifafanua zaidi, Mhe Jafo amesema kwa upande wa nafasi ya wenyeviti wa vijiji CCM imepitwa bila kupingwa katika vijiji 6,248 kati ya vijiji 12,319 vilivyopo nchini ambayo ni sawa na asilimia 51.

Ameendelea kusema kuwa kwa upande wa wenyeviti wa mitaa, CCM imepita bila kupingwa katika mitaa 1,169 kati ya mitaa 4,263 iliyopo nchini ambayo ni sawa na asilimi 27 na kwa upande wa vitongoji CCM imepita bila kupingwa kwenye vitongoji 37,505 kati ya vitongozji 64,384 sawa na asilimia 58.

Mhe Jafo amesema kwa upande wa wajumbe wa kundi la wanawake jumla ya wajumbe 64,085 wamepita bila kupingwa na wajumbe kundi la mchanganyiko jumla ya wajumbe 75,560 wamepita bila kupingwa.

 Aidha, Mhe.Jafo amevitaka vyama vya siasa vinavyoshiriki uchaguzi huo kuhakikisha wanawasilisha ratiba za kampeni kwa wasimamizi wa uchaguzi.



Matangazo

  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert (extension) 1 May 28, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert (extension) May 28, 2025
  • TOR - Msimbazi Watershed Management – Modelling May 26, 2025
  • Monitoring & Support, TOR - DMDP 2 SWM Service Framework & Delivery System in Dar May 26, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • Mhe. Katimba awapokea Wabunge wa Zambia waliokuja kujifunza kuhusu Usimamizi na Uendeshaji wa Mamlaka za Serikali za Mitaa Tanzania Bara

    May 28, 2025
  • Mtwale Atoa Mwongozo kwa Makatibu Tawala Wasaidizi wa Mikoa

    May 27, 2025
  • Nipo tayari kufanya kazi pamoja nanyi kufikia malengo ya Mhe. Rais – Prof. Tumaini Nagu

    May 26, 2025
  • TARURA IMEKUWA NA MCHANGO MKUBWA KWA SERIKALI YA AWAMU YA SITA

    May 26, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.