• Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Machapisho
    • Taarifa za Mapato
    • Majarida
    • Fomu Mbali mbali
    • Presentations
  • Miongozo
    • Miongozo OR TAMISEMI
    • Miongozo ya mradi wa SEQUIP
    • Green and Smart Cities
    • Miongozo ya Kilimo
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Michoro ya Ujenzi
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)

Halmashauri zaagizwa kutumia mapato yao kwenye huduma za jamii

Imewekwa tar.: June 5th, 2019

Na Mathew Kwembe, Dodoma

Serikali imewaagiza wakurugenzi wa halmashauri nchini kuhakikisha kuwa wanaelekeza fedha wanazozikusanya kutoka katika vyanzo vyao mbalimbali katika kuboresha miradi na miundombinu ya jamii ili kuchochea kasi ya maendeleo katika halmashauri zao.

Agizo hilo limetolewa leo jijini Dodoma na Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa anayeshughulikia elimu Mhe. Mwita Waitara wakati akiwa katika shule ya sekondari ya Wella iliyopo eneo la Mkonze katika jiji la Dodoma.

Amesema Wakurugenzi wa Halmashauri hawana budi kutumia vizuri mapatao inayoyakusanya kuboresha miradi ya maendeleo kwani serikali ya awamu ya tano imedhamiria kutatua changamoto na kero mbalimbali kwa jamii.

“Napenda kuwaagiza wakurugenzi wa halmashauri wahakikishe kuwa wanayaelekeza fedha wanazokusanya katika kutatua changamoto mbalimbali zinazozikabili halmashauri zao badala ya kusubiri kero hizo zishughulikiwe na serikali kuu,” amesema.

Naibu Waziri ameongeza kuwa changamoto kama za ukosefu wa matundu ya kutosha ya vyoo, uchakavu wa miundo mbinu ya shule, na kero nyingine za aina hiyo zinaweza kutatuliwa kwa kupitia makusanyo ya halmashauri husika.

Mbali na kutembelea sekondari ya Wella, ambayo imekuwa ikikabiliwa na changamoto kadhaa zikiwemo za majengo yake yote kutokamilika na upungufu wa matundu ya vyoo, Naibu Waziri pia alitembelea eneo la Dodoma Makulu ambapo alijionea namna kikundi cha vijana cha Jikomboe kinavyojishughulisha na ufyatuaji wa matofali, kikiwa ni miongoni mwa vikundi mbalimbali vilivyopata fedha za mkopo kutoka halmashauri ya jiji la Dodoma.

Pia Mhe Waitara ametembelea eneo la Ipagala na kuona ujenzi wa shule ya mfano unavyoendelea , mradi wa kimkakati wa ujenzi wa soko na stendi  wenye thamani ya shilingi bilioni 34, sekondari ya miyuji kukagua umaliziaji wa vyumba sita vya madarasa, na sekondari ya msalato kukagua ukarabati wa miundombinu ya shule hiyo.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa jiji la Dodoma bwana Godwin Kunambi alimweleza Naibu Waziri juu ya mikakati ya jiji hilo katika kutatua changamoto mbalimbali zinazozikabili shuke za msingi na sekondari ambapo amesema kuwa katika bajeti ijayo jiji limetenga kiasi cha shilingi bilioni 8 kutatua changamoto hizo.

Amesema kuanzia sasa jiji la Dodoma litahakikisha kuwa ujenzi wa shule zake utakuwa wa kisasa unaoendana na taswira ya jiji la Dodoma ambapo chini kutawekwa marumaru badala ya sakafu kama ilivyo hivi sasa na juu bati zake zitawekwa rangi kulingana na mpangilio wa ujenzi wa jiji hilo.

Akizungumzia kuhusu changamoto zinazoikabili shule ya sekondari ya wella ambayo majengo yake mengi hayajakamilika licha ya kuanza kutumiwa na walimu na wanafunzi wa shule hiyo, Mkurugenzi huyo amesema kuwa kwa mwaka huu jiji lilipeleka shilingi milioni 50 kwa ajili ya ukarabati wa baadhi ya miundombinu ya shule na kwamba wanatarajia kuwa katika mwaka ujao wa fedha majengo yote ya shule hiyo yatakarabatiwa kwa kuwekewa marumaru na mabati kupakwa rangi pamoja na ujenzi wa matundu ya vyoo vya walimu na wanafunzi.

Katika ziara yake hiyo ambayo ni ya kwanza kutembelea jiji la Dodoma kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo, Mhe. Waitara aliambatana na Mkuu wa Wilaya ya Dodoma mjini Mhe.Patrobas Katambi, Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma bwana Godwin Kunambi na viongozi mbalimbali kutoka mkoa wa Dodoma na jiji la Dodoma

Matangazo

  • Orodha ya waliopata vibali vya Uhamisho Septemba - Disemba 2022 (OR - TAMISEMI) January 21, 2023
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kidato cha Kwanza Waliorudia Mtihani January 15, 2023
  • Matumizi ya Lugha ya Kiswahili na Kingereza January 14, 2023
  • Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Kwanza 2023 December 14, 2022
  • Orodha ya Waliopangwa kwenye Vituo vya Kazi Kada za Afya (Awamu ya Pili) Agosti 2022 August 30, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA KWA KADA ZA AFYA (Marudio) July 20, 2022
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • LAAC YAPOKEA TAARIFA KUHUSU UTAWALA NA UENDESHAJI WA MAMLAKA ZA SERIKALI ZA MITAA

    March 14, 2023
  • SERIKALI YAWEKA MIKAKATI KATIKA USIMAMIZI WA MIRADI YA MENDELEO, UKUSANYAJI NA UDHIBITI WA MAPATO KATIKA HALMASHAURI

    March 13, 2023
  • WAUGUZI NA WAKUNGA WATAKIWA KUSIMAMIA MAADILI YA KAZI

    March 13, 2023
  • ACHENI KUTUMIANA NYARAKA ZA SERIKALI KWENYE MITANDAO YA KIJAMII NA BARUA PEPE BINAFSI - DKT. MPANGO

    March 13, 2023
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.