• Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Machapisho
    • Taarifa za Mapato
    • Majarida
    • Fomu Mbali mbali
    • Presentations
  • Miongozo
    • Miongozo OR TAMISEMI
    • Miongozo ya mradi wa SEQUIP
    • Green and Smart Cities
    • Miongozo ya Kilimo
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Michoro ya Ujenzi
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)

Gwajima Asisitiza Uzalendo, Mapitio Ya Sera Ya Ugatuaji Wa Madaraka

Imewekwa tar.: December 10th, 2019

Naibu Katibu Mkuu anayeshughulikia Afya, OR-TAMISEMI Dkt. Dorothy Gwajima amewataka wakurugenzi wa Sera na Mipango wa Wizara zote kutanguliza uzalendo katika kufanya mapitio ya Sera ya Kitaifa ya Ugatuaji wa Madaraka.

Dkt. Gwajima ameyasema hayo mapema leo wakati wa kufungua kikao kazi cha Wakurugenzi wa Wizara zote wa Sera na Mipango  ambao wamekutana Jijini Dodoma kupitia Sera ya Taifa ya Ugatuaji wa Madaraka na Programmu ya kuimarisha Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa.

Dkt Gwajima amesema kuwa Wakurugenzi wote waliohudhuria kikao hiki ni wabobezi wa masuala ya mipango na bajeti katika Wizara zeo hivyo wanafahamu mahitaji ya wananchi halkadhalika mahitaji ya Wizara wanazofanyia kazi kwa upana wake kwahiyo wako katika nafasi nzuri ya kupitia Sera hii na kutoa mawazo yenye tija kwa manufaa ya Nchi yetu.

“Kazi hii ni nyeti sana kwa mustakabali wa Taifa letu, mnatakiwa mjitoe kwa dhati na muweke uzalendo mbele ili kulinda maslahi ya Nchi yetu, mjitume haswa katika kufanya kazi hii kwa weledi na moyo wote kwa sababu ninyi ndio wataalamu katika eneo hili; Makundi mengine yamepitia Sera hii lakini ninyi ni wataalamu na wabobezi wa Sera hivyo mchango wenu wenye ni muhimu sana kwa mafanikio ya Sera hii” alisisitiza Dkt. Gwajima.

Akizungumzia mafanikio ya Sera iliyokwisha muda wake Gwajima amesema Sera hiyo ilisaidia katika ongezeko la uelewa na ushiriki wa wananchi katika shughuli za maendeleo na utawala, iliongeza ari ya Wananchi katika kujitegemea kupitia upangaji wa Mipango na kuimarika kwa taratibu za kuwajibisha watumishi na viongozi katika ngazi husika.

Gwajima aliongeza kuwa Sera hii pia ilisaidia kuboresha utoaji wa huduma ikiwemo Elimu, Afya, Maji, Miundombinu, biashara, makazi na ustawi wa jamii pamoja na kuimarika kwa uwajibikaji wa watumishi kwa kuwa wanasimamiwa katika ngazi ya msingi.


Wakati huo huo Gwajima alibanaisha changamoto za Sera hiyo kuwa ni pamoja na kuwepo kwa mitazamo inayokinzana kati ya watendaji na viongozi wa kisiasa katika ngazi za vijiji, Kata na halmashauri katika kuweka vipaumbele na kutekeleza miradi ya maendeleo na Mamlaka za Serikali za Mitaa kutegemea fedha kwa kiasi kikubwa kutoka Serikali Kuu.

Aliongeza kuwa Wizara za kisekta kutopeleka fedha zinazoendana na majukumu yaliyogatuliwa, mfumo hafifu wa mawasiliano kwa baadhi ya Wizara za Kisekta na OR-TAMISEMI pamoja kuwepo kwa Sera ya Ugatuaji iliyojengwa kwenye mfumo wa kisheria inayoelekeza mipaka, majukumu na utaratibu wa utekelezaji wake.

Naye Mkurugenzi wa Uratibu wa Sekta OR-TAMISEMI Dr. Andrew Komba amesema kuwa Sera iliyopo sasa ni ya mwaka 1998 hivyo imekwisha muda wake na kuna kila sababu ya kufanya mapitio ya Sera hiyo ili kuendana na mahitaji ya sasa na mabadiliko yaliyopo sasa.

“Tumehakikisha kuwa Sera ya sasa imefanyia kazi changamoto zote zilizojitokeza katika utekelezaji wa Sera iliyokwisha muda wake na itajikita zaidi katika ujenzi wa uchumi katika Mamlaka za Serikali za Mitaa kwa kujenga uchumi wa jamii na pia imejikita katika ushirikishwaji wa sekta binafsi pamoja na asasi zisizo za Kiserikali katika kutoa huduma bora kwa jamii.

Kwa kuwa sasa tunaelekea katika Uchumi wa Viwanda tumehakikisha Sera hii inajielekeza katika ushiriki kikamilifu katika ujenzi wa viwanda na inalenga maridhino ya makundi yote yaani Serikali, Sekta binafsi, Asasi zisizo za kiserikali, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa” alisisitiza Dr. Komba

Kikao hiki cha siku mbili kitapitia na kujadili rasimu ya Sera ya Ugatuaji wa madaraka kwa wananchi, mkakati wa utekelezaji wa Sera pamoja na Programu ya kuimarisha Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa.

Mwisho.


Matangazo

  • Orodha ya waliopata vibali vya Uhamisho Septemba - Disemba 2022 (OR - TAMISEMI) January 21, 2023
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kidato cha Kwanza Waliorudia Mtihani January 15, 2023
  • Matumizi ya Lugha ya Kiswahili na Kingereza January 14, 2023
  • Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Kwanza 2023 December 14, 2022
  • Orodha ya Waliopangwa kwenye Vituo vya Kazi Kada za Afya (Awamu ya Pili) Agosti 2022 August 30, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA KWA KADA ZA AFYA (Marudio) July 20, 2022
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • BODI YA MIKOPO YA SERIKALI ZA MITAA KUSUKWA UPYA

    January 23, 2023
  • MAKAMU WA RAIS AWAPONGEZA DODOMA JIJI KWA UWEKEZAJI

    January 20, 2023
  • SERIKALA YASISITIZA KILA MMOJA KUTUNZA MAZINGIRA

    January 20, 2023
  • TANZANIA ITAENDELEA KUSHIRIKANA NA WADAU KATIKA MAPAMBANO DHIDI YA UKIMWI

    January 20, 2023
  • Angalia zote

Video

Taarifa ya Ukusanyaji wa Mapato ya Halmashauri, kipindi cha robo ya pili ya mwaka wa fedha 2021/22
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.