• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Malalamiko |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
  • Kuhusu Sisi
    • Local Government History
    • Kuhusu Wizara
      • Directories
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi na Programu
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Speech
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Machapisho ya Halmashauri
  • Machapisho
    • Taarifa Mbalimbali
    • Taarifa za Mapato
    • Majarida
    • Fomu Mbali mbali
    • Presentations
  • Miongozo
    • Miongozo OR TAMISEMI
    • Miongozo ya mradi wa SEQUIP
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Michoro ya Ujenzi
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali

Bil 20 Zakusanywa Ada ya Vitambulisho vya Wajasiriamali

Imewekwa tar.: May 14th, 2019

TAKRIBANI Sh bilioni 20.3 zimefikishwa kwenye mfumo wa malipo wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) baada ya kugawa vitambulisho vya wajasiliamali vipatavyo 1,022,178.

Hayo yamebainishwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Selemani Jafo alipokuwa akizungumza na wakuu wa mikoa kabla ya kupitia tathimini ya ugawaji wa vitambulisho hivyo kwa wajasiriamali.

Jafo alisema kuwa kwa wakuu wa mikoa kugawa vitambulisho hiyo 1,022,178, wajasiriamali wameweza kuchangia Sh bilioni 20.44 ambapo Sh bilioni 20.3 ndizo zilizoingizwa kwenye mfumo wa TRA na takribani Sh milioni 135.6 bado ziko mikononi wa wakusanyaji.

“ Mpaka kufikia Aprili 30 mwaka huu kiasi cha Sh milioni 942.47 zilikuwa bado haijaingia kwenye mfumo wa mapato wa TRA, lakini nashukuru ndani ya siku mbili hizi tatu wakuu wa mikoa wameweza kuzifikisha kwenye mfumo fedha nyingi zaidi, niwapongeze kwa hilo.’

Jafo alisema endapo fedha zinazokusanywa kutokana na vitambulisho vya wajasiriamali hazitaingia kwenye mfumo wa mapato wa TRA basi fedha hizo zinakuwa mbichi na kuna hatari ya kuwapo upotevu au kutumika katika matumizi yasiyopangwa.

“ Nitumie fursa hii kuwahimiza wakuu wa mikoa na watendaji ambayo wamekusanya fedha za vitambulisho vya wajasiriamali na kutoziingiza kwenye mfumo wa malipo wa TRA kufanya hivyo mara moja,” alisema

 Aidha, Jafo aliwataka wakuu wa mikoa katika kuhakikisha azima ya Rais John Magufuli ya kutaka wafanyabiashara wadogo watambuliwe na kuwaondolewa usumbufu wanapofanya biashara zao na kushiriki katika uchumi wa nchi kwa kuwaelimisha faida ya kuwa na vitambulisho hiyo.

“ Rais John Magufuli kiu yake ni kuwalinda wafanyabiashara wadogo na kuwaona kuwa na sehemu ya kukuza uchumi wa nchi, alitaka wafanyabiashara wadogo waondokane na adhana zilizokuwa zikiwapata kupitia askari wa majiji ambao walikuwa wakitaifisha bidhaa zao na wakati mwingine kugawana jambo ambalo haikuwa ni haki,”

Kwa awamu ya kwanza na ya pili, vitambulishi vipatavyo 1,850,000 ambavyo vilikuwa na thamani ya Sh bilioni 37 vilitolewa na mpaka Aprili 30 mwaka huu, vitambulisho 1,022,178 vyenye thamani ya Sh bilioni 20.44 vimetolewa kwa wafanyabiashara wadogo.

Aidha, Jafo aliipongeza mikoa ambayo imefanya vizuri katika ugawaji wa vitambulisho vya wajasiriamali na ambayo ni Dar es Salaam iliyogawa vitambulisho kwa asilimia 95.2. Tabora kwa asilimia 94.58, Kilimanjaro kwa asilimia 79.05, Pwani kwa asilimia 77.66 na Tanga kwa asilimia 72.

Mikoa ambayo imefanya viabaya na asilimia zake kwenye mabano ni Katavi(asilimia 5.96), Njombe (asilimia 11.14), Rukwa (asilimia 25.03), Iringa(asilimia 30.74) na Lindi (asilimia 33.58).

“ Tunajua changamoto ya baadhi ya mikoa na ndio maana tuko hapa tufanye tathimini ya ugawaji wa vitambulisho hivyo, lengo letu ni kuwa lengo la Rais la kuwalinda wale wasio na sauti lifikiwe kwa wajasiriamali wadogo kutambuliwa,” alisema.

Mkuu wa mkoa wa Tabora, Aggrey Mwandri alisema utaratibu wa kutoa vitambulisho hivyo ulikuwa mgumu hasa kutokana na wananchi kuwa na dhana ya kuwa Serikali inatumia vitambulisho hivyo kuwalipisha kodi.

 “ Ukweli ulikuwa ni kuwa kiasi cha Sh 20,000 ni cha kugharamia uchapishaji wa vitambulisho, lakini wengi waliona kuwa ni njia ya kuwalipisha kodi.

Mwandri aliongeza: “ Tuliweza kufanikiwa kwa kiasi hicho kwa kuwashirikisha viongozi wa kimila, dini na watendaji kuanzia ngazi ya kitongoji, na tukaitisha mikutano ya adhara ya kutoa elimu, na baada ya hapo mwitiko wa wananchi ukawa mkubwa.”

Matangazo

  • ORODHA YA WAKUU WA KITENGO CHA FEDHA YENYE MABADILIKO 5-5-2022 May 06, 2022
  • Kazi za muda za makarani na wasimamizi wa Sensa 2022 May 05, 2022
  • MUDA WA NYONGEZA MAOMBI YA AJIRA ZA TAMISEMI 2022 May 04, 2022
  • Taarifa ya Kitengo Manunuzi na Ugavi, April 2022 April 04, 2022
  • Safeguard Documents for TACTIC Project March 30, 2022
  • Miongozo ya Operesheni Anwani za Makazi March 24, 2022
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • SOMO LA TEHEMA LIMERAHISISHA UTOAJI WA ELIMU MASHULENI KUPITIA MEWAKA

    May 19, 2022
  • Bashungwa apongeza ongezeko la Mishahara kwa watumishi nchini

    May 18, 2022
  • WALIMU WAMEIOMBA SERIKALI KUENDELEA NA MAFUNZO YA MEWAKA

    May 17, 2022
  • BASHUNGWA ATOA SIKU 30 TARURA KUFANYA USANIFU WA BARABARA YA SUCA - GOLANI ILI IWEKEWE LAMI.

    May 14, 2022
  • Angalia zote

Video

Taarifa ya Ukusanyaji wa Mapato ya Halmashauri, kipindi cha robo ya pili ya mwaka wa fedha 2021/22
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi ( LIVE)
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Tume ya Ajira Tanzania
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.