Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

Zingatieni haya kwenye Hospitali Mpya 28 - Dkt. Ntuli

Imewekwa tar.: July 6th, 2020

Na. Atley Kuni-OR-TAMISEMI

Mkurugenzi wa Afya na Ustawi wa Jamii Ofisi ya Rais TAMISEMI, Daktari Ntuli Kapologwe, akiwa na jopo la wataalamu kutoka Ofisi hiyo, wamelazimika kutoa maelekezo muhimu yakuzingatia katika Hospitali mpya 28 za Halmashauri zinazoendelea kujengwa hivi sasa baada ya Halmashauri husika kupatiwa fedha na serikali kiasi cha milioni 500 za kuanzia.

Akifanya majumuisho hayo Dkt. Ntuli, amesema kwanza wamefurahishwa na utayari wa wanachi katika maeneo yao kwakujitolea kushiriki ujenzi huo unaoendeshwa kwa mtindo wa force account, kwani umeonesha mafaniko makubwa kote nchini, lakini akatahadharisha Kamati za Afya za Mikoa na Halmashauri, kuhakikisha zinaendelea kuwa bega kwa bega na timu za ujenzi shabaha ikiwa ni kuondokana na hatari yakukosewa kosewa kwa majengo hayo na hivyo kufanya kazi mara mbili lakini pia kuongeza gharama za ujenzi.  

Katika ziara hiyo iliyochukua muda wa siku 14, Dkt. Ntuli, amezitaka Kamati hizo kuhakikisha majengo yanazingatia ramani zilizopo lakini pale inapo lazimu kushauri, basi wasisite kufanya hivyo kwani kwa kufanya hivyo itasaidia kutambua kasoro mapema.

Dkt. Kapologwe ameyataja maeneo ya kuta za Chumba cha Mionzi (X-Ray) kuwa zinatakiwa ziwe na unene usiopungua 300mm na Dirisha lake la kuingizia mwanga, liwe angalau Mita 2 kutoka kwenye floor Sehemu ya kuchukulia mionzi huku akitoa tahadhari kwa jengo hilo kuwekewa Aluminum au Grill na badala yake wazingatie kuwa eneo hilo litawekewa lead glass.

Amesema chumba hicho, kinatakiwa kuwa na mlango maalum ambao huwa unawekwa ili kuwazuia watoa huduma pamoja na wateja kutodhurika na mionzi itokanayo na mionzi isiyo dhibitiwa na kusema kwamba, wasitumie milango inayotumika katika nyumba zakuishi na badala yake watumie milango maalum na  

Dkt. Ntuli amesema sehemu za kufanyia kazi Works shop za Maabara zinatakiwa kuwa na Marbles na sio marumaru (tiles), aidha Marbles zilizopendekezwa ni vema zikawa na rangi nyeupe.

“Kwa upande wa Floor za Operating Theatre zinatakiwa kuwa na Epoxy mpaka eneo la sluice na sio marumaru za kawaida, huku akisema, madirisha ya Chumba cha upasuaji yanatakiwa kuwa na Grill Kwa nje na ndani, amesema Dkt. Ntuli, na kuzidi kusisitiza eneo la ndani kuwe na madirisha ya aluminium yasiyofunguka (fixed panels) na vioo viwe ni frosted glass, yaani visivyomuwezesha mtu wa nje kuona ndani.” Amesema, Mkurugenzi Ntuli.

Dkt. Ntuli, amesema pia mawasiliano kati ya Chumba cha kutakasia vifaa na Chumba cha Sluice liwekwe Dirisha na sio Mlango sambamba na tundu la nchi tatu ili kuweza kupitishia bomba la kutolea gas, pindi anapotakasa vyombo, amesisitiza mpangalio wa majengo vizuri ili kuwa na ufanisi wakati wa utoaji huduma, akitolea mfano, Jengo la Wagonjwa wa Nje (OPD)  linatakiwa kuwa uelekeo wa kuangalia Bara bara kuu na nyuma yake likifuatiwa na Jengo la Maabara.

Katika Majumuisho hayo Dkt. Ntuli amesema, Vituo vya kutolea huduma vinavyojengwa au karabatiwa vinatakiwa kuwa na tenki la kuhifadhia maji lenye uwezo wa ujazo usiopungua lita elfu 50, huku akipendekeza majengo yote yaunganishwe na Walk Way ili kurahisishia kazi kumtoa huduma  kutoka eneo moja kwenda eneo jingine.

Akiwa anahitimisha majumuisho hayo Dkt. Ntuli amesema, paa la Jengo la stoo ya dawa, linatakiwa kuwa na Materials maalumu ya kuzuia jotokali katika eneo husika, na kwa upande wa vyoo vya Walemavu, pamoja na maeneo yakupitia amesema kwamba, nilazima yawe na Supports pembeni kwa ajili ya kumsaidia mlemavu aendapo haja, vilevile akitaka, majengo yote sehemu ya kuingilia yawe na ramp kwa ajili ya Walemavu.

Mwisho Dkt. Ntuli, amesema katika chumba cha upasuaji milango yote inayoingia au kutoka wahakikishe   ni ya solid core flush doors, yenye spring hinges zinazofunguka pande zote, isiwe na vitasa bali push plates zilizofungwa pande zote za mlango.

Hivi sasa Ofisi ya Rais-TAMISEMI, inaendelea na zoezi la ufatiliaji wa Hospitali 28 za Halmashauri ambazo zimewekwa katika mpango wa awamu ya pili ukitanguliwa na Hospitali 67 za awamu ya kwanza ambapo  tayari Hospitali 45 zimeanza kutoa huduma kwa wananchi hadi kufikia Mwezi Julai, 2020.


Matangazo

  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert (extension) 1 May 28, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert (extension) May 28, 2025
  • TOR - Msimbazi Watershed Management – Modelling May 26, 2025
  • Monitoring & Support, TOR - DMDP 2 SWM Service Framework & Delivery System in Dar May 26, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • RC CHALAMILA ATAKA MACHINGA KARIAKOO KUFUNGUA NJIA

    May 30, 2025
  • Wamiliki wa vituo vya kulelea watoto wadogo mchana watakiwa kuzingatia miongozo na kanuni zilizopo.

    May 29, 2025
  • Mhe. Katimba awapokea Wabunge wa Zambia waliokuja kujifunza kuhusu Usimamizi na Uendeshaji wa Mamlaka za Serikali za Mitaa Tanzania Bara

    May 28, 2025
  • Mtwale Atoa Mwongozo kwa Makatibu Tawala Wasaidizi wa Mikoa

    May 27, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.