Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

Waziri Jafo, Aongoza Mawaziri utatuzi wa Mgogoro wa Hifadhi Makere kusini

Imewekwa tar.: January 7th, 2019

Mawaziri watano wakioongozwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI, Suleiman Jafo wamekagua hifadhi ya Msitu wa Makere Kusini, uliopo wilaya ya Kasulu mkoa wa Kigoma kwa takriban saa tano ili kubaini changamoto mbalimbali za msitu huo na kuzipatia ufumbuzi.

Mawaziri wengingine mbali ya Mhe. Seleman Jafo, ni Waziri wa Maliasili na Utalii Dk Hamis Kigwangala, Waziri wa Mifugo na Uvuvi Luhaga Mpina, Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dk. Angeline Mabula pamoja na Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira Musa Sima.

Ziara ya mawaziri hao katika hifadhi ya msitu huo ambao pia unatambulika kama Msitu wa Kagera Nkanda ambao niwa kihistoria kutokea hapa nchini ilianza majira ya saa saba mchana jana wakati Mawaziri hao walipokuwa wakitokea wilayani Kigoma ambapo walikuwa na kikao cha utatuzi wa mgogoro wa matumizi ya ardhi katika hifadhi ya Msitu na Pori la Akiba la Moyowosi la mkoani Kigoma na kumalizika kwa ukaguzi majira ya saa kumi na mbili jioni.

Baada ya kumalizika kwa ukaguzi katika Msitu wa Makere Kusini, Mawaziri hao watano walielekea kijiji cha Kabulanzwili na kukagua mpaka baina ya kijiji hicho na hifadhi ya msitu huo kwenye mto Migezibiri na baadaye kukutana na wananchi wa kijiji hicho kwa lengo la kuwaeleza nia ya serikali kunusuru hifadhi ya msitu ambapo walizungumza nao hadi saa moja na nusu usiku.

Wakiwa katika kijiji cha Kabulanzwili waliwapokelewa na wananchi walikuwa na   mabango huku wananchi wakionesha kutoridhishwa na hatua zinazochukuliwa na askari wa wanyama pori katika eneo hilo kwa kuwaondoa kwa nguvu wananchi wanaoendesha shughuli za kilimo na ufugaji kwenye hifadhi hiyo, huku baadhi yao wakidai kutofahamu mipaka halisi baina ya kijiji na hifadhi katika eneo hilo.

Ziara ya viongozi hao ilikwenda sambamba na kufikia maazimio tisa kwa ajili yakunusuru misitu lakini pia kumaliza migogoro iliyokuwepo baina ya serikali na wananchi hao, maazimio yaliyofikiwa ni pamoja na;

Serikali itaendesha Operesheni kubwa kuondoa uvamizi wa wakulima, wafugaji na watu wengine wanaofanya shughuli zisizo halali kwenye misitu na mapori yaliyohifadhiwa kisheria zikiwemo hifadhi za misitu ya serikali kuu, hifadhi za misitu za halmashauri za wilaya na vijiji. Hivyo, wavamizi wote wanaoishi au kuendesha shughuli zozote kwenye mapori na misitu hiyo waondoke mara moja kwa hiyari kabla ya zoezi la kuwaondoa kwa lazima. Operesheni hiyo itafanyika wakati wowote ndani ya kipindi cha miezi sita (6) kuanzia Januari 2019. Hata hivyo, imeshauriwa kwa wakulima ambao tayari wana mazao katika mapori na hifadhi husika wanaweza kuomba idhini maalum ya kuvuna mazao yao.


Azimio linguine ni kwamba, Serikali imemega jumla ya hekta 10,012.61 kutoka kwenye Hifadhi ya Msitu wa Makere Kusini kwa ajili ya kilimo na mipango ya Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu ambapo Hekta 2,174 (ekari 5,435) zimetolewa kwa Kijiji cha Mvinza, Hekta 2,496 (ekari 6,240) zimetolewa kwa Kijiji cha Kagerankanda na Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu Hekta 5,342.61 (ekari 13,356.525). Eneo hili lilitolewa na Mhe. Rais ili litumike kwa ajili ya shughuli za kilimo na ufugaji. Serikali itaandaa mpango mahsusi wa matumizi bora ya ardhi ili kuwezesha zoezi la ugawaji kufanyika vizuri.


Taarifa iliyotolewa kwa umma imesema, Wizara ya Mifugo na Uvuvi imetenga jumla ya hekta 20,000 kutoka katika maeneo mbalimbali katika Mkoa wa Kigoma kwa ajili ya ufugaji wenye tija aidha serikali itaendelea kutafuta maeneo mengine kwa ufugaji wenye tija.


Ilikuweka kuwa na msimamo wa pamoja Serikali imesisitiza kuimarisha utekelezaji wa sheria zinazohusu wakimbizi ili kuhakikisha hawachangii uharibifu wa mazingira, maliasili na usalama;

Maazimio mengine ni kuwa ilibainika wahamiaji haramu kutoka nje ya nchi wamekuwa wakichangia katika uharibifu wa misitu na mapori hivyo serikali imesema wahamiaji hao haramu wataondolewa nchini mara moja kwa kutumia sharia za nchi zilizopo.

Serikali imesema pia wananchi wote waliovamia eneo lililoko kwenye mpango wa uanzishwaji wa vitalu vya ufugaji na mashamba ya kilimo katika Halmashauri ya Wilaya ya Uvinza (Mwanduhubanhu) watapangwa na mamlaka husika kwa ufugaji na kilimo chenye tija, mara baada ya tathimini iliyoelekezwa na Waziri wa Mifugo kukamilika;

Sambamba na hayo hapo juu, Serikali itasaidia vijiji katika maeneo yao kuandaa mipango ya matumizi bora ya ardhi na katika mipango hiyo watenge maeneo kwa ajili ya ufugaji na kilimo kulingana na mahitaji yao;

Katika hatua nyingine maazimio hayo ya serikali kupitia Mwaziri wake, imesema, Mamlaka za Serikali za Mitaa zenye mashamba ambayo hayajaendelezwa zihakikishe taratibu za ubatilisho wa miliki hizo umefanyika ili ardhi itakayopatikana ipangwe kwa matumizi ya kilimo na ufugaji wenye tija huku iki utaka uongozi wa Mkoa na Wilaya uhakikishe kuwa usafirishaji wa mifugo unazingatia Sheria ya Utambuzi, Usajili na Ufuatiliaji wa Mifugo Na. 12 ya mwaka 2010.

Hii ni mara ya kwanza kwa Wizara hizo kukutana mkoani humo na kutafuta suluhu ya migogoro ya hifadhi hapa nchini.


Matangazo

  • TOR - Msimbazi Watershed Management – Modelling May 26, 2025
  • Monitoring & Support, TOR - DMDP 2 SWM Service Framework & Delivery System in Dar May 26, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert May 12, 2025
  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert May 12, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • Nipo tayari kufanya kazi pamoja nanyi kufikia malengo ya Mhe. Rais – Prof. Tumaini Nagu

    May 26, 2025
  • TARURA IMEKUWA NA MCHANGO MKUBWA KWA SERIKALI YA AWAMU YA SITA

    May 26, 2025
  • MAPEPELE AWANOA MAAFISA HABARI WA TAMISEMI, AWATAKA WAWE WAZALENDO 

    May 26, 2025
  • MAHUSIANO MAZURI  NI NGUZO MUHIMU KATIKA UTEKELEZAJI WA MAJUKUMU-MHE.SAGINI

    May 26, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.