Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

Wanafunzi kuanza kuimba nyimbo za kuhamasisha uzalendo wiki ijayo

Imewekwa tar.: July 3rd, 2019

Na Mathew Kwembe, Mtwara

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe.Selemani Jafo amewataka Maafisa elimu wa mikoa, na wilaya kuhakikisha kuwa kuanzia wiki ijayo julai 8, wanasimamia agizo la serikali linalowataka wanafunzi wote wanaosoma katika shule za msingi na sekondari zilizo chini ya Ofisi yake, kuimba nyimbo tatu za kuhamasisha uzalendo kila siku asubuhi kabla ya kuanza masomo.

Akifunga  mashindano ya Umoja wa Michezo ya Shule za Sekondari (UMISSETA) na yale  ya Umoja wa Michezo na Taaluma kwa Shule za Msingi (UMITASHUMTA) yaliyofanyika kwenye uwanja wa Nangwanda mjini Mtwara jana, Mhe.Jafo amesema kuwa kuanzia jumatatu ijayo, pindi shule zitakapofunguliwa maafisa elimu wa mikoa, wilaya na maafisa utamaduni wahakikishe kuwa wanafunzi wanaimba wimbo wa Taifa, wimbo wa tazama ramani, na wimbo wa Tanzania, Tanzania.

Ameongeza kuwa nyimbo hizi ni nzuri sana kwani zikiimbwa kwa pamoja zinaweza kumtoa mtu machozi kwani kielelezo cha kujenga umoja na utaifa kwa watanzania.

“Nyimbo hizi zinajenga umoja wetu, zinajenga utaifa wetu, lakini siyo wote wanaoweza kuimba nyimbo hizo, wengine wakianza kuimba nyimbo hizo wanaishia kugugumia gumia tu,” amesema Mhe.Jafo

Waziri Jafo amesema kuwa uamuzi wa kuagiza nyimbo hizo ziimbwe na wanafunzi kila siku asubuhi kabla ya kuanza masomo unalenga kujenga uelewa kwa wanafunzi ili waweze kuzielewa na kuziimba kwa ufasaha nyimbo hizo zinazojenga utaifa na umoja wa Tanzania.

Hivyo Mhe.Jafo ameagiza kuwa shule zote ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania zilizo chini ya Ofisi ya Rais TAMISEMI zihakikishe kuwa wanafunzi wake wanaimba nyimbo hizo tatu kila siku asubuhi kabla ya kuanza masomo ili kuhamasisha uzalendo, kujenga umoja na utaifa kwa wanafunzi.

Amesema maafisa elimu wahakikishe kuwa wanasimamia utekelezaji wa agizo hilo la serikali na wawafundishe wanafunzi wao ili waweze kuimba kwa ufasaha nyimbo hizo tatu za wimbo wa taifa, Tanzania Tanzania, na Tazama ramani.

Mhe.Jafo amesema kuwa licha ya ugumu utakaojitokeza mwanzoni mwa utekelezaji wa agizo hilo kwa kuzingatia kuwa hata baadhi ya walimu wanaweza wasiimbe kwa ufasaha nyimbo hizo, viongozi hao wanapaswa kuhakikisha kuwa agizo hilo linatekelezwa kwa shule zote nchini.

“Ninajua mtakapoanza jambo hili pengine, hata baadhi ya walimu watakuwa hawajui kuimba nyimbo hizo, nitoe maelekezo kuwa kila shule iwe na nyimbo hizo na ziimbwe kila siku asubuhi ili kujenga umoja na utaifa wetu watanzania,” amesema.

Mhe.Jafo amesisitiza kuwa hata atakapokuwa akifanya ziara zake shuleni jambo la kwanza kabla ya kufanya ukaguzi wowote litakuwa ni kuhakikisha kuwa anasikiliza jinsi vijana katika shule atakazotembelea wanavyoziimba.

Ameongeza kuwa serikali inaamini kuwa maafisa elimu mikoa, wilaya, maafisa utamaduni na wakuu wa shule, na walimu wakuu watasimamia utekelezaji wa agizo hilo ili kuwawezesha wanafunzi wa kitanzania kuweza kuimba nyimbo hizo kwa ufasaha.

“Hatutaki kuona vijana ambao wanapoteza hata uzalendo, hawajui hata kuimba wimbo wa taifa, tutengeneze uzalendo wetu, tutengeneze utaifa wetu kama taifa letu, imani yangu jambo hili litaleta faraja,” amesema.

Kuhusu mashindano ya UMISSETA na UMITASHUMTA Mhe. Jafo amesema kuwa Ofisi ya Rais TAMISEMI itaendelea kuhakikisha kuwa michezo hii inaendelea kudumishwa kwa nguvu zote kwa kuhakikisha vipaji vya wanafunzi vinaendelezwa.

Aidha Mhe.Jafo amemwagiza Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI kuhakikisha kuwa taarifa za wanafunzi wote walioshiriki UMISSETA na UMITASHUMTA mwaka huu zinahifadhiwa katika kanzi data ya wizara na akataka kazi hiyo ikamilishwe ndani ya wiki mbili kuanzia sasa.

   

Matangazo

  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert (extension) 1 May 28, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert (extension) May 28, 2025
  • TOR - Msimbazi Watershed Management – Modelling May 26, 2025
  • Monitoring & Support, TOR - DMDP 2 SWM Service Framework & Delivery System in Dar May 26, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • RC CHALAMILA ATAKA MACHINGA KARIAKOO KUFUNGUA NJIA

    May 30, 2025
  • Wamiliki wa vituo vya kulelea watoto wadogo mchana watakiwa kuzingatia miongozo na kanuni zilizopo.

    May 29, 2025
  • Mhe. Katimba awapokea Wabunge wa Zambia waliokuja kujifunza kuhusu Usimamizi na Uendeshaji wa Mamlaka za Serikali za Mitaa Tanzania Bara

    May 28, 2025
  • Mtwale Atoa Mwongozo kwa Makatibu Tawala Wasaidizi wa Mikoa

    May 27, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.