• Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Machapisho
    • Taarifa za Mapato
    • Majarida
    • Fomu Mbali mbali
    • Presentations
  • Miongozo
    • Miongozo OR TAMISEMI
    • Miongozo ya mradi wa SEQUIP
    • Green and Smart Cities
    • Miongozo ya Kilimo
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Michoro ya Ujenzi
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)

Wakurugenzi zingatieni miongozo ili kudhibiti matumizi mabaya ya fedha za umma

Imewekwa tar.: January 30th, 2019

Majid Abdulkarim na Mathew Kwembe

Serikali imewataka Wakurugenzi wa Halmashauri kuzingatia sheria, taratibu na miongozo ya matumizi ya fedha za serikali ili kupunguza matumizi mabaya ya fedha za serikali zinazotolewa kwa ajili ya Elimu.

Akifunga mafunzo elekezi kuhusu utekelezaji wa mradi wa lipa kulingana na matokeo katika Sekta ya Elimu (EP4R) jana jijini Dodoma, Naibu Waziri, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Afya)  Mhe. Josephat Sinkamba Kandege alisema kuwa serikali itahakikisha kuwa hakuna shilingi hata moja itakayopotea wakati wa utekelezaji wa miradi hiyo.

Alisema kuwa serikali ya awamu ya tano imedhamiria kuhakikisha kuwa fedha yote itakayotolewa kwa ajili ya miradi inayopelekwa halmashauri ama iwe imetoka serikalini au kwa wahisani haitumiki kinyume na malengo yaliyokusudiwa

“Kila shilingi tunataka iwe na tija, hivyo nawataka wakurugenzi wa halmashauri na watendaji wengine mhakikishe kuwa mnafuata miongozo ili muepuke hoja za ukaguzi,” alisema

Aliongeza kuwa kila kiongozi  anatakiwa  kufanya kazi kwa weledi  na kuacha tabia ya kufanyakazi kwa mazoea na kuzingatia  miongozo na maelekezo  ya matumizi ya fedha zinazotolewa na Serikali  pamoja na wadau wa maendeleo  ili kuepuka hoja za wakaguzi.

Pia aliwaagiza watendaji hao kusimamia  na  kufatilia utekelezaji wa miradi hasa ujenzi wa miundombinu ya shule ili ikamilike kwa wakati  na kuwashirikisha  kamati, bodi na jamii inayozuguka  katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo na  kupunguza ghalama zisizoza msingi, kutoa ajira kwa jamii husika na kuharakisha katika utekelezaji wa miradi hiyo.

Alisema matumizi ya fedha yanayotumika katika miradi husika yaendane na thamani ya mradi husika ili kuhakikisha sekta ya elimu inapata matokeo chanya.

Aidha Mhe. Kandege alisema ili kuthibiti ubora wa elimu nchini halmashauri  zihakikishe shule zinakaguliwa kwa wakati  muafaka na changamoto zinazobainishwa na wathibiti ubora zifanyiwe kazi haraka ili watoto wa kitanzania wapate elimu bora.

“Wakaguzi wa Halmashauri toeni ushirikiano kwa wathibiti Ubora wa Elimu na Mafunzo elekezi kwa wakuu wa shule juu ya umuhimu wa kutekeleza ukaguzi wa ndani ya shule pale panapo kuwa na changamoto mawasiliano  yafanyike kwa wakati kupitia  Ofisi ya Mkoa ili  muweze kufikia malengo ya pamoja,” alisema.

Mapema kabla ya kumkaribisha Naibu Waziri kufunga kikao hicho, Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Usimamizi wa  Elimu kutoka Ofisi ya Rais TAMISEMI anayeshughulikia Elimu ya Msingi Dkt. George Jidamva alisema changamoto kubwa waliyoiona kwenye utekelezaji wa mradi huo ni kwa baadhi ya watendaji kushindwa kujibu hoja za ukaguzi kwa kukosa vielelezo muhimu kama risiti na orodha ya malipo.

Changamoto nyingine ni kutofautiana kwa ubora wa majengo kati ya halmashauri na halmashauri licha ya kuwa ramani za miundombinu hiyo kufanana na hivyo kukosekana kwa thamani ya ubora kutokana na baadhi ya majengo kujengwa chini ya kiwango.

Mradi lipa kulingana na matokeo katika sekta ya elimu ( EP4R) ulianza Septemba, 2014 kwenye Mamlaka za serikali za mitaa kwa kupokea kiasi cha shilling bilioni 77.98 na kwa sasa halmashauri hizo zinatarajia kupokea kiasi cha shilling biloni 40 kutoka kwa wadau wa maendeleo ambazo zitatumika  kwa mujibu wa maelekezo yatakayo tolewa na mamlaka husika.

Matangazo

  • Orodha ya waliopata vibali vya Uhamisho Septemba - Disemba 2022 (OR - TAMISEMI) January 21, 2023
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kidato cha Kwanza Waliorudia Mtihani January 15, 2023
  • Matumizi ya Lugha ya Kiswahili na Kingereza January 14, 2023
  • Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Kwanza 2023 December 14, 2022
  • Orodha ya Waliopangwa kwenye Vituo vya Kazi Kada za Afya (Awamu ya Pili) Agosti 2022 August 30, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA KWA KADA ZA AFYA (Marudio) July 20, 2022
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • BODI YA MIKOPO YA SERIKALI ZA MITAA KUSUKWA UPYA

    January 23, 2023
  • MAKAMU WA RAIS AWAPONGEZA DODOMA JIJI KWA UWEKEZAJI

    January 20, 2023
  • SERIKALA YASISITIZA KILA MMOJA KUTUNZA MAZINGIRA

    January 20, 2023
  • TANZANIA ITAENDELEA KUSHIRIKANA NA WADAU KATIKA MAPAMBANO DHIDI YA UKIMWI

    January 20, 2023
  • Angalia zote

Video

Taarifa ya Ukusanyaji wa Mapato ya Halmashauri, kipindi cha robo ya pili ya mwaka wa fedha 2021/22
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.