Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

Wakurugenzi Mamlaka za Serikali za Mitaa watiwa Mtegoni

Imewekwa tar.: January 7th, 2021

Na Atley Kuni, KAGERA

Wakurugenzi katika Mamlaka za Serikali za mitaa nchini, wamewekwa katika sintofahamu ya nyadhifa zao pamoja na wasaidizi wao endapo watashindwa kufikia viwango vya makusanyo ya mapato vilivyo kubalika kwa mwaka wa fedha 2020/21 ambacho ni asilimia 85.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Mhe.Selemani Jafo akiongea kwa Nyakati tofauti wakati wa ziara yake kwenye Mikoa ya Kanda ya Ziwa ziara ambayo inakwenda sambamba na kufanya vikao vya ndani na watumishi, ameendelea kusisitiza kwamba, wakurugenzi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa watapimwa pamoja na vigezo vingine lakini pia suala la ukusanyaji wa Mapato kwenye Halmashauri wanazo ziongoza.

“Tangu Serikali ya awamu ya tano iingie madarakani, ajenda kubwa ya Mhe. Rais imekuwa ni ukusanyaji wa mapato, hili tumeliimba kwa kipindi chote cha miaka mitano iliyopita, sasa tufike mahali tusema basi, haiwezekani leo ni Mwezi Januari 2021, nusu ya Mwaka wa Serikali wa 2020/21 imeisha lakini  wewe Mkurugenzi na wataalam wako katika Halmashauri yenu hamjafikisha hata asilimia 30 hii ni aibu” Amesema Mhe. Jafo

Mhe. Jafo, amesema, wapo baadhi ya watendaji wanaofikiri adhabu itawagusa Wakurugenzi pekee yao, amesema kuwaza hivyo sio sahihi, bali katika wakati wa sasa adhabu hiyo itakwenda sambamba na watu wote wanaoguswa na mnyororo huo wa ukusanyaji wa mapato.

“Ndugu zangu hakuna Halmashauri ambayo itaweza kujiendesha endapo itashindwa kukusanya mapato ipasavyo, hivyo kama mwaka wa jana tuliweka wastani wa asilimia 81 lakini tukafika asilimia 94, ni matumaini yangu kwa mwaka huu haitatokea Halmashauri ikakusanya chini ya asilimia 85” alisisita Waziri Jafo.

Katika hatua nyingine, Waziri jafo, amewataka watumishi wa umma kuacha kufanya kazi kwa fitna na majungu na badala yake wajitahidi kufanya kazi kwakupendana ili waweze kuacha kumbukumbu (Legacy), pindi wanapo staafu utumishi wa umma.

“Asilimia zaidi ya 80 ya muda wenu  ninyi watumishi wa umma mnautumia, mikiwa eneo la kazi, hivyo ni rai yangu lazima muishi kwakupendana ninyi kwa ninyi, wapo baadhi ya watu, wao kila kiongozi anapofika yeye ni wa kwanza kupeleka fitna na majungu, niwaambie hiyo sio tabia nzuri, amesema Jafo.

Kuhusiana na suala la upandishaji wa vyeo kwa watumishi wa umma, Waziri Jafo amesema suala hilo lipo chini ya Himaya ya Mkurugenzi  kwa Ushirikiano wa Karibu na jopo la Menejimenti ya Halmashauri husika.

“Ndugu zangu cheo hapandishi Mkuu wa Nchi wala mimi Waziri wa Nchi, upandishwaji wa vyeo unaanzia katika ngazi unayofanyia kazi kwakuweka katika mipango ya bajeti, lakini inashangaza unakuta mtumishi hajapanda cheo kwa miaka sita na kinachofuata ni kutoa lawama kwa uongozi wa juu, kumbe tatizo lilianza kwa mkuu wako wa idara kutokukuweka katika bajeti” amesema Jafo.

Akitoa Salaam za Mkoa huo kwa nyakati tofauti, Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Mhe. Brig.Gen. Marco Gagut, amempongeza Mhe. Jafo kwa Kuchaguliwa kuwa Mbunge wa Jimbo la Kisarawe na wananchi wa Jimbo hilo, lakini akampongeza zaidi kwakuaminiwa na Mhe. Rais na kurejeshwa tena katika Ofisi hiyo kama Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI.

Waziri jafo akiwa mkoani Kagera, ametembelea Hospitali, Vituo vya Afya pamoja shule kisha kufanya mikutano miwili na watumishi wa umma katika Halmashauri za Wilaya za Biharamulo na Ngara, ambapo sehemu zote alizopita ameendelea kuwasisitiza watumishi kufanya kazi kwa kupendana na kuacha tabia ya majungu na fitna. Aidha katika ziara hiyo Mhe. Waziri Jafo ameridhishwa na kasi ya Miradi ya Maendeleo inayotekelezwa katika Mkoa wa Kagera.

MWISHO.

Matangazo

  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert (extension) 1 May 28, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert (extension) May 28, 2025
  • TOR - Msimbazi Watershed Management – Modelling May 26, 2025
  • Monitoring & Support, TOR - DMDP 2 SWM Service Framework & Delivery System in Dar May 26, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • RC CHALAMILA ATAKA MACHINGA KARIAKOO KUFUNGUA NJIA

    May 30, 2025
  • Wamiliki wa vituo vya kulelea watoto wadogo mchana watakiwa kuzingatia miongozo na kanuni zilizopo.

    May 29, 2025
  • Mhe. Katimba awapokea Wabunge wa Zambia waliokuja kujifunza kuhusu Usimamizi na Uendeshaji wa Mamlaka za Serikali za Mitaa Tanzania Bara

    May 28, 2025
  • Mtwale Atoa Mwongozo kwa Makatibu Tawala Wasaidizi wa Mikoa

    May 27, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.