Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

Waitara ahimiza wazazi na walezi wenye uwezo kuchangia maendeleo ya shule

Imewekwa tar.: July 13th, 2019

Na Mathew Kwembe, Dodoma

Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa anayeshughulikia elimu Mhe.Mwita Mwikwabe Waitara (MB) amesema kuwa serikali haijakataza michango shuleni isipokuwa ile iliyokuwa ya lazima na akataka michango hiyo ifuate mwongozo wa serikali wa kuchangia.

Akizindua jengo jipya la bwalo la chakula lililojengwa na shirika lisilo la kiserikali la CDTF jana katika shule ya msingi mlimwa iliyopo katikati ya jiji la Dodoma, Mhe.Waitara amesema kuwa wapo watu wamekuwa wakipita pita huko mitaani na kutoa tafsiri potofu kuwa Mhe.Rais wa Jamhuri ya Muungano amepiga marufuku michango yote shuleni jambo ambalo si la kweli.

Amesema kuwa michango ambayo Mhe.Rais aliyokataza ni ile ya lazima ambayo ilikuwa ikilazimisha watoto wote shuleni kuchangia ama wana uwezo au la jambo lililokuwa likisababisha watoto wanaokosa kulipia michango hiyo kutokana na wazazi au walezi wao kukosa fedha hufukuzwa shule.

“Ila nafahamu kuwa yapo baadhi ya maeneo ambapo watu wamepotosha, tunao waraka wa serikali wa mwaka 2016, unaoelekeza ni aina gani ya michango inayopaswa kutolewa, namna gani michango ifanywe, na kina nani wasimamie, “ amesema na kuongeza:

“ waraka umeeleza kuanzia mtu wa kawaida hadi ngazi ya taifa, na umeelezwa vizuri kabisa, lakini watu wenye nia zao mbaya walifanya kusudi kabisa kupotosha wazazi wasichangie,” amesema.

Mhe. Waitara ameongeza kuwa maelekezo ya serikali ni kwamba walimu washirikiane na kamati za shule, na viongozi wa serikali, wakae pamoja wajadiliane namna ya kuchangia ili wale wazazi au walezi ambao wana uwezo wa kuchangia wachangie lakini wale wasio na uwezo wasichangishwe na pia wahakikishe watoto wanaotoka familia masikini wasiondolewe madarasani kwa wazazi wao kushindwa kutoa michango.

Akizungumzia hafla hiyo ya kuzindua bwalo hilo la chakula, Mhe.Waitara amelipongeza shirika la CDTF, Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania pamoja na uongozi wa jiji la Dodoma kuhakikisha kuwa bwalo hilo linakamilika ili kuwawezesha wanafunzi wa shule hiyo kupata chakula cha mchana shuleni.

Amesema kuwa ni muhimu kwa wazazi na walezi kutambua kuwa watoto wao wanapaswa kupatiwa chakula shuleni ili waweze kusoma kwa bidii na kufaulu vizuri masomo yao.

Mhe. Waitara pia amewapongeza wazazi na walezi wa shule ya msingi Mlimwa A kwa kuitikia vizuri wito wa serikali kuhakikisha kuwa wanachangia maendeleo ya shule kwa kuwapatia uji kila siku watoto wote wanaosoma shule hiyo.

“Ndiyo maana katika taarifa ya Mwalimu Mkuu inaonyesha kuwa katika kipindi cha miaka mitatu mfululizo watoto wote wanaomaliza darasa la saba katika shule hii wameenda sekondari,”amesema.

Mhe.Waitara amesema watu wazima wanaposhiriki semina waandaaji huhakikisha kuwa washiriki wanapatiwa chai asubuhi, na mchana hupewa chakula, na akashangaa kwa nini watoto wanaosoma katika shule wasile chakula hivyo akawahimiza wazazi na walezi wa watoto wanaosoma katika shule zote nchini kuona umuhimu wa kuchangia ili watoto wao wapate chakula shuleni ili wasome kwa bidii na waweze kufaulu vizuri.

Mapema Mwalimu Mkuu wa shule ya Msingi Mlimwa Bi Salma Machaku alisema kuwa kuanzia mwaka 2016 hadi mwaka 2018 katika matokeo ya kumaliza darasa la saba katika shule hiyo ufaulu umekuwa wa asilimia 100, kadhalika pia kwa darasa la nne jambo ambalo alidai limechangiwa na uongozi mzuri wa shule hiyo.

Amesema kuwa kukamilika kwa jengo hilo lenye thamani ya shilingi 81, 592, 478 utawawezesha wanafunzi wa shule hiyo kupata chakula kwenye eneo salama, pia watumishi wataweza kuandaa chakula katika hali ya usafi, na pia ukumbi utaweza kuwaingizia kipato kupitia kuendesha mikutano mbalimbali ikiwemo ile ya shule.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa CDTF Tanzania bwana Henry Mgingi amesema mradi huo wa ukumbi mbali na shilingi milioni 81 za wahisani, pia wazazi walichangia shilingi milioni 3 na halmashauri ya jiji la Dodoma walichangia shilingi milioni 4.2 hivyo jumla ya kiasi kilichotumika kuwa shilingi milioni 88.2

Bwana Mgingi amesema kuwa mbali na ujenzi wa bwalo hilo la wanafunzi shirika lake pia lilihusika katika ujenzi wa nyumba za walimu na kuwawekea umeme wa jua katika eneo la Losinoni Arusha, na katika mkoa wa Dodoma katika shule za Mlimwa A na B, Kiwanja cha Ndege na Chikoa  katika halmashauri ya jiji la Dodoma ambapo madarasa na samani zilitolewa katika shule hizo kwa vipindi tofauti.

Shirika la CDTF lilianzishwa mwaka 1962 na Mwanamke mwenye asili ya America Bibi Marion Lady Chesham na kwa muda wote huo limekuwa likishirikiana bega kwa bega na serikali za awamu zote katika kusaidia miradi ya maendeleo.

Shirika hili linaongozwa na Mwenyekiti wa Bodi wa sasa bwana Leon Msimbe ambaye alichukua uongozi huo kutoka kwa aliyekuwa spika mstaafu Mhe.Pius Msekwa. Miongoni mwa wadhamini wa kwanza wa shirika hili ni pamoja na Marehemu Rashid Kawawa, Spika wa kwanza Adam Sapi Mkwawa na Mzee Job Lusinde.

Matangazo

  • TOR - Msimbazi Watershed Management – Modelling May 26, 2025
  • Monitoring & Support, TOR - DMDP 2 SWM Service Framework & Delivery System in Dar May 26, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert May 12, 2025
  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert May 12, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • Mtwale Atoa Mwongozo kwa Makatibu Tawala Wasaidizi wa Mikoa

    May 27, 2025
  • Nipo tayari kufanya kazi pamoja nanyi kufikia malengo ya Mhe. Rais – Prof. Tumaini Nagu

    May 26, 2025
  • TARURA IMEKUWA NA MCHANGO MKUBWA KWA SERIKALI YA AWAMU YA SITA

    May 26, 2025
  • MAPEPELE AWANOA MAAFISA HABARI WA TAMISEMI, AWATAKA WAWE WAZALENDO 

    May 26, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.