Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

Uhaba wa Saruji wachelewesha ujenzi wa barabara za Mji wa Serikali

Imewekwa tar.: March 3rd, 2021

Na Atley Kuni, Dodoma.

 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mhe Selemani Jafo, ameagiza ifikapo Julai 30, 2021, mradi wa ujenzi wa barabara katika mji wa Serikali eneo la Mtumba uwe umekamilika. Agizo la Waziri Jafo linafuatia taarifa iliyosomwa leo jijini Dodoma na Mkurugenzi wa Barabara za Mijini na Vijijini kutoka TARURA Mhandisi Mohammed Mkwata kuwa ujenzi wa barabara hizo upo nyuma kwa asilimia 6 kutokana na kukosekana kwa saruji yenye mgandamizo mwepesi yenye ujazo wa 32.5N na badala yake saruji inayopatikana kwa wingi ni ile yenye mgandamizo wa juu aina ya 42.5N.

Mhandisi Mkwata ameeleza kuwa ujenzi ulitarajiwa kufikia asilimia 69 badala ya 63 za sasa kulingana na mpango kazi wa mkandarasi kutokana na uhaba wa saruji katika kipindi cha kuanzia Novemba 26 mwaka 2020 hadi mwishoni mwa februari 2021. 

“Katika kipindi hicho mkandarasi hakuweza kupata saruji aina zote za 32.5N na 42.5N kwa kadiri ya mahitaji halisi hali ambayo iliathiri kazi za ujenzi wa vivuko na ujenzi wa tabaka la kwanza la barabara ambalo nalo linahitaji saruji,” amesema.

 Kufuatia taarifa hiyo Waziri Jafo ameitaka TARURA kuhakikisha kuwa ujenzi wa barabara hizo za mji wa serikali kwa kiwango cha lami unakamilika Julai 30, mwaka huu na kuwa kama kikwazo ni kukosekana kwa saruji hiyo nyepesi basi waangalie uwezekano wa kutumia saruji yenye mgandamizo wa juu. 

“Sijaridhishwa na kasi hii maana ipo chini kwa asilimia sita kwa maana hiyo sihitaji mjadala wa aina yoyote nataka ifikapo Julai 30 mradi huu uwe umekamilika, haiwezekani uchelewe kwa kigezo cha kukosekana Saruji aina ya 32.5N hivyo angalieni namna ya kutafuta suluhisho ya hili,” amesema Jafo.

 Waziri Jafo amewataka Wakala wa barabara za mijini na vijijini TARURA waifanyie utafiti wa kimaabara saruji aina ya 42.5N ambayo kwa sasa inapatikana madukani ili kuona kama inafaa kutumika kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa barabara hizo katika mji wa serikali. 

Katika hatua nyingine, Waziri Jafo ametembelea mradi wa barabara ya kuingia Hospitali ya Uhuru iliyopo Halmashauri ya wilaya Chamwino inayotakiwa kukamilika ifikapo Machi 14, 2021, ambapo ameelezea kuridhishwa na kasi ya ujenzi wa barabara hiyo na kuahidi kuwa ifikapo Machi 15 atafika eneo hilo tena kuona ujenzi ulivyokamilika.

 Awali, akitoa taarifa za mradi, Meneja wa TARURA kutoka halmashauri ya wilaya ya Chamwino, Mhandisi Nelson Maganga alisema kuwa, maendeleo ya jumla ya utekelezaji wa mradi yamefikia asilimia 85. 

Waziri Jafo, amefanya ziara katika miradi hiyo miwili, ikiwa ni sehemu ya muendelezo wa ziara anazozifanya kukagua shughuli mbalimbali za maendeleo na kutolea maelekezo kwa watendaji wa serikali.

 


Matangazo

  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert (extension) 1 May 28, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert (extension) May 28, 2025
  • TOR - Msimbazi Watershed Management – Modelling May 26, 2025
  • Monitoring & Support, TOR - DMDP 2 SWM Service Framework & Delivery System in Dar May 26, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • RC CHALAMILA ATAKA MACHINGA KARIAKOO KUFUNGUA NJIA

    May 30, 2025
  • Wamiliki wa vituo vya kulelea watoto wadogo mchana watakiwa kuzingatia miongozo na kanuni zilizopo.

    May 29, 2025
  • Mhe. Katimba awapokea Wabunge wa Zambia waliokuja kujifunza kuhusu Usimamizi na Uendeshaji wa Mamlaka za Serikali za Mitaa Tanzania Bara

    May 28, 2025
  • Mtwale Atoa Mwongozo kwa Makatibu Tawala Wasaidizi wa Mikoa

    May 27, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.