Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

“Tuendelee kuliombea Taifa, Ndege yetu imeachiwa “Waziri Jafo.

Imewekwa tar.: September 4th, 2019

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo amewataka viongozi wa dini Nchini kote kuendelea kuliombea Taifa hasa wakati huu ambao miradi mikubwa ya maendeleo inatekelezwa.

Waziri Jafo ameyasema hayo wakati akifunga Mkutano wa 82 wa Chama cha Madaktari wa Kikristo Tanzania unaofanyika chini ya Taasisi ya Huduma ya Kijamii za Kikristo(CSSC) katika ukumbi wa St. Gasper Jijini Dodoma.

Waziri Jafo amesema “Serikali ya Awamu ya Tano inatekeleza miradi mikubwa ambayo haijawahi kutokea tangu Uhuru, kila unapopita unaona ujenzi wa miundombinu ya barabara inaendelea, halkadhalika ujenzi wa reli ya kisasa (SGR), huku mradi wa ufuaji umeme wa mto Rufiji unatekelezwa hatuna budi kuendelea kumuombea Rais wetu Dkt. John Joseph Pombe Magufuli azidi kuwa na afya njema na aweze kusimamia miradi hii hadi ukamilifu wake”

Tunashukuru Mungu leo hii Mahakamu Kuu ya Gauteng, Africa Kusini imetoa hukumu na kuamuru ndege yetu ya Air Tanzania iliyokuwa inashikiliwa nchini humo iachiwe na mlalamikaji alipe gharama za kesi hizi ni habari njema sana kwetu na haya ni matunda ya kufanya vitu kwa nia njema na dhamira ya dhati ya kuwainua watanzania tusiache kuomba kwa ajili ya Taifa hili aliongeza Jafo.

Wakati huo huo Waziri Jafo aliziagiza Halmashauri zenye Hospitali  Teule (DDH) kuhakikisha wanafanya vikao na Taasisi za kidini zenye makubaliano ya uendeshaji wa Hospital hizo.  

“Hizi tabia za Halmashauri kusema hawana hela za vikao sjui viburudisho zisikwamishe ufanyikaji wa vikao, kutaneni hata saa nane mchana mpaka kumi jioni cha msingi mjadiliane changamoto zinazokabili hospitali hizo na kuzitaftia njia ya kuzitatua kwa pamoja” alisema Jafo.

Kuna changamoto ndogondogo ambazo zinaweza kutatuliwa kwa mashauriano tu lakini unapoziacha kwa muda mrefu zinakuwa tatizo kubwa, mkiwa mnakutana ni vizuri katika uboreshaji wa huduma za Afya kwenye  Halmashauri husika aliongeza Jafo.

“Taasisi za Dini mnafanya kazi kubwa sana katika Sekta ya Afya na kwa muda mrefu mmekuwa mkimiliki Hospital takribani 105 na Serikali tulikuwa na Hospital 77 tu kabla hatujaanza ujenzi wa Hospital za Wilaya 67.

Mmekuwa msaada katika kuwafikia wananchi ambao Serikali ilikua bado haijajenga Hospital niwapongeze kwa  kuhakikisha huduma za Afya zinapatikana karibu na wananchi na kwa haraka hakika mmewasaidia watanzania wetu kupata huduma bora za Afya  na mmeboresha afya zao Alisema Jafo.

Halkadhalika Waziri Jafo aliweka wazi mpango wa Serikali kukamilisha mchakato wa  kuajiri Watumishi wa Afya takribani 400 ambao kwa kiasi flani wataenda kupunguza uhaba wa watumishi wa Afya katika Vituo vya kiutolea huduma za Afya.

“Ninafahamu fika tatizo la uhaba wa watumishi katika hospital nyingi Serikali tunalifahamu hilo na tumechukua hatua za makusudi za kutangaza ajira za Afya na sasa tunakamilisha mchakato wa ajira hizo na muda si mrefu mtaanza kuwapokea kwenye baadhi ya Hospital ambao wataongeza nguvu katika utoaji wa huduma za Afya Nchini” Alisema Jafo.

Akizungumza katika Kikao hicho Rais wa Chama cha Madaktari wa Kikristo Tanzania Dr. Bwire Chirangi alitaja changamoto zinazowakabili ni pamoja na kukosa vikao vya mashauriano, uhaba wa watumishi wa Afya pamoja na miundombinu duni ya kuzifikia huduma za Afya.

Aidha Dr. Chirangi alieleza kuwa Chama hiki kimeanza mwaka 1937 na kinawakutanisha pamoja wataalamu wote wa Afya wanaohudumu katika Hospital za Dini na wamekuwa wakikutana kila mwaka kujadili changamoto na mafanikio mbalimbali ya huduma za Afya zinazotolewa na Taasisi za Dini ya Kikristo.



Matangazo

  • TOR - Msimbazi Watershed Management – Modelling May 26, 2025
  • Monitoring & Support, TOR - DMDP 2 SWM Service Framework & Delivery System in Dar May 26, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert May 12, 2025
  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert May 12, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • Nipo tayari kufanya kazi pamoja nanyi kufikia malengo ya Mhe. Rais – Prof. Tumaini Nagu

    May 26, 2025
  • TARURA IMEKUWA NA MCHANGO MKUBWA KWA SERIKALI YA AWAMU YA SITA

    May 26, 2025
  • MAPEPELE AWANOA MAAFISA HABARI WA TAMISEMI, AWATAKA WAWE WAZALENDO 

    May 26, 2025
  • MAHUSIANO MAZURI  NI NGUZO MUHIMU KATIKA UTEKELEZAJI WA MAJUKUMU-MHE.SAGINI

    May 26, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.