Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

TAMISEMI Yategua Kitendawili ajira 6,000 za Rais Samia

Imewekwa tar.: April 23rd, 2021

Atley Kuni na Veronica Simba- TAMISEMI

KATIBU Mkuu Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Prof. Riziki Shemdoe, ametegua kitendawili kuhusu ajira elfu sita za watumishi wa kada ya walimu kama ilivyoamriwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, kwamba waajiriwe walimu ili kukabiliana na uhaba wa watumishi wa kada hiyo hasa kwakuzingatia waliostaafu na walioacha kazi kwa sababu mbalimbali.

Akizungumza leo Aprili 23, 2021 jijini Dodoma, wakati wa ziara yake ya kwanza katika Ofisi za Makao Makuu ya Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC), ambayo ni moja ya taasisi inayosimamiwa na Ofisi yake, Prof. Shemdoe amesema, utaratibu wa kuajiri utafuata Sheria, Taratibu na Kanuni, huku akionya wale wote walioanza kutumia matapeli kusaka ajira waache mchezo huo mara moja.

Prof. Shemdoe amesema tokea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan alipo ielekeza Ofisi hiyo kufanya mchakato wa kuajiri walimu 6,000 ili kufidia baadhi ya watumishi hao kwa sababu mbali mbali, kumezuka wimbi la matapeli na wengine kuwadanganya watu wanaoomba ajira kwamba watawasaidia kupata ajira hizo.

“Nimepata taarifa kutoka kwa wasamaria wema kuwa, wapo baadhi ya watu kwa nia ovu wamekuwa wakiwatapeli kwa kuwaomba fedha baadhi ya walimu wanaotaka kuomba ajira na kuwataka watoe pesa ili zifikishwe Wizarani kwa ajili ya kuwapatia ajira, nipende kusema wazi kwamba jambo hili halipo,” amesema Prof. Shemdoe.

Prof. Shemdoe ameongeza kwamba, vishoka wote watakaobainika kutekeleza utapeli huo watachukuliwa hatua za kisheria ikiwemo kufikishwa kwenye vymbo vya dola, huku akiwataka wale wote watakaokumbana na adha hiyo kutosita kutoa taarifa ili hatua stahiki ziweze kuchukuliwa.

Ikiwa ni ziara yake ya kwanza katika chombo hicho kinachoangalia nidhamu ya watumishi walimu, Katibu Mkuu, Shemdoe amewataka watumishi wa ofisi hiyo kutoa ushirikiano kwa Katibu Mtendaji aliyeteuliwa na Kuapishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hivi karibuni kushika wadhifa wa Ofisi hiyo.

Akitoa maelezo ya awali kabla ya kumkaribisha Katibu Mkuu, Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-TAMISEMI, anayeshughulikia Elimu, Gerald Mweli, alisema Tume hiyo inafanya kazi vizuri na imekuwa mstari wa mbele kuhakikisha mashauri ya kero mbali mbali za walimu zinasikilizwa na kutolewa maamuzi kwa wakati.

“Ndugu Katibu Mkuu, Tume hii pamoja na kuhudumia idadi ya watumishi walimu wanaofikia asilimia 51 ya watumishi wote wa umma bado wamekuwa mstari wa mbele kuhakikisha mashauri yanayofikishwa yanatatuliwa kwa wakati. Aidha miongoni mwa mambo ambayo tulikubaliana katika mwaka wa fedha 2020/21, wameweza kufikia malengo kwa asilimia 90, amesema Mweli.

Awali akimkaribisha kuongea na watumishi hao, Katibu Mtendaji wa TSC Bibi Paulina Nkwama, alisema wamefarijika sana kuona wamekuwa miongoni mwa taasisi za mwanzo kabisa za Wizara hiyo kutembelewa ili kujua utendaji wao.

“Ndugu Katibu Mkuu, sisi kwanza tumefarijika sana na ujio wako, ukiangalia una takriban ni majuma mawili toka, Mhe. Rais akuteue na kukuapisha kushika wadhifa wa Katibu Mkuu, TAMISEMI, lakini kwa kuthamini, mchango wa kada ya walimu, umeona ziara yako ya kwanza ujielekeze kwenye Ofisi ya Tume ambayo ndiyo yenye kushughulikia mambo mbalimbali ya walimu,” amesema Bibi Paulina.

Tume ya Utumishi wa Walimu ndiyo chombo kinachoratibu na kushughulikia masuala yote ya walimu, ikiwepo kero na malalamiko ya kada hiyo.


Matangazo

  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert (extension) 1 May 28, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert (extension) May 28, 2025
  • TOR - Msimbazi Watershed Management – Modelling May 26, 2025
  • Monitoring & Support, TOR - DMDP 2 SWM Service Framework & Delivery System in Dar May 26, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • RC CHALAMILA ATAKA MACHINGA KARIAKOO KUFUNGUA NJIA

    May 30, 2025
  • Wamiliki wa vituo vya kulelea watoto wadogo mchana watakiwa kuzingatia miongozo na kanuni zilizopo.

    May 29, 2025
  • Mhe. Katimba awapokea Wabunge wa Zambia waliokuja kujifunza kuhusu Usimamizi na Uendeshaji wa Mamlaka za Serikali za Mitaa Tanzania Bara

    May 28, 2025
  • Mtwale Atoa Mwongozo kwa Makatibu Tawala Wasaidizi wa Mikoa

    May 27, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.