Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

SERIKALI YATOA MAAGIZO MAZITO KWA MAAFISA USTAWI  WA JAMII WA MIKOA NA HALMASHAURI

Imewekwa tar.: October 4th, 2024

Na Angela Msimbira, OR-TAMISEMI

NAIBU Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-TAMISEMI (Miundombinu), Mhandisi Rogatus Mativila amewaagiza Maafisa Ustawi wa Jamii kuhakikisha  wanahamasisha uanzishwaji wa vituo vya kulelea Watoto Wadogo Mchana vya Kijamii katika vijiji/mtaa na kuwasilisha taarifa hii ifikapo Januari 30,2025 

Mhandisi Mativila ametoa maagizo hayo leo Oktoba 4,2024, Jijini Dodoma  alipomuakilisha Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Adolf Ndunguru wakati akifungua mafunzo ya Kitaifa ya Uratibu na Utekelezaji wa Programu Jumuishi ya Taifa ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto kwa Maafisa ustawi wa Jamii wa Mikoa na Halmashauri.

Amesema kuwa katika kipindi hiki ukuaji na ujifunzaji wa watoto unakwenda kwa haraka sana huku mazingira yanayowazunguka yakiwa na mchango mkubwa wa kuamua hatima ya maisha yao, kivyo uwekezaji wa mapema katika huduma bora na kwa wakati kunawezesha kukuza rasilimali watu yenye tija kwa familia, jamii na taifa.

Amesema pia wahakikishe wanasimamia kwa ukamilifu Programu hii katika maeneo yao na taarifa za utekelezaji wa kila kipengele cha programu hii kuwezesha serikali kupata mafanikio na changamoto za Malezi na Makuzi ya watoto wa taifa hili.

Mhandisi Mativila amewataka kuendelea kutoa elimu kwa jamii kwa njia mbalimbali kuhusu umuhimu wa kuwekeza kwenye malezi bora ya watoto.

Aidha, amewataka kuhakikisha wanawatambua na kuendelea kushirikiana na wadau wote wa MMMAM waliopo kwenye mikoa na halmashauri ili kuchangia utekelezaji wa programu hiyo.

“Pia hakikisheni vikao vya mapitio ya Programu vinavyowaleta wadau kwenye ngazi ya mkoa na halmashauri vinafanyika kama vilivyoelekezwa na Programu hii.”amesisitiza

“Napenda kutoa rai kwenu mkawe mabalozi wazuri wa kuhakikisha watoto wadogo wenye umri wa miaka 0-8 wanapatiwa huduma zote za Malezi Jumuishi ikiwemo, Afya bora, Malezi yenye Mwitikio, Lishe toshelevu, Ujifunzaji wa Awali, na Ulinzi na Usalama wa Mtoto.

Naye, Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Chirdren in Crossfire Tanzania Craig Ferla amesema Uwekezaji wenye tija kwa watoto walio chini ya miaka 0-8  nchini kutasaidia kuchagiza nguvukazi ya maendeleo katika vizazi vijavyo hivyo jamii haina budi kuhakikisha inatumia muda kuwekeza kwenye makuzi ya mtoto ili kupata taifa lenye tija.

Aidha, amewataka Maafisa Ustawi wa Jamii kuhakikisha wanatumia ujuzi, akili na maarifa waliyoyapata katika mafunzo hayo katika kuhakikisha wanatoa huduma bora kwa jamii ili kupata watoto wenye malezi, makuzi na maendeleo yatakayosaidia Jamii na Taifa kwa ujumla

Matangazo

  • TOR - Msimbazi Watershed Management – Modelling May 26, 2025
  • Monitoring & Support, TOR - DMDP 2 SWM Service Framework & Delivery System in Dar May 26, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert May 12, 2025
  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert May 12, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • Nipo tayari kufanya kazi pamoja nanyi kufikia malengo ya Mhe. Rais – Prof. Tumaini Nagu

    May 26, 2025
  • TARURA IMEKUWA NA MCHANGO MKUBWA KWA SERIKALI YA AWAMU YA SITA

    May 26, 2025
  • MAPEPELE AWANOA MAAFISA HABARI WA TAMISEMI, AWATAKA WAWE WAZALENDO 

    May 26, 2025
  • MAHUSIANO MAZURI  NI NGUZO MUHIMU KATIKA UTEKELEZAJI WA MAJUKUMU-MHE.SAGINI

    May 26, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.