• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Malalamiko |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
  • Kuhusu Sisi
    • Local Government History
    • Kuhusu Wizara
      • Directories
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi na Programu
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Speech
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Machapisho ya Halmashauri
  • Machapisho
    • Taarifa Mbalimbali
    • Taarifa za Mapato
    • Majarida
    • Fomu Mbali mbali
    • Presentations
  • Miongozo
    • Miongozo OR TAMISEMI
    • Miongozo ya mradi wa SEQUIP
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Michoro ya Ujenzi
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali

Serikali yataka uwazi kwenye matumizi ya Tsh. 12 bilioni za Mradi wa USAID Boresha Afya

Imewekwa tar.: October 18th, 2018

Na Mathew Kwembe, Dodoma

Naibu katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Dkt Zainab Chaula amewataka Wakurugenzi kutoka Halmashauri 44 zilizo kwenye mradi wa USAID Boresha Afya kanda ya Kaskazini na kati kuhakikisha kuwa fedha zote zinazosaidia jitihada za serikali katika kuboresha sekta ya afya zinaonekana katika mipango kazi ya halmashauri zao.

 Akizungumza kwenye hafla fupi ya kutiliana saini mikataba na matumizi ya fedha za mradi kwa mwaka wa fedha 2018/2019 kwa viongozi wa wilaya nane za mkoa wa Dodoma ambao walitia saini mikataba ya halmashauri zao, na kuwawakilisha wenzao kutoka wilaya nyingine 37, Dkt Chaula alisema kuwa kwa kufanya hivyo kutaondoa changamoto za kiutendaji na kuongeza uwazi na uwajibikaji katika usimamiaji wa fedha zinazotolewa na wadau wa maendeleo katika miradi ya afya kwenye wilaya hizo.

Aliongeza kuwa wadau wengi wa maendeleo wanapobuni miradi ya afya hawashirikishi ngazi mbalimbali za serikali na hivyo wadau hawa kushindwa kuvielewa na kutekeleza vipaumbele vya serikali.

Hata hivyo Dkt Chaula aliusifu mradi wa USAID Boresha Afya kanda ya kati na Kaskazini kwa kuwa wazi na kuweka fedha za mradi katika halmashauri husika.

Mapema Mkurugenzi Mkazi wa Shirika lisilo la Kiserikali la Elizabeth Glaser linalopambana na na VVU/UKIMWI kwa watoto bwana Nelson Ojanji amemweleza Naibu Katibu Mkuu kuwa katika kipindi cha mwaka 2018/19 zaidi ya shilingi bilioni 12 zitatolewa kwa halmashauri 44 zinazotekeleza afua za Kifua Kikuu na Uzazi wa mpango.

“Bajeti za halmashauri washirika wa USAID Boresha Afya zote ziko tayari na viongozi wake watatia saini wakiwa katika halmashauri zao,” alisema Bwana Ojanji

Aidha katika kipindi cha mwaka 2017/2018, bwana Ojanji alisema kuwa zaidi ya shilingi bilioni 11 zilitolewa na Mradi huo kwa halmashauri 44 nchini ambako mradi huo unafanya kazi.

Alisema fedha hizo huwekwa kwenye mipango kazi ya idara za afya za halmashauri hivyo kuzipa halmashauri uwezo wa kupanga na kusimamia matumizi ya fedha na utekelezaji wa kazi za mradi.

Pamoja na kutoa fedhakwa halmashauri USAID Boresha Afya imetoa vifaa tiba mbalimbali vyenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 3 katika halmashauri zote 44 zinazotekeleza mradi.

Halmashauri zinazotekeleza mradi wa USAID Boresha Afya kanda ya kati na kaskazini ni za kutoka mikoa ya Arusha, Dodoma, Kilimanjaro, Manyara, Singida na Tabora.

Matangazo

  • ORODHA YA WAKUU WA KITENGO CHA FEDHA YENYE MABADILIKO 5-5-2022 May 06, 2022
  • Kazi za muda za makarani na wasimamizi wa Sensa 2022 May 05, 2022
  • MUDA WA NYONGEZA MAOMBI YA AJIRA ZA TAMISEMI 2022 May 04, 2022
  • Taarifa ya Kitengo Manunuzi na Ugavi, April 2022 April 04, 2022
  • Safeguard Documents for TACTIC Project March 30, 2022
  • Miongozo ya Operesheni Anwani za Makazi March 24, 2022
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • BARABARA YA MVUMI KUWEKWA LAMI KM 3

    May 26, 2022
  • PROF. SHEMDOE AZINYOOSHEA KIDOLE HALMASHAURI 8 KWA KUTOKUTENGE FEDHA ZA LISHE

    May 25, 2022
  • WAZIRI MKUU MAJALIWA ASIMAMISHA KAZI MKURUGENZI WA JIJI, MAAFISA WATANO ARUSHA

    May 24, 2022
  • WAKUU WA MIKOA SIMAMIENI UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO KWENYE HALMASHAURI

    May 24, 2022
  • Angalia zote

Video

Taarifa ya Ukusanyaji wa Mapato ya Halmashauri, kipindi cha robo ya pili ya mwaka wa fedha 2021/22
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi ( LIVE)
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Tume ya Ajira Tanzania
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.