Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

SERIKALI YASISITIZA UBORA NA USIMAMIZI WA MIRADI YA SERIKALI ZA MITAA.

Imewekwa tar.: December 16th, 2024

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais -TAMISEMI Dkt. Festo John Dugange amesema Serikali imetekeleza miradi mbalimbali ya kuwanufaisha wananchi ikiwemo ujenzi wa zahanati ,vituo vya Afya, hospitali,shule, barabara na huduma za maji mijini na vijiji kufuatia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kutoa fedha nyingi kwenye bajeti za Mamlaka za Serikali za Mitaa kote nchini. 

Dkt. Dugange amesema hayo wakati akifungua kongamano la wadau wa Serikali za mitaa kutoka maeneo mbalimbali nchini leo Desemba 16, 2024 Jijini Dodoma ambapo amesema Serikali imejenga zahanati zaidi ya 1900, vituo vya afya 872 huku asilimia 99 ya Halmashauri zote nchini zikiwa na hospitali.

“Kazi ya serikali za mitaa ni kuharakisha maendeleo yanawafikia wananchi. Serikali tutaendelea kuimàrisha ufanisi katika utoaji wa huduma kwa wananchi, tumefanya uwekezaji mkubwa na kuwekeza rasilimali nyingi katika miradi mbalimbali inayotekelezwa na Serikali za Mitaa ikiwemo ujenzi wa madarasa, maabara, mabweni ya wanafunzi na barabara” amesisitiza Dkt. Dugange.

Amesema viongozi wa serikali za mitaa wanalo jukumu la kuwezesha ustawi wa wananchi na kuhakikisha usimamizi mzuri wa rasilimali zinazoelekezwa kwenye maeneo ya Serikali za Mitaa huku akibainisha kuwa kongamano hilo linatoa fursa kwa wadau wa Serikali za mitaa kujadili namna ambavyo Serikali itaendelea kuimarisha na kuboresha ufanisi na utendaji kazi ili kufikia malengo ya kitafa. 

Dkt. Dugange amesema viongozi wa serikali za mitaa wana kazi kubwa ya kuibua na kusimamia vyanzo vya mapato katika maeneo yao ili wananchi waone faida na matunda ya uwepo wa Serikali za mitaa kupitia miradi mbalimbali ya maendeleo inayoanzishwa.

“Tunapaswa kukusanya mapato ya ndani kwa ufanisi, kudhibiti matumizi na kupunguza utegemezi wa Halmashauri zetu kwa Serikali kuu, matarajio ya Serikali ni kuona miradi iliyopangwa hususani ujenzi wa majengo ya Serikali ya kutolea huduma yanakamilika kwa wakati na ubora kwa kuzingatia fedha zilizotengwa.

Kwa upande wake Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya UONGOZI (Uongozi Institute), Kadari Singo amesema taasisi ya uongozi imekutana na wadau hao ili kutoa mafunzo yenye lengo la kuimarisha utoaji wa huduma katika maeneo ya Serikali za Mitaa.

Amesema taasisi ya uongozi itaendelea kuimarisha uelewa na kutoa fursa kwa viongozi wa serikali na wadau mbalimbali kupatiwa mafunzo ili kuongeza ufanisi na utoaji wa huduma kwa wananchi.

Matangazo

  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert (extension) 1 May 28, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert (extension) May 28, 2025
  • TOR - Msimbazi Watershed Management – Modelling May 26, 2025
  • Monitoring & Support, TOR - DMDP 2 SWM Service Framework & Delivery System in Dar May 26, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • RC CHALAMILA ATAKA MACHINGA KARIAKOO KUFUNGUA NJIA

    May 30, 2025
  • Wamiliki wa vituo vya kulelea watoto wadogo mchana watakiwa kuzingatia miongozo na kanuni zilizopo.

    May 29, 2025
  • Mhe. Katimba awapokea Wabunge wa Zambia waliokuja kujifunza kuhusu Usimamizi na Uendeshaji wa Mamlaka za Serikali za Mitaa Tanzania Bara

    May 28, 2025
  • Mtwale Atoa Mwongozo kwa Makatibu Tawala Wasaidizi wa Mikoa

    May 27, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.