Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

Serikali yagawa vifaa vya bilioni 3 kwa Wanafunzi 18,488 wenye mahitaji maalum

Imewekwa tar.: January 14th, 2021

Na Atley Kuni, Dodoma

Serikali imetoa vifaa na visaidizi maalum vya aina mbalimbali vyenye thamani ya Shilingi bilioni 3 kwa ajili ya wanafunzi 18,488, ambao wana mahitaji maalum wa shule za msingi na sekondari nchini ili kuwawezesha wanafunzi hao kumudu masomo katika shule zao.

Akizindua zoezi la usambazaji wa vifaa hivyo leo mjini Dodoma, Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Mhe. Selemani Jafo, amesema, Ofisi ya Rais - TAMISEMI kupitia Programu ya EP4R imeweza kununua jumla ya vifaa na visaidizi maalum 51,339 vya aina mbalimbali kwa ajili ya wanafunzi wenye mahitaji maalum wa shule za msingi na sekondari.

Amesema kuwa Vifaa hivi vilivyonunuliwa vimegharimu jumla ya Shilingi 2,833,374,280 na vitasambazwa kwa wanafunzi wenye mahitaji maalum ambao wamegawanyika kwenye makundi maalum yapatayo manane.

Waziri Jafo ameyataja makundi hayo ya wanafunzi wenye mahitaji maalum kuwa ni Viziwi, Wasioona, Albino, Wenye Uoni Hafifu, Wenye Ulemavu wa Viungo, Wenye Ulemavu wa Akili, Wenye Usonji na Wenye Uziwi na kutokuona.

Amesema shabaha ya Serikali ni kuhakikisha watoto wote wa kitanzania wanapata elimu iliyokusudiwa ikiwa ni mpango wa utekelezaji wa sera ya Elimu ya mwaka 2014.

“Ofisi ya Rais TAMISEMI imeweka mkazo katika kukabiliana na vikwazo dhidi ya uwepo ushiriki na ujifunzaji kwa wanafunzi wenye mahitaji maalum. Mojawapo ya hatua ambayo imechukua ni kununua vifaa maalum vya kielimu na visaidizi kwa ajili ya wanafunzi wenye mahitaji maalum,” amesema.

Akizungumza katika hafla hiyo, Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Mhandisi Joseph Nyamhanga, amesema, katika kipindi cha miaka mitano, 2016/2020 cha Serikali ya awamu ya Tano chini ya Mhe. John Pombe Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, imefanya mambo mengi katika utoaji wa elimu kwa wanafunzi wenye mahitaji maalum ikiwemo kuongezeka kwa shule zinazo wahudumia wanafunzi wa Elimu ya Awali, zilizoongezeka kwa asilimia 46.1, msingi asilimia 23.9 na Sekondari 24.6.

“Mheshimiwa Waziri mbali na hayo, ongezeko la Watoto wenye mahitaji maalum walioandikishwa ni asilimia 46.1 kwa elimu ya awali, asilimia 34.0 kwa elimu ya msingi na asilimia 74.6 ni kwa sekondari,” alisema Nyamhanga.

Katibu Mkuu ameongeza kuwa, wanafunzi wenye Ulemavu wanaohitimu Elimu ya Msingi na kujiunga na Sekondari imeongezeka kutoka asilimia 69.9 mwaka 2016 hadi asilimia 76.3 mwaka 2020.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Msaidizi kutoka Ofisi ya Rais-TAMISEMI, anayeshughulikia Elimu maalum, Julius Migeha, alisema hivi sasa Serikali inaendelea na la kuwabaini watoto wenye mahitaji maalum ili waweze kuandikishwa na kupatiwa elimu, hivyo akawataka wazazi wenye watoto wa aina hiyo kutoa ushirikiano kwa timu ili dhamira ya serikali iweze kutimia.

Katika mwaka wa fedha 2017/18, serikali ilifanikiwa kuendesha utaratibu wa kuwabaini watoto wenye mahitaji maalum, ambapo jumla ya  watoto 16,436 waliweza kufikiwa na kwa mwaka huu lengo la serikali ni kuwafikia Watoto 18,000.

Ofisi ya Rais TAMISEMI inajukumu la kuratibu na kusimamia utekelezaji wa utoaji wa elimu bora kwa wanafunzi wa Elimu ya Awali, Shule za Msingi na Shule za Sekondari, hii ni pamoja na kuhakikisha mahitaji muhimu ya kujifunzia na kufundishia yanapatikana kwa lengo la kupata idadi kubwa ya Watanzania walioelimika na wanaopenda kujielimisha zaidi ili waweze kuchangia katika kufikia malengo ya maendeleo ya Taifa letu bila kujali tofauti zao.

Matangazo

  • TOR - Msimbazi Watershed Management – Modelling May 26, 2025
  • Monitoring & Support, TOR - DMDP 2 SWM Service Framework & Delivery System in Dar May 26, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert May 12, 2025
  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert May 12, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • Nipo tayari kufanya kazi pamoja nanyi kufikia malengo ya Mhe. Rais – Prof. Tumaini Nagu

    May 26, 2025
  • TARURA IMEKUWA NA MCHANGO MKUBWA KWA SERIKALI YA AWAMU YA SITA

    May 26, 2025
  • MAPEPELE AWANOA MAAFISA HABARI WA TAMISEMI, AWATAKA WAWE WAZALENDO 

    May 26, 2025
  • MAHUSIANO MAZURI  NI NGUZO MUHIMU KATIKA UTEKELEZAJI WA MAJUKUMU-MHE.SAGINI

    May 26, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.