Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

Serikali yagawa Pikipiki 2894 kwa Waratibu Elimu Kata nchini

Imewekwa tar.: July 4th, 2018

Serikali imezindua zoezi la usambazaji wa pikipiki 2,894 kwa Waratibu Elimu kata nchini kwa kutoa wito kwa Maafisa Elimu wa Wilaya kuhakikisha kuwa pikipiki hizo zinawafikia walengwa hao.

Akizungumza mara baada ya kukabidhiwa funguo za pikipiki hizo na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako, kwa niaba ya Waziri Mkuu Mhe.Kassim Majaliwa, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Seleman Jafo, amewataka Maafisa wa Elimu kuhakikisha kuwa pikipiki hizo aina ya Honda zitumiwe na Waratibu Elimu kata.

Alisema kuwa serikali ya Awamu ya tano chini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt John Pombe Magufuli imelipa uzito suala la utoaji wa elimu bora nchini ndiyo maana serikali imeamua kuanzisha mpango wa kutoa elimu bila malipo.

“Ni matumaini yangu baada ya serikali kukubali kutoa pikipiki hizi suala la usimamizi wa elimu katika kata zenu litaenda kufanyika vizuri bila visingizio vyovyote,” alisema.

Mhe.Jafo alisisitiza kuwa  serikali inaenda kuwapatia waratibu wa elimu kata pikipiki hizo na kamwe pikipiki hizo zisitumiwe kwa ajili ya shughuli nyingine zozote mbali na ufuatiliaji na usimamizi wa shule katika kata husika.

“Napenda kulisisitiza jambo hili, pikipiki hizi siyo za kuendea kwenye viti virefu, na pia zisitumike kufanyia shughuli ya bodaboda,” alisema Mhe.Jafo.

Aidha aliwataka Maafisa Elimu Wilaya kuhakikisha kuwa pikipiki hizo aina ya Honda ndiyo zitakazogawiwa kwa waratibu elimu kata na si vinginevyo.

“Sitaki kusikia kuwa waratibu wa elimu kata wamegawiwa pikipiki za aina nyingine badala ya aina hii ya Honda tunazozigawa leo,” alisema.

Alisema serikali inalenga kupandisha ubora wa elimu katika ngazi ya kata, hivyo amewaagiza wakurugenzi wa halmashauri kuhakikisha kuwa pikipiki hizo zinapatiwa huduma ya mafuta bure katika kipindi cha miezi sita.

Naye Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako alisema kuwa pikipiki hizo zilinunuliwa na Wizara yake kupitia programu ya Lanes ambapo serikali imehakikisha kuwa pikipiki hizo ina vifaa vyote vya usalama barabarani.

Alisema kuwa ni matarajio yake kuwa pikipiki hizo zitawawezesha waratibu elimu kata kuboresha ubora wa elimu katika kata kwa kufanya ufuatiliaji wa mara kwa mara katika shule zao.

Alisema kuwa hatarajii kuona wanafunzi wengi wanaendelea kupata daraja la sifuri, na kamwe shule zisiwe vituo vya kulea watoto badala yake kata ziimarishe usimamizi wa elimu.

Mapema Mwakilishi wa wadau wa Maendeleo Bibi Susan Steven alisema kuwa wao kama wadau wa maendeleo  wamefurahishwa na hatua ya serikali kushirikiana nao katika kuleta maendeleo ya elimu Tanzania.

Anaandika  Mathew Kwembe  OR TAMISEMI

Matangazo

  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert (extension) 1 May 28, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert (extension) May 28, 2025
  • TOR - Msimbazi Watershed Management – Modelling May 26, 2025
  • Monitoring & Support, TOR - DMDP 2 SWM Service Framework & Delivery System in Dar May 26, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • RC CHALAMILA ATAKA MACHINGA KARIAKOO KUFUNGUA NJIA

    May 30, 2025
  • Wamiliki wa vituo vya kulelea watoto wadogo mchana watakiwa kuzingatia miongozo na kanuni zilizopo.

    May 29, 2025
  • Mhe. Katimba awapokea Wabunge wa Zambia waliokuja kujifunza kuhusu Usimamizi na Uendeshaji wa Mamlaka za Serikali za Mitaa Tanzania Bara

    May 28, 2025
  • Mtwale Atoa Mwongozo kwa Makatibu Tawala Wasaidizi wa Mikoa

    May 27, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.