Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

Serikali Kuendelea Kuimarisha Ukusanyaji wa Mapato ya halmashauri

Imewekwa tar.: February 26th, 2019

Mamlaka za Serikali za Mitaa nchini zimetakiwa kuhakikisha kuwa fedha zote zinazokusanywa katika mapato zinawekwa benki kabla ya kupangiwa matumizi husika ili kuwa salama zaidi na kuhakikisha zinakwenda kutekeleza matumizi husika.

Hayo yamebainishwa na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI), Mhandisi Joseph Nyamhanga katika hafla ya upokeaji wa mashine za kielektroniki (point of sales machines) kutoka Serikali ya Dernmark ofisini kwake Jijini Dodoma leo.

“Makatibu Tawala wa Mikoa kuweni makini katika ukusanyaji wa mapato ili kutimiza azma ya serikali ya kuongeza udhibiti na kuleta tija katika ukusanyaji wa mapato katika Mamlaka za Serikali za Mitaa kwa kuhakikisha fedha ilokusanywa inahifadhiwa benki kabla ya matumizi yoyote”Amesema Mhandisi Nyamhanga.

Aidha, Mhandisi Nyamhanga ameongeza kuwa jitihada hizi zinazofanywa na Serikali ya Awamu ya Tano zitasaidia kuongeza kipato katika Mamlaka za Serikali za Mitaa, kupunguza mianya ya izi wa fedha, kupunguza utegemezi na kuboresha utoaji wa huduma za kijamii kwa wananchi.

Naye Mkurugenzi wa Serikali za Mitaa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Dkt.Charles Muhina amesema kuwa hafla hiyo ya kukabidhi mashine hizo kwa mikoa hiyo ni mwendelezo wa kuziwezesha Halmashauri kuwafikia walipa kodi waliopo kwenye maeneo yao na kuongeza wigo katika ukusanyaji wa mapato katika maeneo yao.

“Sisi OR-TAMISEMI jukumu letu ni kufanya ufuatiliaji na tathimini ya utekelezaji wa mradi ili kuhakikisha kuwa mradi husika unatekelezwa kwa kuzingatia sheria, kanuni, na taratibu za nchi hii” Ameongezea Dkt. Muhina

Kwa upande wake Mkurugenzi wa TEHAMA Ofisi ya Rais TAMISEMI Erick Kitali ametoa wito kwa halmashauri kuwa na kifaa maalumu cha kuzuia radi ili kutatua changamoto ya mitandao ya mifumo ya mapato kaharibiwa radi kipindi cha mvua katika halmashauri hizo.

Awali Kiongozi wa Mradi Maboresho ya Mazingira ya Biashara Flemming Olsen ametoa wito kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano waTanzania kuhakikisha  mapato yanakusanywa kwa ufasaha kwani kuna wafanya biashara wanabidhaa ya thamani kubwa  lakini wanalipa ushuru mdogo.

Wakati huo huo Katibu Tawala wa Mkoa wa Kigoma Rashid Mchatta amesema kuwa atakwenda kusimamia vyema mashine hizo ili zifanye kazi ipasavyo na itasaidia kuongeza mapato katika maeneo yao ya kazi.

Katika hafla hiyo Mhandisi Nyamhanga amehitimisha kwa kutoa shukurni za dhati  kwa niaba ya Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kwa wananchi wa Serikali ya Denmark kupitia Ubalozi wa Denmark nchini Tanzania na kusema kuwa ushirikiano wa nchi hizi mbili utaleta maendeleo kwa wananchi wa Tanzania kwa ujumla.

                                                          Anaandika Fred Kibano na Majid Abdulkarimu

Matangazo

  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert (extension) 1 May 28, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert (extension) May 28, 2025
  • TOR - Msimbazi Watershed Management – Modelling May 26, 2025
  • Monitoring & Support, TOR - DMDP 2 SWM Service Framework & Delivery System in Dar May 26, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • RC CHALAMILA ATAKA MACHINGA KARIAKOO KUFUNGUA NJIA

    May 30, 2025
  • Wamiliki wa vituo vya kulelea watoto wadogo mchana watakiwa kuzingatia miongozo na kanuni zilizopo.

    May 29, 2025
  • Mhe. Katimba awapokea Wabunge wa Zambia waliokuja kujifunza kuhusu Usimamizi na Uendeshaji wa Mamlaka za Serikali za Mitaa Tanzania Bara

    May 28, 2025
  • Mtwale Atoa Mwongozo kwa Makatibu Tawala Wasaidizi wa Mikoa

    May 27, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.