Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

MTWALE ASISITIZA UBUNIFU KATIKA KUANDAA NA KUTEKELEZA MIPANGO NA MIKAKATI YA KUKUZA UCHUMI NA UZALISHAJI

Imewekwa tar.: January 27th, 2025

Na. James Mwanamyoto, OR-TAMISEMI

Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-TAMISEMI Bw. Sospeter Mtwale amewataka Makatibu Tawala Wasaidizi wa Mikoa wa Sehemu ya Uchumi na Uzalishaji kuwa wabunifu katika kuandaa na kutekeleza mikakati na mipango ya kukuza uchumi inayolenga kutatua changamoto za uchumi na uzalishaji katika mikoa na halmashauri wanazozisimamia. 

Bw. Mtwale wito huo leo katika Ukumbi wa Ofisi ya Rais-TAMISEMI jijini Dodoma, wakati akifungua kikao kazi cha Makatibu Tawala Wasaidizi wa Mikoa wa Sehemu ya Uchumi na Uzalishaji kilicholenga kujadili utekelezaji wa Mipango ya Bajeti ya Mwaka wa Fedha 2024/2025 pamoja na kuandaa mipango ya Mwaka wa Fedha 2025/2026.

“Sehemu za uchumi na uzalishaji katika mikoa ndio zinabeba dira ya ukuaji wa uchumi na maendeleo endelevu katika nchi yetu hivyo ni muhimu mipango yenu ilenge vipaumbele vya Serikali kwa kuzingatia uendelezaji wa uchumi mahalia,” Bw. Mtwale amesisitiza.

Bw. Mtwale amehimiza kuwa, katika kipindi hiki ambacho Serikali inaendelea na maandalizi ya Mipango na Bajeti ya mwaka wa fedha 2025/2026 ni vema mipango na bajeti za mikoa na halmashauri zikazingatia mwongozo wa bajeti na vipaumbele vya nchi ili kuakisi utatuzi wa matatizo ya kiuchumi yanayowakabili wananchi na taifa kwa ujumla.

Sanjari na hilo, amewakumbusha Makatibu Tawala hao Wasaidizi wa Mikoa kuwa, wanajukumu muhimu katika maendeleo ya taifa hivyo waendelee kutekeleza majukumu yako kwa weledi na uzito unaostahili ili kuongeza ufanisi wa utekelezaji wa majukumu yao hususani katika kutatua changamoto za uchumi na uzalishaji kwenye mikoa na halmashauri wanazozisimamia. 

Kwa upande wake, mwakilishi wa makatibu tawala hao wasaidizi Bw. Said Maditto ambaye ni Katibu Tawala Msaidizi wa Mkoa wa Mbeya amesema kuwa kitendo cha kufanya kikao kazi na wakurugenzi wa wizara za kisekta ni fursa ya kujenga ushirikiano wa kiutendaji katika kutekeleza mikakati na mipango ya kukuza uchumi nchini. 

Aidha, Bw. Maditto amemuahidi Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-TAMISEMI Bw. Sospeter Mtwale kuwa watatekeleza kwa vitendo maelekezo yote aliyoyatoa pamoja na kutekeleza maazimio wakakayotokanayo katika kikao kazi hicho kwa lengo la kuandaa mikakati na mipango endelevu itakayokuza uchumi wa taifa.

Naye, Mkurugenzi wa Tawala za Mikoa Ofisi ya Rais-TAMISEMI Bi. Beatrice Kimoleta amesema TAMISEMI iliona ni muhimu kukutana na Makatibu Tawala Wasaidizi wa Mikoa wa Sehemu ya Uchumi na Uzalishaji pamoja na wakurugenzi wa Wizara za Kisekta kwa ajili ya kupata maoni, maono na mtazamo wa namna bora ya kuandaa na kutekeleza mikakati na mipango ya kukuza uchumi nchini.

Pia, Bi. Kimoleta ameongeza kuwa kikao kazi hicho kitatoa fursa ya kupitia utekelezaji wa bajeti ya mwaka wa fedha 2024/2025 ili kuona nini kimetekelezwa mpaka hivi sasa na ni changamoto zipi zifanyiwe kazi ili zisikwamishe utekelezaji wa bajeti hiyo.

Kikao kazi hicho cha siku mbili kimeudhuriwa na Makatibu Tawala Wasaidizi wa Mikoa wa Sehemu ya Uchumi na Uzalishaji kutoka mikoa 26, Wakurugenzi na Wakurugenzi Wasaidizi kutoka Wizara za Kisekta pamoja na Wakurugenzi na Wataalam kutoka Ofisi ya Rais-TAMISEMI.

Matangazo

  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert (extension) 1 May 28, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert (extension) May 28, 2025
  • TOR - Msimbazi Watershed Management – Modelling May 26, 2025
  • Monitoring & Support, TOR - DMDP 2 SWM Service Framework & Delivery System in Dar May 26, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • RC CHALAMILA ATAKA MACHINGA KARIAKOO KUFUNGUA NJIA

    May 30, 2025
  • Wamiliki wa vituo vya kulelea watoto wadogo mchana watakiwa kuzingatia miongozo na kanuni zilizopo.

    May 29, 2025
  • Mhe. Katimba awapokea Wabunge wa Zambia waliokuja kujifunza kuhusu Usimamizi na Uendeshaji wa Mamlaka za Serikali za Mitaa Tanzania Bara

    May 28, 2025
  • Mtwale Atoa Mwongozo kwa Makatibu Tawala Wasaidizi wa Mikoa

    May 27, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.