Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

Mhandisi Nyamhanga ataka Halmashauri zijibu na kufanyia kazi mapendekezo ya CAG

Imewekwa tar.: March 26th, 2019

Na Mathew Kwembe, Dodoma

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhandisi Joseph Nyamhanga amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri kuhakikisha kuwa hoja zote zilizoibuliwa kwenye taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) zinajibiwa na kufanyiwa kazi mapendekezo ya wakaguzi kwa kuanzia na wakaguzi wa ndani.

Akizungumza kwenye kikao kazi cha upokeaji na uhakiki wa taarifa za majibu na mipango kazi ya utekelezaji wa hoja na mapendekezo ya CAG kwa hesabu za Mamlaka za Serikali za Mitaa za mwaka 2017/18 leo katika Chuo cha Serikali za Mitaa Hombolo jijini Dodoma, Mhandisi Nyamhanga amesema kuwa ni muhimu hoja zote zikafanyiwa kazi haraka na kwa ufasaha ili kunusuru upotevu wa fedha, kuboresha utendaji na kuimarisha utawala bora, jambo ambalo ndio msingi wa ukaguzi.

Amesema kuwa ni vema kila Mtumishi afanye kazi kwa kuzingatia sheria, Kanuni, Miongozo, Taratibu na kuwajibika bila kuoneana haya.

“Tukifanya hivyo, hoja zisizo za lazima zitaondoka na hata wakaguzi hawatatumia muda mwingi katika kufuatilia mambo ya msingi zaidi katika kuboresha utendaji,” amesema.

Kauli ya Katibu Mkuu Nyamhanga inafuatia kukamilika kwa zoezi la kujibu hoja za CAG lililofanywa na Wakurugenzi wa Halmashauri, Waweka hazina na Wakaguzi wa Ndani kutoka Halmashauri zote 185, zoezi lililoanza tarehe 19 na kukamilika tarehe 26 machi, 2019.

Mhandisi Nyamhanga ameongeza kuwa katika kujibu hoja za CAG na kuandaa mpango kazi wa utekelezaji wa maagizo ya CAG ya Hesabu za mwaka 2016/17 imeonekana kuwa kufikia mwezi januari 2019, jumla ya hoja asilimia arobaini na saba (47%) zilifungwa wakati asilimia 53% zilikuwa bado hazijajibiwa.

Katibu Mkuu amesema kuwa zoezi hilo liliendelea katika ukaguzi wa Hesabu za Mwaka 2017/2018 ambapo hali halisi ya utekelezaji wa maagizo ya CAG zitaonekana baada ya taarifa hiyo kuwasilishwa bungeni mwaka 2019.

Aidha Katibu Mkuu amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri kuhakikisha kuwa hoja na mapendekezo ya taarifa ya CAG wanayafanyia kazi ili kuboresha utendaji wa kazi na kuimarisha uwajibikaji hali ambayo itawahakikishia wananchi na umma kwa ujumla matumizi mazuri ya fedha zao, na utendaji wenye ufanisi katika Mamlaka za Serikali za Mitaa.

“Kwa kufanya hivyo tutakuwa tunatekeleza maagizo ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuhusu kufanyia kazi maagizo ya CAG na kuchukua hatua stahiki kwa Watumishi,” amesema Mhandisi Nyamhanga na kuongeza:

“Ninaelekeza kuwa, Watendaji wakaendelee kufanyia kazi hoja na mapendekezo ya CAG na kuwasilisha kwa wakaguzi wa CAG.”

Katibu Mkuu amewaambia wakurugenzi wa Halmashauri kuhakikisha kuwa mara tu baada ya taarifa ya CAG kuwasilishwa bungeno majibu na vielelezo viwasilishwe kwa wakaguzi wa CAG ndani ya siku 21 kwa mujibu wa sheria ambapo amesema kuwa hategemei kuona majibu ya awali yasiyojitosheleza ilihali watendaji hao walikutana jijini Dodoma kwa ajili ya kuyaboresha majibu hayo.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Kitengo cha Ukaguzi na Ufuatiliaji wa fedha za Mamlaka za Serikali za Mitaa Bi Miriam Mmbaga amesema kuwa kikao hicho kimefanyika kuanzia tarehe 19-26 Machi, 2019 ambapo kimewahusisha Wakurugenzi, Waweka Hazina na Wakaguzi wa Ndani kutoka Mikoa 26 na Halmashauri zote 185 nchini.

Amesema lengo la kikao hicho lilikuwa ni kuwawezesha Watendaji hao kujibu hoja za CAG, kuongeza uwajibikaji katika utendaji wao wa kazi ili hoja hizo zisijitokeze tena katika halmashauri zao.

Naye Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza Kiomoni Kibamba akiongea kwa niaba ya Wakurugenzi wa Halmashauri amesema kuwa halmashauri zimekuwa zikikabiliana na changamoto mbalimbali katika kujibu hoja za ukaguzi kwani hoja nyingine hasa zile za kisera zilipaswa kujibiwa na Wizara husika badala ya ilivyo sasa kujibiwa na halmashauri.

Pia amewaasa wakurugenzi wenzake wa halmashauri kuwapa ushirikiano wakaguzi wa ndani wa halmashauri zao pindi wanapohitaji magari kwa ajili ya kwenda kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa katika halmashauri zao.

Matangazo

  • TOR - Msimbazi Watershed Management – Modelling May 26, 2025
  • Monitoring & Support, TOR - DMDP 2 SWM Service Framework & Delivery System in Dar May 26, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert May 12, 2025
  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert May 12, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • Mtwale Atoa Mwongozo kwa Makatibu Tawala Wasaidizi wa Mikoa

    May 27, 2025
  • Nipo tayari kufanya kazi pamoja nanyi kufikia malengo ya Mhe. Rais – Prof. Tumaini Nagu

    May 26, 2025
  • TARURA IMEKUWA NA MCHANGO MKUBWA KWA SERIKALI YA AWAMU YA SITA

    May 26, 2025
  • MAPEPELE AWANOA MAAFISA HABARI WA TAMISEMI, AWATAKA WAWE WAZALENDO 

    May 26, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.