Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

MAREKANI KUTOA FEDHA ZAIDI KUPAMBANA NA UKIMWI

Imewekwa tar.: June 12th, 2023

OR-TAMISEMI

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Angellah Kairuki amesema Serikali ya Marekani kupitia Mpango wa Dharura wa Rais wa Marekani wa Kupambana na Ukimwi (PEPFAR) imetenga dola za Marekani milioni 450 kwa ajili ya kutekeleza afua mbalimbali za afya ikiwamo kupambana na UKIMWI.

Pia amesema Serikali itaendelea kushirikiana na Marekani katika kutekeleza afua za kupambana na UKIMWI, Kifua kikuu na Malaria.

Kairuki ameyasema hayo  jijini hapa wakati wa ziara ya timu ya viongozi kutoka mpango wa dharura wa kupambana na UKIMWI (PEPFAR), Programu ya UNAIDS na Global fund.

Alisema pia PEPFAR imeahidi kutenga dola za Marekani milioni 450 kwa mwaka 2023 ambazo zitatumika kati ya Oktoba 2023 hadi Septemba 2024 kwa ajili ya afya ikiwemo, kupambana na UKIMWI, kuimarisha mifumo ya afya na uzazi wa mpango.

“Ofisi ya Rais-TAMISEMI inathamani ziara hii ambayo inasaidia kuimarisha ushirikiana kati ya Serikali ya Tanzanua na Serikali ya Marekani kupitia PEPFAR.”

Alisema Serikali inatekeleza afua mbalimbali za afya katika maeneo ya msingi ya VVU/UKIMWI, Kifua kikuu, Afya ya Uzazi, Mama na Mtoto; Uzazi wa Mpango, lishe, Malaria, Magonjwa ya Kitropiki yasiyopew kipaumbele na kuimarisha mifumo ya afya. 

Kairuki alisema ikiwa PEPFAR inaadhimisha miaka 20 tangu kuanza ufadhili wake hapa nchini mwaka 2003, Serikali ya Marekani imekuwa mstari wa mbele katika mapambano dhidi ya UKIMWI ambapo takribani dola za Marekani bilioni 6.6 zimewekezwa kwenye afua ambalimbali za afya.

Alisema Tanzania, kuna vituo vya afya vya umma na binafsi vilivyosajiliwa 8,796 na kati ya hivyo 6,893 vinatoa huduma kamili za VVU chini ya msaada wa PEPFAR na asilimia 90 ya vituo hivyo vinatoa hduma ya afyamsingi.

Kairuki alisema wakati PEPFAR inaanza kusaidia Tanzania mwaka 2004, watu 500 wanaoishi na VVU ndio waliokuwa wanapata huduma kamili za VVU katika vituo vya afya na kwa sasa watu milioni 1.6 wanapata matibabu ya bure ya dawa za kurefusha maisha.

Alisema juhudi hizo zimesaidia kupunguza vifo vitokanavyo na UKIMWI kwa asilimia 76 wakati maambukizi mapya yakipungua kwa asilimia 58.

“Tunashukuru kwa msaada wa PEPFAR katika kusaidia katikakuimarisha mfumo wa afya, kuziba pengo la rasilimali watu kwa ajili ya afya, kuimarisha uwezo wa maabara, kuimarisha mifumo ya taarifa za afya, na kushiriki katika ufuatiliaji wa magonjwa, utafiti na tathmini ya afua za afya.

“Pia tunatambua msaada wa PEPFAR katika kupanua huduma za uzazi wa mpango, na mapambano dhidi ya magonjwa ya milipuko.”

Kwa upande wa Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu alisema Tanzania haijafanya vizuri kwenye lengo la kujua hali ya maambukizi ambayo kwa sasa ni asilimia 86 chini ya lengo la kidunia la asilimia 95 na kuwa hilo linachangiwa na mwitikio mdogo wa wanaume kutopima afya zao.

Alisema ili kuendelea kufanya vizuri, Wizara ya afya imeweka mikaka ya kuhakikisha idadi ya wananchi wanaojua hali zao inaongezeka na kuzuia maambukizi mapya ya VVU kwa wasichana balehe ambao ndio waathdirika wakubwa.

“Pia tunakwenda kupambana na suala la maambukizi ya VVU kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto ambalo bado kama nchi hatujafanya vizuri.”

Mratibu wa PEPFAR na Mwakilishi Maalum wa serikali ya Marekani katika masuala ya Diplomasi ya Afya, Balozi Dk.John Nkengasong aliipongeza Serikali kwa kusimamia utekelezaji wa afua za afya amabo imetokana na uongozi shupavu wa Rais Samia Suluhu Hassan.

Naye Mwakilishi Maalumu wa Global Heath Diplomacy na Makamu Mkurugenzi Mtendaji wa masuala ya program wa UNAIDS, Angeli Achrekar alisema wamefurahishwa na kuona jinsi Tanzania imefanya kisichowekezaka katika kusimamia afua za afya

Matangazo

  • TOR - Msimbazi Watershed Management – Modelling May 26, 2025
  • Monitoring & Support, TOR - DMDP 2 SWM Service Framework & Delivery System in Dar May 26, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert May 12, 2025
  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert May 12, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • Mtwale Atoa Mwongozo kwa Makatibu Tawala Wasaidizi wa Mikoa

    May 27, 2025
  • Nipo tayari kufanya kazi pamoja nanyi kufikia malengo ya Mhe. Rais – Prof. Tumaini Nagu

    May 26, 2025
  • TARURA IMEKUWA NA MCHANGO MKUBWA KWA SERIKALI YA AWAMU YA SITA

    May 26, 2025
  • MAPEPELE AWANOA MAAFISA HABARI WA TAMISEMI, AWATAKA WAWE WAZALENDO 

    May 26, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.