• Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Machapisho
    • Taarifa za Mapato
    • Majarida
    • Fomu Mbali mbali
    • Presentations
  • Miongozo
    • Miongozo OR TAMISEMI
    • Miongozo ya mradi wa SEQUIP
    • Green and Smart Cities
    • Miongozo ya Kilimo
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Michoro ya Ujenzi
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)

Mabingwa watetezi Mtwara wawasha indiketa kutetea taji lao

Imewekwa tar.: June 25th, 2021

Na Mathew Kwembe, Mtwara

Kama kuna timu ya wasichana ya mpira wa wavu inayoshiriki mashindano ya UMISSETA mwaka huu hapa Mtwara inadhani inaweza kuchukua kombe hilo mwaka huu basi iwaulize timu ya mkoa wa Tabora.

Katika mchezo huo uliochezwa leo asubuhi timu ya Mtwara ikiongozwa na kocha wao Gabriel Joshua iliweza kuisambaratishaTabora baada ya kuilaza kwa seti 3-0.

Jambo la kushangaza katika mchezo wa leo ni pale timu ya wasichana ya Tabora iliposhindwa kupata hata pointi moja katika seti ya pili kwa kukubali kupoteza pointi 25 kwa 0.

Kocha wa Tabora Mwalimu Masingija Muyanga kutoka sekondari ya Mwanzugi anakiri kuwa vijana wake walizidiwa kabisa katika mchezo wa leo licha ya timu yake kushinda michezo yake mitatu ya awali.

“Wenyeji Mtwara wamenizidi kwani wanacheza kwenye uwanja wao wa nyumbani lakini wachezaji wao pia wamekaa muda mrefu na wamekuwa exposed (uzoefu wa kucheza) katika mashindano makubwa,” alisema.

Kauli hiyo iliungwa mkono na nahodha wa timu ya wasichana ya Tabora Flora Frank ambaye  anacheza kama ‘seta’ alisema kuwa wachezaji wake walijawa na hofu kutokana na wachezaji wenzao wa Mtwara kuwa na majina makubwa na kushiriki mashindano makubwa kama FEASSA.

Akizungumzia matokeo mazuri ya timu yake kocha wa timu ya wasichana ya Mtwara Gabriel Joshua alisema timu yake imejiandaa vizuri kulitetea kombe hilo na hakuna timu inayoweza kulichukua kombe hilo.

Amesema timu yake ambayo inaundwa na wanafunzi kutoka shule ya sekondari ya Mkalapa ambayo ipo kilometa 35 kutoka mji wa Masasi inafanya mazoezi kila siku kwa ajili ya kujiandaa na mashindano mbalimbali.

Joshua ambaye ni mtumishi wa halmashauri ya mji wa Masasi kama Mkuu wa Idara ya Ardhi na Maliasili katika halmashauri hiyo amesema timu yake inaundwa na wasichana ambao alianza kuwafundisha tangu wakiwa wadogo yaani darasa la nne.

“Baadhi ya wachezaji unaowaona hapa nilianza kuwafundisha volleyball tangu wakiwa darasa la nne na leo nipo nao katika mashindano haya ya UMISSETA na ndoto yangu ni kuwa na timu kali ya Volleyball ambayo haijapata kutokea nchini,” amesema.

Joshua ambaye pia hufundisha timu ya UMITASHUMTA ya wasichana ya mkoa wa Mtwara amesema mkoa wa Mtwara wamekuwa mabingwa wa UMITASHUMTA tangu waliposhiriki mashindano hayo mwaka 2013 huko Kibaha Pwani na amekuwa bingwa wa UMISSETA tangu mwaka 2019.

Amesema siri kubwa ya mafanikio ya timu yake ni mazoezi ya kila siku na kucheza michezo mbalimbali ya ligi kubwa ikiwemo kushiriki ligi ya muungano na mashindano mengine nchini.

Joshua ambaye anasaidiwa na walimu wawili mmoja kutoka shule ya msingi na mwingine sekondari ya Mkalapa anatamani kuiona timu anayoifundisha ikishiriki mashindano ya kimataifa kama Olimpiki na kurudi na medali ya dhahabu.

Kwa upande wao wanafunzi Proscovia Condrad mwenye miaka 15 ambaye anasoma kidato cha pili na mwenzake Lafia Hassan Matandika ambaye yupo kidato cha nne wanasifu uwezo wa Kocha Joshua kwani ameweza kuwafanya wapende mchezo huo na kufanya vizuri darasani katika masomo yao.

“Dada zetu ambao walisoma Mkalapa wamechukuliwa na timu ya JKT, nasi tunatamani kufika huko au zaidi,” amesema Lafia (Kulwa) ambaye pacha wake Lazia (Doto) pia anachezea timu hiyo.

Katika michezo mingine ya Volleyball iliyochezwa leo asubuhi Singida imeifunga Kigoma seti 3-0, Mara ikaifunga Songwe seti 3-0, na Dar es salaam ikaifunga Tanga seti 3-0

Kwa upande wa volleyball wavulana Manyara imeifunga Simiyu seti 3-0, Dar es salaam imeifunga Arusha seti 3-1, Dodoma imefungwa na Tabora seti 0-3, Kigoma imefunga Mbeya seti 3-1, Unguja imeifunga Mara seti 3-0 na Pwani imefungwa na Mwanza seti 0-3.

Katika soka wasichana Iringa na Arusha sare 1-1, Simiyu imeifunga Katavi 1-0, Lindi na Kilimanjaro sare 1-1, Morogoro na Ruvuma sare 1-1, Geita wasichana 3 Dar es salaam 1, Mwanza imewafunga wenyeji Mtwara magoli 3-0 na Rukwa na Lindi wametoka sare 2-2.

Michezo mingine Tabora imeifunga Kagera 2-0, Mara na Kilimanjaro wametoka sare 1-1, Iringa na Arusha sare 1-1, na Manyara imeifunga Dodoma 3-0.

Matokeo ya mchezo wa Netiboli Kagera 23 Manyara 19, Njombe 7 Mara 33, Shinyanga 22 Dar es salaam 29, Tabora 38 Dodoma 19, Rukwa 31 Lindi 15, Arusha 26 Kigoma 27.

Katika mpira wa kikapu wasichana Lindi dhidi ya Arusha magoli 7-73, Kilimanjaro dhidi ya Dodoma 51-23, na Mwana dhidi ya Songwe 47-16.

Matokeo ya mpira wa kikapu kwa wavulana Songwe dhidi ya Kagera 6-27, Dar es salaam dhidi ya Mwanza 28-18, Simiyu dhidi ya Morogoro 20-72 na Unguja dhidi ya Tabora 43-15.

Matangazo

  • Orodha ya waliopata vibali vya Uhamisho Septemba - Disemba 2022 (OR - TAMISEMI) January 21, 2023
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kidato cha Kwanza Waliorudia Mtihani January 15, 2023
  • Matumizi ya Lugha ya Kiswahili na Kingereza January 14, 2023
  • Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Kwanza 2023 December 14, 2022
  • Orodha ya Waliopangwa kwenye Vituo vya Kazi Kada za Afya (Awamu ya Pili) Agosti 2022 August 30, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA KWA KADA ZA AFYA (Marudio) July 20, 2022
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • LAAC YAPOKEA TAARIFA KUHUSU UTAWALA NA UENDESHAJI WA MAMLAKA ZA SERIKALI ZA MITAA

    March 14, 2023
  • SERIKALI YAWEKA MIKAKATI KATIKA USIMAMIZI WA MIRADI YA MENDELEO, UKUSANYAJI NA UDHIBITI WA MAPATO KATIKA HALMASHAURI

    March 13, 2023
  • WAUGUZI NA WAKUNGA WATAKIWA KUSIMAMIA MAADILI YA KAZI

    March 13, 2023
  • ACHENI KUTUMIANA NYARAKA ZA SERIKALI KWENYE MITANDAO YA KIJAMII NA BARUA PEPE BINAFSI - DKT. MPANGO

    March 13, 2023
  • Angalia zote

Video

Taarifa ya Ukusanyaji wa Mapato ya Halmashauri, kipindi cha robo ya pili ya mwaka wa fedha 2021/22
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.