Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

MAAFISA VIUNGO WA MIKOA WAAGIZWA KUTOA TAKWIMU NA TAARIFA SAHIHI ZA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM

Imewekwa tar.: June 4th, 2024

Katibu Tawala Mkoa wa Singida Dkt. Fatma Mganga amefungua mafunzo ya kuwajengea uwezo Maafisa Viungo wa Mikoa na kuwataka kuandaa takwimu zenye uhalisia na taarifa wanazoziandaa kwa wakati. 

Dkt. Fatma Mganga ameyasema hayo leo tarehe 4 juni, 2024 katika ukumbi wa VETA Manispaa ya Singida mkoani Singida wakati akifungua mafunzo ya kupitia mpango kazi wa utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2020 ili kuandaa mpango kazi wa mwaka 2024. 

Dkt. Mganga amesema baadhi ya takwimu zinazoandaliwa na Maafisa hao hazina uhalisia na hali hiyo hujitokeza katika miradi ambayo haitegemewi kuwa na idadi kubwa kuzidi maelfu mfano idadi ya madaraja yaliyojengwa na barabara za lami zinazojengwa.

“takwimu zote zinazoingizwa kwenye mipango kazi na taarifa za utekelezaji wa ilani ni muhimu zikahakikiwa kupitia vikao na Wakuu wa Idara husika kuridhia takwimu hizo ili kuwa na uhalisia” alisema Dkt. Mganga.

 Aidha, amewaasa Maafisa hao kuhakikisha hakuna utofauti wa malengo yaliyopangwa na taarifa za utekelezaji wa ilani ya CCM lakini pia kuacha kuchelewesha mipango kazi na taarifa za utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi ili kuendana na kalenda ya uwasilishaji wa taarifa katika vikao vya Chama cha Mapinduzi. 

Awali akitoa neno la utangulizi kabla ya mgeni rasmi Bw. Johnson Nyingi Mkurugenzi Msaidizi Sehemu ya Uratibu wa Shughuli za Serikali Ofisi ya Rais TAMISEMI amesema mafunzo hayo yanahudhuriwa na Maafisa Viungo wa mikoa 26 na baadhi ya Halmashauri za mkoa wa Dar es Salaam ili kuweza kutatua changamoto ya uandaaji wa taarifa ya Ilani ya CCM kwani kazi nyingi zinafanyika serikalini lakini hazitolewi taarifa.

Naye Bw. Omar Ilyas Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Sera na Uratibu wa Shughuli za Serikali Ofisi ya Waziri Mkuu alisema jukumu la Maafisa hao sio kufuatilia taarifa za utekelezaji bali ni uratibu na ufuatiliaji wa Ilani ya uchaguzi lakini pia uratibu wa shughuli nyingine za Serikali.

Akitoa neno la shukrani Susana Ndunguru Mwenyekiti wa Maafisa Viungo Tanzania Bara ambaye pia ni Afisa Kiungo Mkoa wa Mwanza aliishukuru Serikali na kuahidi kuzifanyia kazi taarifa kwa usahihi na kuzitoa kwa wakati. 


Mafunzo hayo ya siku nne yana lengo la kuwajengea uwezo Maafisa Viungo wa mikoa kupitia mpango kazi wa utekelezaji wa Ilani ya chama cha mapinduzi ya mwaka 2020 ili kuandaa mpango kazi wa mwaka 2024 yakihusisha Maafisa Viungo wa Mikoa 26, Wataalam kutoka Ofisi ya Rais TAMISEMI na Wataalam kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu.



Matangazo

  • TOR - Msimbazi Watershed Management – Modelling May 26, 2025
  • Monitoring & Support, TOR - DMDP 2 SWM Service Framework & Delivery System in Dar May 26, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert May 12, 2025
  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert May 12, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • Mtwale Atoa Mwongozo kwa Makatibu Tawala Wasaidizi wa Mikoa

    May 27, 2025
  • Nipo tayari kufanya kazi pamoja nanyi kufikia malengo ya Mhe. Rais – Prof. Tumaini Nagu

    May 26, 2025
  • TARURA IMEKUWA NA MCHANGO MKUBWA KWA SERIKALI YA AWAMU YA SITA

    May 26, 2025
  • MAPEPELE AWANOA MAAFISA HABARI WA TAMISEMI, AWATAKA WAWE WAZALENDO 

    May 26, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.