• Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Machapisho
    • Taarifa za Mapato
    • Majarida
    • Fomu Mbali mbali
    • Presentations
  • Miongozo
    • Miongozo OR TAMISEMI
    • Miongozo ya mradi wa SEQUIP
    • Green and Smart Cities
    • Miongozo ya Kilimo
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Michoro ya Ujenzi
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)

KAIRUKI ATOA MAAGIZO SABA KWA WAGANGA WAKUU WA MIKOA NA HALMASHAURI

Imewekwa tar.: February 22nd, 2023

Na. Angela Msimbira OR- TAMISEMI


WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Angellah Kairuki ametoa maagizo saba kwa waganga wakuu wa mikoa na Halmashauri ikiwemo kuwataka kufanya ukaguzi wa vifaa vya afya ili kudhibiti upotevu na matumizi mabaya ya bidhaa hizo.

Aidha, amewaagiza wakurugenzi wa Halmashauri, waganga wakuu na wafawidhi wa vituo vya afya kuhakikisha fedha za Mfuko wa Afya wa pamoja zinatumika kwa wakati na kuzingatia mipango iliyoidhinishwa na hatakuwa na mzaha na watakaokiuka hilo.

Waziri Kairuki alitoa maagizo hayo leo Februari 22, 2023 jijini Dodoma wakati akifunga mkutano mkuu wa mwaka wa waganga wakuu wa mikoa na Halmashauri ambao uliambatana na uzinduzi wa mwongozo wa utekelezaji wa mshitiri kwenye ununuzi   wa dawa,vitendanishi vifaa na vifaa tiba ili kudhibiti ununuzi holela wa bidhaa hizo.

Waziri  Kairuki amesema kutofanyika kwa ukaguzi wa bidhaa za afya ikiwemo dawa, vitendanishi vifaa na vifaa tiba katika vituo vya kutolea huduma za afya kunaweza kuchangia upotevu na matumizi mabaya ya bidhaa hizo.

“Nichukue nafasi hii kuwaelekeza Waganga Wakuu wa Mikoa na Halmashauri kuwa kafanyeni ukaguzi wa vifaa vya afya kwa ushirikiano kati ya Idara ya Afya na Wakuu wa Idara nyingine ikiwa ni pamoja na wakaguzi wa ndani.

Pia kuanzia sasa ukaguzi wa bidhaa za afya itakuwa ni moja ya kiashiria cha ufanisi kwa Waganga Wakuu wa Mikoa na Halmashauri,”alisisitiza Waziri Kairuki.

Amefafanua  kuwa hilo litaenda sambamba na kuhakikusha kuwa vifaa tiba, mashine za maabara na X-ray zilizosambazwa katika vituo vya kutolea huduma za afya, Wahandisi wa vifaa tiba ngazi ya Halmashauri na watumiaji wa vifaa wanajengewa uwezo ili waweze kumudu kuvitumia na kuvifanyia ukarabati au matengenezo Kinga.

Waziri Kairuki amesema kilio cha kuchelewa kwa fedha za mfuko wa afya wa pamoja kimesikika na kwamba kutakuwepo utaratibu wa kutolewa mwanzoni mwa robo mwaka kama ilivyopendekezwa kupitia mkutano huo.

Hata hivyo, kumekuwepo na tatizo la baadhi ya Halmashauri hasa ngazi ya vituo kutotumia fedha za Mfuko wa Afya wa Pamoja hali inayopelekea kuwa na bakaa kubwa, nitumie nafasi hii kuwataka Wakurugenzi wa Halmashauri, Waganga Wakuu Mikoa na Halmashauri, Waganga Wafawidhi wa Vituo kuhakikisha fedha hizi zinatumika kwa wakati na kuzingatia Mipango ilioidhishwa

Ameongeza Kwa wale watakaoshindwa kufanya hivyo, tutazihamisha na kuzipeleka kwa wale wenye kuzihitaji zaidi,”.

Mbali hayo amewaagiza wahakikishe  kuwa vituo vyote vilivyokamilika vinaanza kutoa huduma na baadhi ambazo vituo vinakamilika lakini juhudi za kuanza kutoa huduma hazifanyiki na vituo vinafikia hatua ya kuchakaa kabla ya kuanza huduma.

Alieleza katika mwaka wa fedha 2021/ 2022 jumla ya miradi ya miundombinu ya Afya 1,445 ilikuwa inatekelezwa, ikijumuisha miradi ya Zahanati 786, Vituo vya Afya 471 na Hospitali 154.

Aidha, uchambuzi wa utekelezaji wa miradi hiyo unaonesha jumla ya miradi 208 sawa na asilimia 14 ipo katika hatua ya Chini ya lenta, miradi 106 sawa na asilimia 8 ipo katika hatua ya upauaji na miradi 845 sawa na asilimia 58 ipo katika hatua ya umaliziaji.

Amewaelekeza wa Waganga Wakuu wote wa Mikoa na Halmashauri kwenda kusimamia miradi hyoi ikamilike na kuanza kutoa huduma zilizokusudiwa kwa  wananchi.

Pia, ameagiza kuwa miradi ambayo ipo katika hatua ya upauaji iwe imekamilika ifikapo Februari 28 mwaka huu na miradi iliyo chini ya lenta iwe imekamilika ifikapo Machi 31 mwaka huu

Matangazo

  • Orodha ya waliopata vibali vya Uhamisho Septemba - Disemba 2022 (OR - TAMISEMI) January 21, 2023
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kidato cha Kwanza Waliorudia Mtihani January 15, 2023
  • Matumizi ya Lugha ya Kiswahili na Kingereza January 14, 2023
  • Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Kwanza 2023 December 14, 2022
  • Orodha ya Waliopangwa kwenye Vituo vya Kazi Kada za Afya (Awamu ya Pili) Agosti 2022 August 30, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA KWA KADA ZA AFYA (Marudio) July 20, 2022
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • LAAC YAPOKEA TAARIFA KUHUSU UTAWALA NA UENDESHAJI WA MAMLAKA ZA SERIKALI ZA MITAA

    March 14, 2023
  • SERIKALI YAWEKA MIKAKATI KATIKA USIMAMIZI WA MIRADI YA MENDELEO, UKUSANYAJI NA UDHIBITI WA MAPATO KATIKA HALMASHAURI

    March 13, 2023
  • WAUGUZI NA WAKUNGA WATAKIWA KUSIMAMIA MAADILI YA KAZI

    March 13, 2023
  • ACHENI KUTUMIANA NYARAKA ZA SERIKALI KWENYE MITANDAO YA KIJAMII NA BARUA PEPE BINAFSI - DKT. MPANGO

    March 13, 2023
  • Angalia zote

Video

Taarifa ya Ukusanyaji wa Mapato ya Halmashauri, kipindi cha robo ya pili ya mwaka wa fedha 2021/22
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.