Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

Jafo akemea mlundikano wa taka kwenye dampo la Dodoma

Imewekwa tar.: January 17th, 2020

Waziri wa Nchi, OR-TAMISEMI Mhe. Selemani Jafo amekemea hali ya mlundikano wa takataka kwenye madampo ya kisasa yaliyojengwa kwenye baadhi ya Majiji na Manispaa nchini kupitia mradi wa mpango miji ya kimkakati (Tscp).

Waziri Jafo amekemea hali hiyo wakati alipotembelea dampo la Chidaya lilipo Jijini Dodoma na kukuta mlundikano wa taka ambayo zimesababisha hali ya uchafu, inzi na harufu katika eneo hilo la kuhifadhia taka.

“Madampo haya yamejengwa kwa gharama kubwa sana na yana lengo la kuimarisha usafi kwenye miji yetu na kuchataka taka hizo kwa utaalamu wa kisasa kabisa usioleta athari zozote za kimazingira huku yakihakikisha usafi wa eneo la dampo unazingatiwa” alisema Jafo.

Aliongeza kuwa naona mitambo ya kuchakata taka hizi imeegeshwa tu na haifanyi kazi na takataka zimelundikana hapa na taarifa mnazonipa haziniridhishi, sioni sababu yeyote ya msingi inayopelekea uongozi wa dampo hili ushindwe kushindilia hizi taka kila zinapoletwa.

Jafo aliagiza uongozi wa Jiji la Dodoma kuongeza usimamizi katika Dampo hilo ili kazi iweze kufanyika kama inavyotakiwa ili kukamarisha usafi wa Jiji la Dodoma ambapo ndipo Makao Makuu ya Nchi.

Pia Waziri Jafo ametoa wiki mbili kwa uongozi wa Jiji la Dodoma kukamilisha matengenezo ya mitambo yote ambayo inahitilafu ili iweze kuwa sawa na kutumika katika kuchakata na kusindika taka katika Dampo la Chidaya.


“Wakati natembelea madampo mengine nilikuta Manispaa ya Kigoma  mitambo imeegeshwa tu bila kufanya kazi inayotakiwa na niliwaambia kuwa mitambo ile nitaihamishia Dodoma kwenye Dampo hili  lakini kwa hali hii siwezi kuleta ile mitambo rekebisheni hii yenu haraka ili kazi za hapa ziendelee kama inavyotakiwa alisisitiza Waziri Jafo.

Akitoa ufafanuzi katika ziara hiyo Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma Godwin Kunambi kuwa kwenye bajeti ya mwaka 2019/20 imetengwa bajeti ya shilingi mil 600 kwa ajili ya uendeshaji wa mitambo na dampo la Chidaya hivyo hakuna upungufu katika fedha za uendeshaji na usimamizi ila changamoto hii iliyotokea ya ubovu uliotokea wa mitambo hii haujakwamishwa na uhaba wa fedha ila ni upatikanaji wa vipuli vya mitambo hiyo.

Naye Kaimu Mkuu wa Idara ya mazingira Ally Mfinanga alisema mitambo hiyo iliharibika mwishoni mwa mwezi Novemba, 2019 na mvua zinazoendelea kunyesha zimesababisha magari ya taka kumwaga taka mwanzoni hapo bila kusambazwa kwa sababu gari la kusambaza haliwezi kufika eneo la taka kutokana na mvua hizi.

Aliongeza kuwa mitambo miwili iliyoharibika tumeshaanza mchakato wa kutengeneza magari hayo na yatatengemaa baada ya muda mfupi na kazi ya kuchakata na kusindikika taka hapa Dampo itaendelea vizuri na kwa ufanisi kama ilivyokuwa kama awali.

Dampo hili la kisasa limejengwa kupitia mradi wa mpango miji mkakati na madampo yenye hadhi hii yamejengwa katika Miji ya Tanga, Arusha, Mbeya, Mwanza, Kigoma pamoja na hapa Dodoma.

Mwisho.


Matangazo

  • TOR - Msimbazi Watershed Management – Modelling May 26, 2025
  • Monitoring & Support, TOR - DMDP 2 SWM Service Framework & Delivery System in Dar May 26, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert May 12, 2025
  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert May 12, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • Nipo tayari kufanya kazi pamoja nanyi kufikia malengo ya Mhe. Rais – Prof. Tumaini Nagu

    May 26, 2025
  • TARURA IMEKUWA NA MCHANGO MKUBWA KWA SERIKALI YA AWAMU YA SITA

    May 26, 2025
  • MAPEPELE AWANOA MAAFISA HABARI WA TAMISEMI, AWATAKA WAWE WAZALENDO 

    May 26, 2025
  • MAHUSIANO MAZURI  NI NGUZO MUHIMU KATIKA UTEKELEZAJI WA MAJUKUMU-MHE.SAGINI

    May 26, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.