Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

HUDUMA ZA KIJAMII KUSOGEZWA KWENYE MAKAZI YA WAATHIRIKA WA MAPOROMOKO YA TOPE HANANG - Mhe. Majaliwa

Imewekwa tar.: December 21st, 2024

Na. James K. Mwanamyoto OR-TAMISEMI

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa amesema Serikali itajenga shule, zahanati, sekondari na kituo cha afya ili kusogeza huduma za kijamii kwenye makazi mapya ya waathirika wa maporomoko ya tope Hanang mkoani Manyara.

Mhe. Kassim Majaliwa amesema hayo akiwa Wilayani Hanang, wakati akikabidhi nyumba 109 kwa waathirika wa maporomoko ya tope wilayani humo, ambazo zimejengwa na Serikali kwa kushirikiana na Shirika la Msalaba Mwekundu kwenye Kitogoji cha Waret kijiji cha Gidagamowd.

“Tunataka wananchi hawa wawe na mwingiliano na wengine,waendelee kuishi hapa na wapate huduma muhimu za kijamii na ndio maana tutajenga shule, zahanati, sekondari na kituo cha afya,” Mhe. Majaliwa amesisitiza.

Aidha, Mhe. Majaliwa amefafanua kuwa, kati ya nyumba hizo 109 alizozikabidhi kwa waathirika wa maporomoko ya tope, nyumba 73 zimegharamiwa na Serikali, nyumba 35 zimegharamiwa na Shirika la Msalaba Mwekundu Tanzania na nyumba moja imegharamiwa na Umoja wa Wanawake wa Tanzania (UWT).

Mhe. Majaliwa ameongeza kuwa, nyumba zote hizo zimejengwa kwa uratibu mzuri wa timu ya wataalam kutoka Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Ofisi ya Waziri Mkuu, Wizara ya Fedha, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Hanang pamoja na Halmashauri ya Wilaya ya Hanang.

Sanjali na hilo, Mhe. Majaliwa ameipongeza na kuishukuru TARURA kwa ujenzi mzuri wa barabara kwenye eneo hilo ambalo zimejengwa nyumba 109 za waathirika wa maporomoko ya tope na kuongeza kuwa toka amefika na kuanza ukaguzi wa nyumba hajaona barabara iliyoteleza licha uwepo wa mvua iliyokuwa ikinyesha.

“Mhe. Waziri wa TAMISEMI na TARURA yako mmefanya kazi nzuri sana ya ujenzi wa barabara kwenye nyumba hizi 109, hivyo jukumu mlilobakia nalo ni kutuwekea lami hivyo jaribu kuangalia kwenye vifungu vyako vya bajeti ili barabara ziwekwe lami,” Mhe. Majaliwa ameeleza.

Maporomoko ya tope wilayani Hanang yaliyotokea Desemba 7, 2023 katika mji mdogo wa Katesh pamoja na vijiji jirani yalipelekea baadhi ya wakazi wa maeneo hayo kupoteza nyumba za kuishi, hivyo Serikali ilichukua hatua ya kukabiliana na changamoto hiyo na hatimaye Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa amekabidhi nyumba 109 kwa waathirika wa maporomoko hayo.

Matangazo

  • TOR - Msimbazi Watershed Management – Modelling May 26, 2025
  • Monitoring & Support, TOR - DMDP 2 SWM Service Framework & Delivery System in Dar May 26, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert May 12, 2025
  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert May 12, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • Mtwale Atoa Mwongozo kwa Makatibu Tawala Wasaidizi wa Mikoa

    May 27, 2025
  • Nipo tayari kufanya kazi pamoja nanyi kufikia malengo ya Mhe. Rais – Prof. Tumaini Nagu

    May 26, 2025
  • TARURA IMEKUWA NA MCHANGO MKUBWA KWA SERIKALI YA AWAMU YA SITA

    May 26, 2025
  • MAPEPELE AWANOA MAAFISA HABARI WA TAMISEMI, AWATAKA WAWE WAZALENDO 

    May 26, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.