Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

Dkt. Dugange, Awataka Watumishi Afya Wajitafakari wenyewe

Imewekwa tar.: December 11th, 2020

Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, (TAMISEMI) Mhe. Festo Dugange, anayeshughulikia Afya amewataka wataalam wa Afya katika ngazi za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa kujitafakari na kubadilika ili kuendana na kasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli. Aidha kwa yeyote atakayeshindwa kufanya hivyo ni vema akawa tayari kupisha watu wenye uwezo.

Akizungumza kwenye kikao maalumu cha kujitambulisha mbele ya Watumishi wa Idara ya Afya na Ustawi wa Jamii, ndani ya Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Dkt. Dugange, alisema, kutokana na mikakati iliyopo na mipango ya kusukuma sekta ya afya, nilazima kila mmoja ajitathimini kwa nafasi yake na majukumu aliyo nayo kama kweli anaitendea haki nafasi aliyo kabidhiwa.

Akiainisha vipaumbele muhimu Dkt. Dugange alisema, kubwa watakalo anza nalo ni uboresha wa upatikanaji wa dawa, vifaa tiba na vitendanishi; uboreshaji wa mapato ametaja kama kipaumbele namba mbili huku akihimiza matumizi ya Mfumo wa GoTHOMIS, alisema suala la ukarabati mdogo mdogo kwenye vituo pamoja na maslahi na marupurupu ya watumishi yatategemea sana suala la uboreshaji wa mapato katika vyanzo vyote muhimu na hasa wakizingatia matumizi ya Mfumo.

“Katika ajenda hii ya mapato waganga wakuu wa Halmashauri wahakikishe baada ya tathmini ya ufatiliaji, yaonekane mabadiliko kwa macho ikiwepo vituo kupunguza utegemezi, ili kuweza kujifanyia baadhi ya mambo wao wenyewe”, alisema Dkt. Dugange na kuongeza kuwa, mbali ya boreshaji wa mapato vilevile ni lazima uboreshaji wa miundombinu iwe ni suala endelevu.

“Ni lazima pia tuboreshe miundombinu yetu na kuhakikisha ile asilimia ishirini ya ongezeko inayotajwa katika Ilani ya Chama Cha Mapinduzi ya 2020 hadi 2025, tunaifanyia kazi mapema kuanzia sasa kwa bajeti tulizo zipanga lakini pia kwakuwatumia wadau wetu wa maendeleo tunaoshirikiana nao, bila kusahau uhamasishaji wa jamii kuanza shughuli za ujenzi kama mpango wa jamii unavyo elekeza”. Alisema Naibu Waziri huyo.

Awali kabla ya kuzungumza na watumishi hao, Mkurugenzi wa Tiba na Ustawi wa Jamii, Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Dkt. Ntuli Kapologwe, alimpongeza na kisha kutoa taarifa fupi ya utendaji kazi mbele ya Naibu Waziri huyo, ambapo pamoja na mambo mengine, Dkt. Ntuli alimuelezea Naibu Waziri juu ya ujenzi wa miundombinu ya afya katika ngazi mbali mbali.

“Sisi katika suala zima la miundombinu, ndani ya miaka mitano tumefanikiwa kujenga vituo 487 na kati ya hivyo 293 tayari vimeanza kutoa huduma na vingine vikiwa katika hatua mbalimbali, vile vile tumefanikiwa kusimamia ujenzi wa Hospitali za Halmashauri 102, ambapo 99 ni zile zilizojengwa kwa fedha za Serikali na Wadau na Halmashauri mbili za Nyamagana na Arusha hawa walijizatiti na wameweza kujenga wao wenyewe kwa mapato yao ya ndani, aidha jumla ya Zahanati 1,198 zimekamilika, lakini pia kuna baadhi ya Mikoa inayofanya jitihada binafsi ikiwepo Mkoa wa Geita ambao wapo katika mpango wa kujenga Zahanati 100.” Alisisitiza Dkt. Ntuli

Mbali na ujenzi huo pia Dkt. Ntuli alielezea suala la maboma ya Zahanati, yapatayo 555 katika mwaka wa fedha wa 2020/21, ambapo katika hali ya sasa lazima kila Halmashauri, iweze kufanya maombi ya fedha zenyewe, utaratibu huo ambao ni mpya una lengo la kuonesha hatua na juhudi binafasi kwa kila Halmashauri. Aidha taarifa hiyo imeonesha mbali ya Zahanati vipo pia vituo vya Afya 52 ambavyo vilipata Milioni. 200 kila kimoja na sasa kila Kituo kitalazimika kuongezewa Milioni. 300 kila kimoja ili waweza kufikisha jumla ya Milioni. 500 ili wakamilishe ujenzi na kuanza kutoa huduma.

Katika Hatua Nyingine Dkt. Ntuli, alimfafanulia, Naibu Waziri juu ya tafiti tunduizi na kubaini baadhi ya Hospitali za Wilaya kama Sengerema na Kahama,  ambazo zimekuwa zikipokea kina mama kwa ajili ya kujifungua wapatao 900 kila mwezi, hivyo ipo haja Hospitali hizo kuzipatiwa huduma za kibingwa kwani umbali wa Hospitali hizo na Makao Makuu zilipo Hospitali za Rufaa za Mikoa ni mbali.

“Mfano kwa Wilaya ya Kahama hadi Shinyanga Mjini ni zaidi ya Kilomita.102, hali inayochangia Vifo vya kina Mama kutokana na kusafirishwa umbali mrefu, kwa mantiki hiyo, tumeamua suala hili kuwapelekea wenzetu wa Wizara ya Afya, ili Hospitali hizi sasa ziweze kupewa hadhi ya Rufaa ya Mkoa na kupelekewa huduma za kibingwa”. Alisema Ntuli.

Dkt. Festo John Dugange, aliteuliwa kuwa Naibu Waziri anayeshughulikia Afya Ofisi ya Rais-TAMISEMI tarehe 05 Desemba, 2020 na kuapishwa tarehe 09 Desemba, 2020 na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, Ikulu ya Chamwino Dodoma.

Na. Atley Kuni-TAMISEMI, Dodoma

Mwisho.

Matangazo

  • TOR - Msimbazi Watershed Management – Modelling May 26, 2025
  • Monitoring & Support, TOR - DMDP 2 SWM Service Framework & Delivery System in Dar May 26, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert May 12, 2025
  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert May 12, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • Nipo tayari kufanya kazi pamoja nanyi kufikia malengo ya Mhe. Rais – Prof. Tumaini Nagu

    May 26, 2025
  • TARURA IMEKUWA NA MCHANGO MKUBWA KWA SERIKALI YA AWAMU YA SITA

    May 26, 2025
  • MAPEPELE AWANOA MAAFISA HABARI WA TAMISEMI, AWATAKA WAWE WAZALENDO 

    May 26, 2025
  • MAHUSIANO MAZURI  NI NGUZO MUHIMU KATIKA UTEKELEZAJI WA MAJUKUMU-MHE.SAGINI

    May 26, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.