Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

Dar es Salaam na Tabora zatwaa ubingwa mpira wa Kengele

Imewekwa tar.: June 29th, 2019

Na Mathew Kwembe, Mtwara

Timu ya wavulana kutoka mkoa wa Dar es salaam na timu ya wasichana kutoka mkoa wa Tabora zimefanikiwa kujishindia nafasi ya kwanza baada ya kufanikiwa kuwabwaga wapinzani wao katika kuwania ubingwa wa mpira wa kengele katika fainali za UMITASHUMTA zilizofanyika jana kwenye viwanja vya chuo cha ualimu Mtwara.

Timu ya wavulana kutoka mkoa wa Dar es salaam ndiyo ilikuwa ya kwanza kufanikiwa kutwaa taji hilo baada ya kuifunga timu ya mkoa wa Lindi 23-13, huku mshindi wa tatu kwa upande wa wavulana ilikuwa timu ya Tanga baada ya kuifunga Tabora 14-7.

Kwa wasichana Tabora ilishika nafasi ya kwanza baada ya kuilaza Morogoro 16-7 na mshindi wa tatu kwa wasichana  ilikuwa timu kutoka mkoa wa Arusha baada ya kuilaza Tanga 8-6.

Wakati huo huo matokeo ya mchezo wa robo fainali soka wasichana baina ya Mwanza na Dar es salaam matokeo ni kuwa timu ya Mwanza ilifanikiwa kuingia nusu fainali baada ya kuifunga Dar es salaam kwa kutumia mikwaju ya penati 3-2 baada ya kutoka sare ya goli 1-1, Manyara ilifungwa na Mara 0-1, Kagera iliitoa Simiyu kwa penati 4-1 baada ya kutoka suluhu ya bila kufungana, na Morogoro iliondolewa na Kilimanjaro kwa penati 5-6 baada ya kutoka suluhu ya bila kufungana.

Katika soka maalum timu ya mkoa wa Dodoma ilifanikiwa kuilaza Kilimanjaro 1-0, Tabora ilichapwa na Ruvuma 0-5, Mtwara iliifunga Kagera 2-0, na Dar es salaam ilichabangwa na Shinyanga 1-5.

Kufuatia matokeo hayo, timu zilizofuzu hatua ya nusu fainali kwa soka wasichana ni Mwanza ambayo itacheza na Mara, huku mchezo mwingine utahusisha Kagera watakaomenyana na Kilimanjaro.

Katika soka maalum wavulana michezo ya nusu fainali itahusisha Dodoma watakaopambana na Ruvuma na mchezo mwingine utahusisha timu za Mtwara itakayopambana na Shinyanga

Kwa upande wa soka wavulana timu za Dar es salaam, Manyara, Mwanza, Geita, Kagera na Tanga tayari zimefuzu hatua ya robo fainali na zinasubiri wapinzani wao wacheze ili waweze kujua timu zitakazoshindana nazo.

Katika matokeo ya mechi zilizochezwa jana Iringa ilibugizwa na Lindi 1-7, Mbeya ilifungwa na Pwani 0-1, Mwanza iliichapa Simiyu 6-1, katavi ilifungwa na Songwe 2-4, Kagera ilifungwa na Rukwa 0-1 na Arusha iligalagazwa na Tabora kwa magoli 0-9.

Matangazo

  • TOR - Msimbazi Watershed Management – Modelling May 26, 2025
  • Monitoring & Support, TOR - DMDP 2 SWM Service Framework & Delivery System in Dar May 26, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert May 12, 2025
  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert May 12, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • Mtwale Atoa Mwongozo kwa Makatibu Tawala Wasaidizi wa Mikoa

    May 27, 2025
  • Nipo tayari kufanya kazi pamoja nanyi kufikia malengo ya Mhe. Rais – Prof. Tumaini Nagu

    May 26, 2025
  • TARURA IMEKUWA NA MCHANGO MKUBWA KWA SERIKALI YA AWAMU YA SITA

    May 26, 2025
  • MAPEPELE AWANOA MAAFISA HABARI WA TAMISEMI, AWATAKA WAWE WAZALENDO 

    May 26, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.