Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

Dar es Salaam kucheza na Mwanza robo fainali soka Wasichana UMITASHUMTA

Imewekwa tar.: June 29th, 2019

Na Mathew Kwembe, Mtwara

Timu za soka za wasichana za mikoa ya Dar es salaam na Mwanza zimetinga hatua ya robo fainali ya michuano ya UMITASHUMTA na zinatarajiwa kucheza leo katika viwanja vya chuo cha ualimu Mtwara.

Dar es salaam imefikia hatua hiyo baada ya kuibuka kinara katika kundi A na hivyo itachuana na mshindi wa pili kundi C Mwanza katika hatua ya robo fainali. Pambano lingine la robo fainali litazikutanisha timu za mikoa ya Manyara ambao iliibuka mshindi wa kwanza kutoka kundi B watakaochuana na mshindi wa pili kundi D timu ya soka ya wasichana kutoka mkoa wa Mara.

Mshindi wa kwanza kutoka kundi C, timu ya soka wasichana kutoka mkoa wa Kagera imepangwa kuchuana na mshindi wa pili kundi B, Simiyu huku mshindi wa kwanza kundi D Morogoro watachuana na mshindi wa pili kundi A, Kilimanjaro.

Kwa upande wa soka maalum wavulana, michuano hiyo pia imefikia hatua ya robo fainali na inatarajiwa kuchezwa leo katika viwanja vya chuo cha ualimu Mtwara ambapo mshindi wa kwanza kundi A Kilimanjaro atachuana na mshindi wa pili kundi C Dodoma. Mshindi wa kwanza kundi B Tabora atachuana na mshindi wa pili kundi D Ruvuma. Mchuano mwingine mkali utahusisha mshindi wa kwanza kundi C, Mtwara atachuana na mshindi wa pili kundi B, Kagera huku mshindi wa kwanza kundi D, Dar es salaam atachuana na mshindi wa pili kundi A, timu ya soka maalum wavulana kutoka mkoa wa Shinyanga.

Kwa upande wa soka wavulana, michuano hiyo bado inaendelea katika hatua ya makundi na inatarajiwa kuchezwa hatua ya robo fainali tarehe 1, julai, 2019 ambapo mshindi wa kwanza kundi A atacheza na mshindi wa pili kundi C, mshindi wa kwanza kundi B atachuana na mshindi wa pili kundi D, mshindi wa kwanza kundi C atacheza na mshindi wa pili kundi B na mshindi wa kwanza kundi D atachuana na mshindi wa pili kundi A.

Matokeo ya michezo iliyochezwa kundi A kuanzia tarehe 24 juni hadi tarehe 28 juni, 2019 katika soka wavulana inaonyesha kuwa Tanga imeifunga Singida 4-0, Dodoma wameichapa Mara 2-1, Dar es salam imetoka sare na Kilimanjaro 1-1, Singida imetoka suluhu na Kilimanjaro 0-0, Mara imefungwa na Dar es salaam 0-1, Tanga imeifunga Dodoma 2-1, na Dodoma imefungwa pia na Dar es salaam 2-3.

Kilimanjaro  iliifunga Tanga 1-0, Singida iliichapa Mara 2-0, Dodoma nayo iliifunga singida 2-1, Mara ikaichapa Kilimanjaro 2-1, Dar es salaam ikatoka suluhu na Tanga, Tanga ikaifunga Mara 3-0, Singida ikachapwa na Dar es salaam 0-3 na Kilimanjaro pia ikachapwa na Dodoma 0-3.

Matokeo ya kundi B soka wavulana, Mbeya ilichabangwa na mwanza 2-5, Pwani iliibugiza Iringa 4-0, Lindi nayo ikaichapa Mtwara 2-0, Mwanza ikaifunga Pwani 3-0, Simiyu ikaifunga Iringa 2-0, na Mbeya ikaichapa Mtwara 1-0, Lindi ikatoka suluhu na Simiyu, Mtwara ikafungwa na pwani 0-3, Iringa nayo ikabugizwa na Mwanza 1-5 na Mbeya ilipata kipigo kutoka Simiyu 0-1, Mwanza imeichapa Mtwara 4-0, Pwani ikatoka sare na Lindi 1-1, Iringa ikapata kipigo kutoka Mbeya 0-4, Mtwara nayo ikafungwa na Simiyu 1-3 na Mwanza ikatoka sare na Lindi 1-1.

Matokeo ya michezo ya kundi C yanaonyesha Geita iliichapa Kigoma 1-0, Manyara iliifunga Njombe 2-1, Shinyanga ilikubali kichapo kutoka kwa Ruvuma 0-2, Kigoma iliifunga Ruvuma 1-0, na Njombe ikaifunga Shinyanga 4-1. Pia Geita ikaifunga Manyara 2-0, Manyara ilikubali kipigo kutoka kwa Shinyanga 0-5, Ruvuma nayo ilifungwa na Geita 0-2, Kigoma ikaifunga Njombe 1-0, Manyara ikaichapa Kigoma 4-0, Njombe na Ruvuma zikatoka suluhu, Shinyanga ikafungwa na Geita 0-1, Geita ikaichapa Njombe 4-0, Kigoma ikatoka sare na Shinyanga 1-1 na Ruvuma ikakubali kichapo kutoka kwa Manyara 1-3.

Katika michezo iliyochezwa kundi D soka wavulana, matokeo yanaonyesha Katavi ilifungwa na Kagera 1-2, Morogoro ilichapwa na Tabora 1-2, Rukwa ikaifunga Songwe 3-1, Morogoro ikatoka sare na Rukwa 1-1, Kagera ikaichapa Arusha 3-0, huku Katavi na Tabora zikitoka suluhu ya bila kufungana. Matokeo mengine Songwe ilichapwa na Kagera 0-2, Tabora na Rukwa zikatoka suluhu, Arusha ikachapwa na Morogoro 1-3, Arusha pia ilibugizwa na Songwe 1-7, Katavi ilifungwa na Rukwa 0-1, Morogoro ilifungwa na kagera 1-2, Arusha ilifungwa na katavi 0-2, Tabora ilichapwa na Kagera 0-3 na Morogoro na Songwe zilitoka suluhu ya bila kufungana.

Michuano hiyo inatarajiwa kuendelea leo na kesho ili kukamilisha ratiba kwa timu za soka wavulana kutoka makundi A hadi D kwa soka wavulana ili kukamilisha ratiba ya michuano hiyo kabla ya kuchezwa hatua ya robo fainali kesho kutwa katika viwanja hivyo hivyo vya chuo cha ualimu Mtwara.

Matangazo

  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert (extension) 1 May 28, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert (extension) May 28, 2025
  • TOR - Msimbazi Watershed Management – Modelling May 26, 2025
  • Monitoring & Support, TOR - DMDP 2 SWM Service Framework & Delivery System in Dar May 26, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • RC CHALAMILA ATAKA MACHINGA KARIAKOO KUFUNGUA NJIA

    May 30, 2025
  • Wamiliki wa vituo vya kulelea watoto wadogo mchana watakiwa kuzingatia miongozo na kanuni zilizopo.

    May 29, 2025
  • Mhe. Katimba awapokea Wabunge wa Zambia waliokuja kujifunza kuhusu Usimamizi na Uendeshaji wa Mamlaka za Serikali za Mitaa Tanzania Bara

    May 28, 2025
  • Mtwale Atoa Mwongozo kwa Makatibu Tawala Wasaidizi wa Mikoa

    May 27, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.