Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

Bil 16.4/- zarejesha hadhi ya Shule za Sekondari za Ufundi nchini

Imewekwa tar.: January 22nd, 2021

Na Atley Kuni, Dodoma

WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe. Selemani Jafo, amesema uwekezaji wa sh. bilioni 16.4 zilizotumika kukarabati shule 9 za ufundi nchini imezifanya shule hizo kurejea katika hadhi yake.

Ameeleza kumalizika kwa kazi hiyo ya kukarabati shule hizo zilizokuwa na miundombinu chakavu kutawezesha wanafunzi wote watakaochaguliwa kujiunga na shule hizo kuhitimu wakiwa na ujuzi uliokusudiwa na Serikali.

Mbali na uwekezaji wa fedha hizo, Serikali pia imeajiri walimu 150 ambao wamepangwa katika shule zote 9 lengo likiwa ni kupata tija iliyokusudiwa kwa Watoto wa kitanzania kuhitimu wakiwa na maarifa yakuweza kujiajiri.

Waziri Jafo, amesema lengo la Serikali ya awamu tano, inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt John Pombe Magufuli, ni utekelezaji sera ya Tanzania ya Viwanda iliyo asisiwa mwaka 2016, ambapo amesema wanafunzi hao baada ya kuhitimu elimu zao wataweza kujiajiri katika viwanda vidogo, lakini vile vile kutumika katika viwanda mbalimbali hapa nchini.

“Hatutegemei kuona, wanafunzi wakiwa shuleni wanajifunza nadharia peke yake, tunataka wajifunze pia kwa vitendo ili wawe na ujuzi wakuzalisha baadhi ya vitu wanavyo jifunza mathalani chaki, Vijiti vya kusafisha kinywa ‘toothpick’, kwakutaja baadhi, na kuongeza kuwa,

“katika wakati wa sasa ni vema kufikiria zaidi nje ya boksi, na hasa kwakuwashirikisha baadhi ya wataalam mafundi wa mtaani wenye maarifa ya kutosha katika fani tofauti tofauti ili  kuwaongezea maarifa na ujuzi wanafunzi hao”.

Shule zilizokarabatiwa na ambazo tayari zimesha pangiwa wanafunzi na walimu wa fani mbalimbali ni Bwiru wavula ya mkoani Mwanza iliyo fanyiwa ukarabati kwa gharama ya Zaidi ya sh. Milioni 825, Shule ya Ufundi Chato ya mkoani Geita iliyokarabatiwa kwa gharama ya shilingi bilioni 3.9, Shule ya Ufundi Ifunda ya mkoani Iringa kwa gharama ya shilingi bilioni, 3.6, Shule ya Ufundi Iyunga iliyopo mkoani Mbeya iliyo gharimu shilingi bilioni 1.01 na Moshi Ufundi ya mkoani Kilimanjaro iliyokarabatiwa kwa shillingi bilioni 2.1.

Shule zingine ni Shule ya Ufundi Mtwara, kwa gharama ya bilioni, 1.3 Musoma ufundi ya mkoani Mara, kwa gharama ya shilingi bilioni 1.2 Mwadui ya mkoani Shinyanga, iliyo pokea milioni sh. Milioni 226 kwa ajili ya ukarabati na Shule ya Ufundi Tanga ya mkoani Tanga, iliyo gharimu shilingi, bilioni 2.1 ambapo gharama yake kuu ni sh. bilioni 16,4.

Wakiongea kwa njia ya Mkutano kwa masafa ‘Video Conferences’ wakuu wa mikoa hiyo pamoja na wataalamu walioshiriki kikao hicho, kutoka katika Mikoa hiyo tisa, waliiomba Serikali kuhakikisha inaboresha Mitaala ili iweze kukidhi mahitaji ya sasa, ambapo Waziri Jafo, akitolea ufafanuzi alisema, anaipongeza Wizara ya Elimu kwa kazi kubwa ya maboresho ya Mitaala lakini akautaka uongozi wa Elimu TAMISEMI, kulichukua jambo hilo na kulifanyia kazi kama ilivyo shauri.

Akihitimisha kikao hicho, Waziri Jafo, amewaelekeza Wakuu wa Mikoa kuwa walezi wakuu shule hizo, kwakuzitembelea na kujua changamoto wanazokabiliana nazo lakini pia kuzitafutia ufumbuzi wa kudumu.

Katika hatua nyingine, Waziri jafo ametumia wasaa huo, kuwagiza Wakurugenzi kuhakikisha wanawalipa fedha za kujikimu watumishi wote waliopangiwa kazi katika maeneo yao ndani ya siku saba.

 

Matangazo

  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert (extension) 1 May 28, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert (extension) May 28, 2025
  • TOR - Msimbazi Watershed Management – Modelling May 26, 2025
  • Monitoring & Support, TOR - DMDP 2 SWM Service Framework & Delivery System in Dar May 26, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • RC CHALAMILA ATAKA MACHINGA KARIAKOO KUFUNGUA NJIA

    May 30, 2025
  • Wamiliki wa vituo vya kulelea watoto wadogo mchana watakiwa kuzingatia miongozo na kanuni zilizopo.

    May 29, 2025
  • Mhe. Katimba awapokea Wabunge wa Zambia waliokuja kujifunza kuhusu Usimamizi na Uendeshaji wa Mamlaka za Serikali za Mitaa Tanzania Bara

    May 28, 2025
  • Mtwale Atoa Mwongozo kwa Makatibu Tawala Wasaidizi wa Mikoa

    May 27, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.