Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

WAZIRI MKUU MAJALIWA AFUNGUA RASMI MASHINDANO YA UMITASHUMTA NA UMISSETA 2025

Imewekwa tar.: June 9th, 2025

 OR-TAMISEMI,  Iringa

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa, amezitaka Ofisi ya Rais – TAMISEMI, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, pamoja na Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kushirikiana kikamilifu katika kukamilisha mradi wa ujenzi wa shule 56 za kuendeleza vipaji vya michezo.

Mhe. Majaliwa ametoa agizo hilo leo, Juni 9, 2025, wakati wa ufunguzi rasmi wa mashindano ya Umoja wa Michezo na Taaluma kwa Shule za Msingi (UMITASHUMTA) na Sekondari (UMISSETA), yaliyofanyika katika Viwanja vya Kichangani, Kata ya Kihesa, Manispaa ya Iringa, mkoani Iringa.

Aidha, amezitaka Ofisi ya Rais – TAMISEMI pamoja na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kuhakikisha kuwa ratiba za michezo zinawekwa rasmi kwenye mipango ya kila shule na kutekelezwa ipasavyo ili kutoa nafasi kwa wanafunzi kushiriki michezo mara kwa mara kwa lengo la kukuza vipaji.

 "Katika shule zetu tunahitaji ratiba za michezo ili vijana wetu baada ya masomo waweze kushiriki katika shughuli za michezo. Hili litasaidia kuinua vipaji na kuwaandaa kwa mashindano haya ya kitaifa," alisema Waziri Mkuu.

Mhe. Majaliwa amevitaka vyama vya michezo vya kitaifa kupeleka wataalamu kwenye mashindano ya UMITASHUMTA na UMISSETA ili kuwabaini wachezaji wenye vipaji maalum watakaoendelezwa kwa lengo la kuunda timu bora za taifa.

Aidha, amewaagiza Wakurugenzi wa Halmashauri zote kuhakikisha walimu wa michezo wanapewa mafunzo maalum ya kisasa kuhusu sheria, mbinu na mabadiliko ya michezo, na kuwapeleka kwenye vyuo vya michezo vilivyopo nchini ili kuongeza ufanisi wa ufundishaji.

Waziri Mkuu pia ameagiza Kituo cha Mafunzo cha Malia kutumika kikamilifu kwa ajili ya kuwajengea uwezo walimu wa michezo ili kusaidia kukuza vipaji vya wanafunzi katika ngazi ya shule.

Vilevile, amezitaka Halmashauri zote nchini kuhakikisha maeneo ya wazi yaliyotengwa kwa michezo hayavamiwi na shule zote za msingi na sekondari zinakuwa na viwanja kwa ajili ya michezo mbalimbali inayoshirikishwa kwenye mashindano haya.

Ameitaka TAMISEMI, kwa kushirikiana na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, kuandaa mpango mkakati wa kitaifa utakaohakikisha kila shule inakuwa na miundombinu ya michezo, ikiwemo viwanja vya riadha, ili kuimarisha ushiriki wa wanafunzi katika michezo.

Pia, amezihimiza taasisi hizo kushirikiana na wadau wa michezo, kama makampuni ya biashara yanayodhamini michezo, kuendeleza vipaji vilivyoibuliwa mashuleni kwa lengo la kuzalisha wanamichezo bora.

Kwa upande mwingine, Waziri Mkuu ameitaka Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo kutoa vibali kwa shule binafsi na academies zinazolenga kukuza vipaji vya michezo kuanzia ngazi ya awali, ili ifikapo umri wa miaka 14 vijana wawe wameimarika kitaaluma na kimwili.

Mwisho, amewataka Watanzania wote kujenga tabia ya kufanya mazoezi ya viungo mara kwa mara ili kuwa  na afya bora ambayo ndio msingi wa taifa lenye nguvu.

Matangazo

  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert (extension) 1 May 28, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert (extension) May 28, 2025
  • TOR - Msimbazi Watershed Management – Modelling May 26, 2025
  • Monitoring & Support, TOR - DMDP 2 SWM Service Framework & Delivery System in Dar May 26, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • SERIKALI YAIPONGEZA TARURA KWA KAZI NZURI WANAZOFANYA MHE: MCHENGERWA AWASIHI KUTOKATISHWA TAMAA

    June 26, 2025
  • MIRADI YA TACTIC IMELETA MAPINDUZI YA KIUCHUMI MAJIMBONI KWETU- WABUNGE

    June 26, 2025
  • MIJI 11 YA MRADI WA TACTIC KUIMARISHA  HUDUMA ZA USAFIRI

    June 25, 2025
  • ZAIDI YA WATU 700 KUPATIWA MATIBABU YA MACHO RUNGWE.

    June 25, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.