Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

Waziri Mkuu kufungua mashindano ya FEASSSA kesho jijini Arusha

Imewekwa tar.: August 15th, 2019

Na Mathew Kwembe, Arusha

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Kassim Majaliwa kesho anatarajiwa kuwa mgeni rasmi kwenye ufunguzi wa mashindano ya Michezo ya shule za Sekondari za Afrika Mashariki (FEASSA) utakaofanyika katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha.

Jumla ya wanamichezo 3500 kutoka nchi za Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi, wenyeji Tanzania bara na Zanzibar pamoja na nchi ya Malawi ambayo imealikwa watashiriki michuano hiyo.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Arusha Mratibu wa Mashindano hayo bwana Leonard Thadeo amesema kuwa ufunguzi rasmi utafanyika kesho saa 8.00 mchana kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid ambapo utachezwa mchezo mmoja wa ufunguzi wa mashindano hayo kati ya timu ya soka ya Lindi dhidi ya timu ya St. Mary’s kutoka Uganda.

 “Tayari timu nyingi zimekwishawasili, Uganda waliwasili jana, na nimeambiwa timu kutoka Rwanda jana walilala Singida na kwa ujumla maandalizi kwa ajili ya mashindano hayo yamekamilika,” amesema.

Mratibu huyo ameitaja michezo itakayoshindaniwa kwenye michuano hiyo kuwa ni pamoja na Soka, riadha, netiboli, mpira wa mikono, mpira wa mikapu, vinyoya, raga, mpira wa magongo, mpira wa meza, mpira wa kengele na michezo mingineyo.

Michezo hiyo imepangwa kuchezwa kuanzia kesho tarehe 16 agosti na fainali za michuano hii inatarajiwa kufanyika tarehe 24 agosti, 2019.

Bwana Thadeo amevitaja viwanja vitakavyotumika kwa ajili ya michuano hiyo kuwa ni pamoja na uwanja wa Magereza, Sheikh Amri Abeid, ISM, St. Constantine, TGT na ukumbi wa michezo wa Paloti.

Wakati huo huo semina ya siku tatu kwa walimu wa michezo wa shule mbalimbali nchini iliyokuwa ikifanyika katika ukumbi wa shule ya St Patrick ya jijini Arusha imefungwa rasmi leo na Mwenyekiti wa Baraza la Michezo Tanzania bwana Leodger Tenga.

Akizungumza mara baada ya kufunga semina hiyo ambayo iliwahusisha wakufunzi kutoka chuo kikuu cha Tsukuba cha nchini Japan, bwana Tenga amesema kuwa wamefundisha mambo mengi yakiwemo utawala, mbinu za michezo, afya za michezo pamoja na namna wanamichezo wanavyoweza kupiga vita matumizi ya madawa ya kulevya.

Pamoja na kuwashukuru wakufunzi hao, bwana Tenga amesema kuwa kozi za namna hiyo ni vizuri zikafanyika mara kwa mara kwani dunia imebadilika, michezo siyo tu inafanikiwa kwa kutaka, lazima kuhakikisha kuwa kuna mbinu sahihi, vifaa sahihi na wataalamu sahihi wa michezo.

Amesifu kuwepo kwa ushirikiano baina ya chuo kikuu cha Tsukuba na Tanzania katika kuendeleza sekta ya michezo ambapo chimbuko la ushirikiano huo limetokana na mahusiano baina ya Mratibu wa Michezo kutoka Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa bwana Leonard Thadeo ambaye aliwahi kusoma katika chuo kikuu cha Tsukuba cha nchini Japan.

Bwana Tenga amesema kufuatia kuimarika kwa ushirikiano huo wamewaomba wakufunzi hao wawe wanakuja mara kwa mara nchini kwa ajili ya kutoa mafunzo ya aina kama hiyo kwani mahitaji ya mafunzo bado ni makubwa sana.l

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert May 12, 2025
  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert May 12, 2025
  • Fursa kwa Wahitimu wa Kidato cha Nne 2024 kubadili Tahasusi na Kozi April 02, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI AJIRA ZA AFYA - TAMISEMI 2025 March 15, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • NENDENI MKAITANGAZE SERIKALI.

    May 24, 2025
  • SOKO LA KISASA LA NYAMA CHOMA LAZINDULIWA VINGUNGUTI

    May 24, 2025
  • DKT. Biteko asisitiza wazazi kuthamini nafasi ya familia katika malezi na makuzi ya mtoto.

    May 24, 2025
  • Mhe. Rais Samia amtaka Prof. Nagu kuboresha  huduma ya afya ya msingi.

    May 24, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.