• Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Machapisho
    • Taarifa za Mapato
    • Majarida
    • Fomu Mbali mbali
    • Presentations
  • Miongozo
    • Miongozo OR TAMISEMI
    • Miongozo ya mradi wa SEQUIP
    • Green and Smart Cities
    • Miongozo ya Kilimo
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Michoro ya Ujenzi
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)

Waziri Mkuu ashusha Neema kwa Maafisa Ustawi wa Jamii

Imewekwa tar.: January 30th, 2019

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ameziagiza Wizara ya Ofisi ya Rais, Tamisemi na ile ya Afya, maendeleo ya jamii, jinsia, wazee na watoto kukutana na kupitia muundo wa utumishi kwa maafisa ustawi wa jami ili kuwawezesha kufanya kazi zao kwa ufanisi.
Waziri Mkuu ameyasema hayo wakati akifungua Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Maafisa Ustawi wa Jamii wa Mikoa na Halmashauri unaofanyika kwa siku tatu kwenye ukumbi wa mikutano wa Jakaya Kikwete uliopo Jijini, Dodoma.
Wizara hizi mbili zikutane na kuangalia namna bora ya kubadili muundo wa maafisa hawa ili kuwatengenezea mazingira mazuri kwa ajili ya kazi yao.
“Maafisa Ustawi ni watu muhimu sana kwenye jamii ni muhimu nafasi yao iakwekwa vizuri kwenye muundo na kama italazimu kubadili muundo ili kazi yao ifanyike vizuri mfanye hivyo  na kama ni suala linalohitaji marakebisho ya sheria mlete na bahati nzuri hapa tuna mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa Mhe Jason ( Mb) litafanyiwa kazi” alisema Mhe Majaliwa.
Wakati huo huo Waziri Mkuu Majaliwa  amekemea tabia ya halmashauri kuwataka watu wenye ulemavu kutoa asilimia 10 ya mkopo wanaochukua kama dhamana wakati wa kupewa mikopo.
“Kuna mbunge amesema kuna halmashauri zinawataka watu wenye ulemavu kutoa asilimi 10 ya thamani ya mkopo wanaochukua kama depost, jambo hilo haliwezekani.
Mhe. Majaliwa aliongeza: “ Kuwataka waweke depost hilo jambo halipo na hata Sheria yenyewe haisemi hivyo, hivi watu wenye ulemavu watazipata wapi fedha hizo?
“ Ninyi maafisa ustawi wa jamii hakikisheni mnalisimamia hilo, fedha inatakiwa kutolewa kama sheria inavyoruhusu, na hii si kwa mapenzi ya mkurugenzi au baraza la madiwani.
Serikali iliweka sheria ambayo inazitaka kisheria halmashauri zote nchini kutenga asilimia 10 kutoka kwenye mapato ya ndani kwa ajili ya wanawake na vijana na  asilimia 2 zinaelekezwa kwa watu wenye ulemavu, asilimia nne kwa wanawake na asilimia 4 kwa vijana.
Naye Naibu Waziri wa Tamisemi, Mhe. Josephat Kandege alisema Serikali imekuwa ikichukua hatua mbalimbali kuimarisha sekta ya ustawi wa jamii kwa kutekeleza matakwa ya kisheria yenye dhamira ya kuboresha ustawi wa jamii yetu hapa Nchini .
Alisema tumeandaa  Waraka wa utekelezaji wa Sheria ya Wati wenye Ulemavu Na. 9 ya mwaka 2010 lengo ikiwa ni kuhimiza wajibu wa Wakuu wa Mikoa katika kusimamia utekelezaji wa Sheria Na. 9 ya watu wenye ulemavu.
Pia tumepeleka Waraka wa mwaka 2018 kwa Wakuu wa Mikoa kushughulikia mashauri ya watoto  ili kupunguza ama kuzuia ukatili dhidi ya watoto alisema Kandege.
“Kwa nyakati tofauti bajeti ua utekelezaji wa masuala ya Ustawi wa Jamii umekua ukifungamanishwa pamoja na bajeti ya Lishe , kwa bajeti ya mwaka 2019/20 tumefanikiwa kufanya maboresho ya kimfumo ambapo Bajeti za Ustawi wa Jamii umewekewa dirisha maalumu ndani ya mfumo wa Planrep ambalo linajulikana kama “Council Comprehensive Social Welfare Operatiobal Plan”; Jitihada hizi zitasaidia kuongeza ufanisi katika uwajibikaji wa watendaji, kuweka uwazi na kudhibiti matumizi ya fedha za miradi ikiwemo fedha za wadau wa maendeleo” alisema Kandege.
Naye Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Faustine Ndugulile aliwaagiza maafisa ustawi wa jamii nchi nzima kukaguza vituo vya kulelea watoto ili ambavyo havina sifa na vibali halali vifungwe.
“ Kumekuwa na ongezeko la vituo vya kulelewa watoto yatima, bahati nzuri kuna watu ambao ni waaminifu, lalini kuna wengine wasiowaadilifu, Tumepokea malalamiko kuwa baadhi ya watu wanawatumikisha watoto hao kwenye biashara ya ombaomba, biashara ya ngono na vingine kuwa vituo vya kususanyia watoto kwa ajili ya biashara ya utumwa.
“ Hivyo maafisa wote manatakiwa kuvikagua vituo hivi na visivyo na sifa vifungwe na hakikisheni wanawaletea taarifa zao kila robo mwaka, nusu mwaka na za mwaka mzima.”
Pia Dk. Ndungulile alisema serikali iko katika hatua ya kuandika sheria itakayosimamia sekta hiyo sambamba na uanzishwaji wa Baraza litakalosimamia maadili ya maafisa ustawi wa jamii.
Naye Mwakilishi wa Mkazi wa UNICEF, Maniza Zamani pamoja na kuishauri serikali kuweka mazingira rafiki ya ufanyaji kazi kwa maafisa ustawi wa jamii na kuahidi kuwa wadau wa maendeleo nchini Tanzania wataendelea kuisaidia serikali katika kuimarisha sekta hiyo ili kuboresha utoaji wa huduma.
Naye Mkurugenzi Msaidizi wa Huduma za Ustawi wa Jamii, Ofisi ya Rais Tamisemi, Rasheed Maftah alisema lengo la mkutano huo ni kukumbushana maadili ya kazi Lengo la kukumbushana maandili ya kazi, uwajibikaji na weledi katika kuhudumia wananchi wenye mahitaji.
“ Pia tumekutana ili kuepana mrejesho wa utekelezaji wa shughuli za ustawi wa jambii kwenye mamlaka za serikali za mitaa na kuwezesha kufahamu mafanikio na
“ Pia kujadili maendeleo na changamoto zinazohusu utoaji wa huduma za ustawi wa jamii katika mikoa na mamlaka za serikali za mitaa na kushirikishana mbinu za utatuzi na hatimaye kupeana uelekeo wa pamoja wa utekelezaji wa mwaka huu wa fedha 2019/2020.
Mkutano huu unaofanyika kwa mara ya kwanza toka majukumu ya ustawi wa jamii yagatuliwe  mwaka 2006 unaenda sambamba na Kauli Mbiu “Uadilifu, Weledi na Uwajibikaji katika utoaji wa huduma za Ustawi wa Jamii Ngazi ya Mamlaka ya Serikali za Mitaa ni Nguzo katika kuelekeza uchumi wa kati wa viwanda”.

Matangazo

  • Orodha ya waliopata vibali vya Uhamisho Septemba - Disemba 2022 (OR - TAMISEMI) January 21, 2023
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kidato cha Kwanza Waliorudia Mtihani January 15, 2023
  • Matumizi ya Lugha ya Kiswahili na Kingereza January 14, 2023
  • Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Kwanza 2023 December 14, 2022
  • Orodha ya Waliopangwa kwenye Vituo vya Kazi Kada za Afya (Awamu ya Pili) Agosti 2022 August 30, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA KWA KADA ZA AFYA (Marudio) July 20, 2022
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • BODI YA MIKOPO YA SERIKALI ZA MITAA KUSUKWA UPYA

    January 23, 2023
  • MAKAMU WA RAIS AWAPONGEZA DODOMA JIJI KWA UWEKEZAJI

    January 20, 2023
  • SERIKALA YASISITIZA KILA MMOJA KUTUNZA MAZINGIRA

    January 20, 2023
  • TANZANIA ITAENDELEA KUSHIRIKANA NA WADAU KATIKA MAPAMBANO DHIDI YA UKIMWI

    January 20, 2023
  • Angalia zote

Video

Taarifa ya Ukusanyaji wa Mapato ya Halmashauri, kipindi cha robo ya pili ya mwaka wa fedha 2021/22
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.