• Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

Waziri Jafo ataka Zimamoto, Skauti wakomeshe majanga ya moto shuleni

Imewekwa tar.: February 26th, 2021

Na Atley Kuni, DODOMA

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo amelitaka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji nchini lishirikiane na Chama cha Skauti Tanzania katika kukomesha majanga yatokanayo na moto kwenye Shule za Msingi na Sekondari.

Mhe.Jafo ameyasema hayo leo katika makao Makuu ya Jeshi la Zimamoto Tanzania jijini Dodoma, wakati akizindua kampeni ya pamoja kati ya taasisi hizo mbili, huku akitaja kuwa, mojawapo ya sababu zinazo changia kutokea kwa majanga ya moto ni pamoja na kundi la wanafunzi kutokuwa na uwelewa wa kutosha dhidi ya elimu, hivyo kuanza kwa ushirikiano huo itakuwa ni mwanzo mpya ma mzuri katika kupambana na majanga ya moto shuleni.

Amesema majanga ya moto yanapotokea wanafunzi wanapaswa kuwa na maandalizi ya kutoshaikiwepo  kielemu, pili ya kupambana nayo na tatu katika hali ya kuzuia yasitokee.

“Lakini katika siku za hivi karibuni tumeshuhudia baadhi ya shule zikiungua kwa moto na nyingine kuteketea, chanzo kikubwa ukiangalia ni hizi sababu zilizo ainishwa na Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zima Moto na uokoaji” amesisitiza Mhe Jafo.

Amesema hivi sasa Serikali chini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, inazidi kujenga na kuimarisha miundombinu ya shule nchi nzima, ikiwa ni pamoja na ujenzi wa Shule mpya 1000, hivyo kukamilika kwake lazima kuendane na elimu ya Majanga mbali mbali ikiwemo elimu ya kujikinga dhidi ya moto.

Kuhusu makubaliano baina ya Jeshi la Zimamoto na Uokoaji na Chama cha Skauti Tanzania  kushirikiana katika kutokomeza majanga ya moto shuleni, Waziri Jafo amesema ushirikiano huo unampatia faraja kubwa kwani ana imani, miundombinu inayojengwa sasa hata ile iliyokarabatiwa ya shule kongwe 86 kati ya 89 zilizotumia Shilingi bilioni 89 itatunzwa na kulindwa ipasavyo kutokana na elimu kwa Skauti wanafunzi waliopo shuleni.

Waziri Jafo, amesema Chama cha Skauti Tanzania kimekuwa na jukumu kubwa la kujenga uzalendo miongoni mwa vijana wa kitanzania wawapo shuleni huku akiwataka Maafisa Elimu wa Mikoa na Halmashauri kuendelea kutoa ushirikiano kwa vyama vya Skauti ngazi ya Mkoa na Wilaya, ili uzalendo uliojengeka miongoni mwao uzidi kuimarika.

Akitoa salam za Jeshi hilo wakati wa hafla hiyo, Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto nchini John Masunga, amesema, Jeshi limeanzisha kikosi kazi kwa ushirikiano na Wizara ya elimu, sayansi na teknolojia na Ofisi ya Rais-TAMISEMI, shabaha ikiwa ni kuhakikisha elimu dhidi ya majanga ya moto inawafikia wanafunzi lakini kuongeza uelewa wa pamoja juu ya athari za moto miongoni mwao.

Naye Kamishna Mkuu wa Skauti nchini Mhe. Mwantumu Mahiza, amesema mara zote Skauti wamekuwa wakitekeleza wajibu wao kwa mujibu wa viapo vyao na kuwa wanatambua Serikali inatumia fedha nyingi kwenye uwekezaji wa miundombinu ya shule kwa mantiki hiyo wao kama Skauti lazima wawe mstari wa mbele katika kuilinda.

Hafla hiyo imehudhuriwa na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi, Makatibu Wakuu wa Wizara ya elimu, sayansi na teknolojia na Mambo ya Ndani, na Naibu Katibu Mkuu anayeshughulikiwa Elimu Ofisi ya Rais-TAMISEMI.

Wageni wengine walioshiriki katika hafla hiyo ni Makamishana wa Jeshi hilo kutoka Makao Makuu, Makamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji wa Mikoa, Maafisa Elimu wa mikoa na Makamanda wa Skauti kote Tanzania.

 


Matangazo

  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert (extension) 1 May 28, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert (extension) May 28, 2025
  • TOR - Msimbazi Watershed Management – Modelling May 26, 2025
  • Monitoring & Support, TOR - DMDP 2 SWM Service Framework & Delivery System in Dar May 26, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • NIMESAINI NOTISI ZA KUVUNJA MABARAZA YA MADIWANI - MCHENGERWA

    June 15, 2025
  • MANYARA BINGWA RIADHA WASICHANA NA WAVULANA MITA 1,500

    June 15, 2025
  • MHE MCHENGERWA AWATAKA MA RC, DC KUONGOZA JOGGING KWENYE MAENEO YAO

    June 14, 2025
  • MANYARA NA MWANZA MABINGWA RIADHA MITA 800 

    June 14, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.