Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

WAKURUGENZI WAPEWA MWEZI MMOJA KUKAMILISHA UJENZI WA MIUNDOMBINU YA SHULE ZA WASICHANA

Imewekwa tar.: July 31st, 2024

Na. James K. Mwanamyoto OR-TAMISEMI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Mohamed Mchengerwa ametoa mwezi mmoja kwa Wakurugenzi wa Halmashauri kukamilisha ujenzi wa miundombinu ya shule mpya za sekondari za bweni za wasichana za mikoa ambazo zimejengwa katika halmashauri zao ili wanafunzi walioripoti katika shule hizo wapate mazingira bora na rafiki ya kupata elimu.

Mhe. Mchengerwa ametoa maelekezo hayo wakati akipokea taarifa za ujenzi wa shule hizo 26 za sekondari za wasichana za mikoa wakati wa kikao cha tathmini ya ujenzi wa shule hizo kilichofanyika katika Ukumbi wa Arnautoglo wa Manispaa ya Ilala jijini Dar es Salaam.

Mhe. Mchengerwa amesema, alitegemea wakurugenzi watoe taarifa ya kukamilika kwa ujenzi wa shule hizo kwa asilimia 100 jambo ambalo halijatekelezeka, wakati yeye akiwa kwenye ziara ya Mhe. Rais Mkoani Rukwa alimuahidi Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa ndani ya mwezi mmoja miundombinu ya shule zote 26 itakuwa imekamilika.

Waziri Mchengerwa ameanisha kuwa, wapo wakurugenzi amewapatia wiki mbili, wiki tatu na wengine mwezi mmoja wa kuhakikisha wanakamilisha ujenzi wa miundombinu iliyosalia katika shule hizo za wasichana za mikoa, isipokuwa mkurugenzi anayesimamia ujenzi wa shule ya mkoa wa Rukwa ambaye amempatia miezi 2.

“Hakutakuwa na nyongeza ya muda katika kipindi ambacho tumekubaliana mkamilishe ujenzi wa miundombinu ya shule hizo, na sitosita kumchukulia hatua mkurugenzi yeyote atakayeshindwa kukamilisha ujenzi wa miundombinu ya shule kwa mujibu wa makubaliano yetu,” Mhe. Mchengerwa amesisitiza.

Mhe. Mchengerwa ameongeza kuwa, yeye binafsi pamoja na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan wanawategemea wakurugenzi hao katika usimamizi wa miradi mbalimbali inayolenga kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo Bw. Kagurumjuli Titus amesema kwamba wamepokea maelekezo ya Waziri Mchengerwa na kuhaidi kuwa, manispaa yake itakamilisha ndani ya siku 15 hadi 21 ujenzi wa miundombinu ya shule ya mkoa ya Dar es Salaam ambayo ilikuwa haijakamilika kwani Mhe. Rais ameshawapatia fedha.

Naye, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Tunduma Bi. Mariam Chaurembo amesema kuwa, Halmashauri yake kwa niaba ya mkoa wa Songwe imejipanga kutekeleza maelekezo na Waziri Mchengerwa ya kukamilisha ujenzi wa miundombinu ya Shule ya Wasichana ya Mkoa wa Songe ndani ya mwezi mmoja kama alivyoelekeza.

Kikao hicho cha tathmini ya ujenzi wa shule 26 za sekondari za wasichana za mikoa, kimeudhuriwa na Wakurugenzi wa Halmashauri, Maafisa Elimu wa Sekondari, Wahandisi wa Halmashauri na Maafisa manunuzi wa Halmashauri.

Matangazo

  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert (extension) 1 May 28, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert (extension) May 28, 2025
  • TOR - Msimbazi Watershed Management – Modelling May 26, 2025
  • Monitoring & Support, TOR - DMDP 2 SWM Service Framework & Delivery System in Dar May 26, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • RC CHALAMILA ATAKA MACHINGA KARIAKOO KUFUNGUA NJIA

    May 30, 2025
  • Wamiliki wa vituo vya kulelea watoto wadogo mchana watakiwa kuzingatia miongozo na kanuni zilizopo.

    May 29, 2025
  • Mhe. Katimba awapokea Wabunge wa Zambia waliokuja kujifunza kuhusu Usimamizi na Uendeshaji wa Mamlaka za Serikali za Mitaa Tanzania Bara

    May 28, 2025
  • Mtwale Atoa Mwongozo kwa Makatibu Tawala Wasaidizi wa Mikoa

    May 27, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.