• Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Machapisho
    • Taarifa za Mapato
    • Majarida
    • Fomu Mbali mbali
    • Presentations
  • Miongozo
    • Miongozo OR TAMISEMI
    • Miongozo ya mradi wa SEQUIP
    • Green and Smart Cities
    • Miongozo ya Kilimo
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Michoro ya Ujenzi
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)

‘Wakurugenzi Msiingie Mtegoni’ – Jafo.

Imewekwa tar.: October 3rd, 2019

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mhe. Seleman Jafo amewatahadharisha wakurugenzi wapya walioteuliwa hivi karibuni kukwepa mtego uliowanasa wenzao waliondolewa madarakani na badala yake wakajenge mshikamano na umoja kwa watumishi watakao wakuta kwenye vituo vyao vipya vya kazi.

Akizungumza katika kikaokazi cha Wakurugenzi hao kilichokwenda sambamba na zoezi la kula kiapo cha Maadili kwa viongozi wa umma, Jafo amewatahadharisha viongozi hao dhidi ya baadhi ya watumishi watakao wapelekea majungu kwakujipendekeza na kutaka kuchonganisha watendaji na kuvuruga utendaji wa Halmashauri.

“Ajenda kuu ya Serikali hivi sasa ni ukusanyaji wa mapato, lakini pia usimamizi wa Miradi ya maendeleo ikiwepo fedha za vituo vya afya ambazo baadhi walishindwa kuzisimamia hivyo ili muweze kufanikiwa katika hili lazima mkatengeneze mahusiano   na morali miongoni mwa watumishi ili   msikwame na watu wachape kazi kwa hamasa kubwa” alisema Waziri Jafo.

Awali akitoa maneno ya utangulizi, Kaimu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mathias Kabunduguru, aliwataka wakurugenzi hao watambue huu ni mwaka wa uchaguzi wa Serikali za Mitaa hivyo wakasimamie ipasavyo zoezi la kuandikisha wapiga kura litakalo anza tarehe 08 Oktoba, 2019.

“Idadi kubwa mlioteuliwa mlikuwa watumishi katika ngazi ya mamlaka ya Serikali za Mitaa, hivyo haitakuwa kazi sana, lakini yapo yale ambayo yalikuwa yanakukera ukiwa kama Afisa Tarafa unapoagizwa na Mkurugenzi, sasa hayo usiende kuwafanyia waliochini yako bali mkafanye kazi kwa ushirikiano” Alisema Kabunduguru.

Bw. Mohamed Mavura ni miongoni mwa Wakurugenzi wapya aliyeteuliwa kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti mkoani Pwani, amesema kuwa anakwenda Kibiti akiwa anajua kabisa ipo Miradi ya Maendeleo, suala la mapato, lakini pia Uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka huu wa 2019 na Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020 hivyo ameahidi kufanya kazi kwa umoja na mshikamano kama Waziri alivyowaasa.

Wakurugenzi waliokula kiapo hicho mbele ya Afisa Mfawidhi wa Sekretarieti ya Maadili ni pamoja na Bw. Ndaki Stephano Muhuli, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Siha mkoani Kilimanjaro, Bi. Rehema Said Bwasi, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro, Bi. Sheillah Edward Lukuba, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro mkoani Morogoro, Bw. Mohamed Mavura Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti mkoani Pwani.

Wengine ni  Bw. Ezekiel Henrick Magehema, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela mkoani Mbeya, Bi. Diana Sono Zacharia, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Butiama mkoani Mara, Bi. Hanji Godigodi Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi mkoani Songwe, Bw. Said H. Magaro Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Uyui mkoani Tabora, Bi. Hawa Lumuli Mposi Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Malinyi Mkoani Morogoro, na Bw. Godwin Justin Chacha Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Rombo Mkoani Kilimanjaro.

Wakurugenzi wapya wakila kiapo cha Maadili ya viongozi wa umma.


Na. Atley Kuni- TAMISEMI.





Matangazo

  • Orodha ya waliopata vibali vya Uhamisho Septemba - Disemba 2022 (OR - TAMISEMI) January 21, 2023
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kidato cha Kwanza Waliorudia Mtihani January 15, 2023
  • Matumizi ya Lugha ya Kiswahili na Kingereza January 14, 2023
  • Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Kwanza 2023 December 14, 2022
  • Orodha ya Waliopangwa kwenye Vituo vya Kazi Kada za Afya (Awamu ya Pili) Agosti 2022 August 30, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA KWA KADA ZA AFYA (Marudio) July 20, 2022
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • LAAC YAPOKEA TAARIFA KUHUSU UTAWALA NA UENDESHAJI WA MAMLAKA ZA SERIKALI ZA MITAA

    March 14, 2023
  • SERIKALI YAWEKA MIKAKATI KATIKA USIMAMIZI WA MIRADI YA MENDELEO, UKUSANYAJI NA UDHIBITI WA MAPATO KATIKA HALMASHAURI

    March 13, 2023
  • WAUGUZI NA WAKUNGA WATAKIWA KUSIMAMIA MAADILI YA KAZI

    March 13, 2023
  • ACHENI KUTUMIANA NYARAKA ZA SERIKALI KWENYE MITANDAO YA KIJAMII NA BARUA PEPE BINAFSI - DKT. MPANGO

    March 13, 2023
  • Angalia zote

Video

Taarifa ya Ukusanyaji wa Mapato ya Halmashauri, kipindi cha robo ya pili ya mwaka wa fedha 2021/22
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.